Msaada jinsi ya kufika NACTE ukitokea Mbagala

Msaada jinsi ya kufika NACTE ukitokea Mbagala

Hahaha ni hapo hapo msimchanganye msukuma mwenzetu huyo. Akifika na ikawa sipo, atauliza walinzi hapo hapo watamuelekeza.
ʼnACTE ipo karibu na chuo cha kodi njia ya kufika ni ashuke kituo cha ITV anyooshe barabara moja kwa moja
 
Aaah bahati mbaya me nipo tandahimba na sijawahi toka huku.
 
Panda magari ya makumbusho ukifika stendi makumbusho panda magari yanayoelekea Tegeta au tabata mwambie konda akaushushe kituo cha BAMAGA ukishuka hapo vuka barabara fata ofisi za startimes ukifika TBC ujue umefika NACTE
Mkuu umemuelekeza baraza la mitihani sio NACTE kama alivyoomba
 
Nimeedit kwenye post uliyoniquote.
Fika Makumbusho kisha panda magari kati ya haya; MAKUMBUSHO kwenda TEGETA, BUNJU,KAWE UNUNIO,UBUNGO nk.
Kisha mwambie konda akushushe ITV. Ukifika ITV vuka barabara, chukua bajaji utafikishwa hadi NACTE.
Kama nauli majanga ni dk kama 20 kutoka hapo ITV Ila utapata tabu sana na hili jua, lakini Mimi nishatembea kwa mguu kama Mara tatu hivi
Ahsante, nitajitahidi nauli iwepo
 
Wazima humu wapendwa,

Samahan, naomba kuelekezwa jinsi ya kufika NACTE ukitokea mbagala, naomba kuelekezwa nipande magari ya wapi hatua kwa hatua ili nifike maana ni mgeni kabisa Dar es salaam.

Ahsanteni
chukua TAXI mwambie dereva akupeleke
 
Nimeedit kwenye post uliyoniquote.
Fika Makumbusho kisha panda magari kati ya haya; MAKUMBUSHO kwenda TEGETA, BUNJU,KAWE UNUNIO,UBUNGO nk.
Kisha mwambie konda akushushe ITV. Ukifika ITV vuka barabara, chukua bajaji utafikishwa hadi NACTE.
Kama nauli majanga ni dk kama 20 kutoka hapo ITV Ila utapata tabu sana na hili jua, lakini Mimi nishatembea kwa mguu kama Mara tatu hivi
Ubarikiwe sana, nimefika narudi sasa
 
Panda magari ya makumbusho then ukifika makumbusho panda magari ya kwenda Tegeta au bunju then waambie wakushushe ITV hapo utachukua bajaj ya shs 1000 itakupeleka mpaka geti la nacte.
Hata kutembea tu ni chini ya dk 15
 
Mkuu ukifika hapo itv kituoni unaweza kutembea tu ni chini ya dakika 15
 
Panda magari ya kivukoni ukifika panda ferry vuka upande wa pili ,kwa panton,baada ya hapo chukua bajaj ya 500 waambie unaenda gezaulole ukishuka tu ndo hapo hapo
 
Mkuu panda magari yanayoishia simu2000 then chukua boda pale waambie unaenda NACTE,buku tu,ungekuwa mwenyeji ungetembea,zipo katikati ya mwenge na ubungo,karibia na mlimani city,utaliona jengo limeandikwa NACTE..
Anakupotosha, Nenda Makumbusho kama ni kijana tembea mpaka TBC utakuwa umefika.
 
Panda magari ya kivukoni ukifika panda ferry vuka upande wa pili ,kwa panton,baada ya hapo chukua bajaj ya 500 waambie unaenda gezaulole ukishuka tu ndo hapo hapo
mkuu huko unakompeleka unataka kumtoa kafara nn...
 
Sasa kwanini usitafute kwenye google map unakuja kuuliza huku?
 
Ubarikiwe sana, nimefika narudi sasa
Nimejifunza kitu kwenye huu uzi. Ni either watu hatuna muda wa kusoma kitu tukakielewa vizuri or hatutaki kupitwa so hata kama kitu mtu hana uhakika nacho atataka tu kutia neno.
 
Panda magari ya makumbusho ukifika stendi makumbusho panda magari yanayoelekea Tegeta au tabata mwambie konda akaushushe kituo cha BAMAGA ukishuka hapo vuka barabara fata ofisi za startimes ukifika TBC ujue umefika NACTE
Wewe unampeleka NECTA, yeye anaenda NACTE.
 
Kwani we mleta mada uko ndani ya yai? Huna majirani hapo kuwauliza? Au unataka kutuaminisha mbagala mambo ya kitaaluma hakuna. Siku ntingine utakuja kutuuliza muda. Jiongeze
 
Wazima humu wapendwa,

Samahan, naomba kuelekezwa jinsi ya kufika NACTE ukitokea mbagala, naomba kuelekezwa nipande magari ya wapi hatua kwa hatua ili nifike maana ni mgeni kabisa Dar es salaam.

Ahsanteni
Nyie watu wa mikoani ebu acheni kumpoteza jamaa.
Kwenda NACTE unashuka kituo cha basi ITV kisha unachukua ile barabara ya lami na unanyooka nayo moja kwa moja mpaka chuo cha tra cha kodi, mbele kidogo Ni NACTE maeneo hayo hayo. Kwa mguu toka ITV ni kama dk 15 kwa bodaboda ni buku.
 
Panda magari ya kivukoni ukifika panda ferry vuka upande wa pili ,kwa panton,baada ya hapo chukua bajaj ya 500 waambie unaenda gezaulole ukishuka tu ndo hapo hapo
Fata maelekezo haya asikupotoshe mtu
 
Panda magari ya makumbusho then ukifika makumbusho panda magari ya kwenda Tegeta au bunju then waambie wakushushe ITV hapo utachukua bajaj ya shs 1000 itakupeleka mpaka geti la nacte.
Kwanini asipande ya Kawe akashuka My fair ?
 
Back
Top Bottom