Msaada; Jambo la mahari hufanyikaje kwa Wasukuma..?

Msaada; Jambo la mahari hufanyikaje kwa Wasukuma..?

makaghari

JF-Expert Member
Joined
Jun 20, 2014
Posts
544
Reaction score
530
Habari za jumapili ndugu zangu..!

Katika mihangaiko ya hapa na pale suala la familia ni muhimu. Nipo katika harakati za kuyafanya mahusiano yangu na binti wa kisukuma kufikia hatua ya ndoa. Jambo linalonifanya nije hapa jukwaani naomba mnisaidie mambo yafuatayo maana huyu binti kwa kiasi Fulani taratibu za kikwao hazifahamu vyema.

1. Katika kumtolea mahari binti wa kisukuma ni mambo gani huambatanishwa na tukio hilo..?

2. Tofauti na mahari, ni gharama gani/vitu gani vinvine ambavyo natakiwa kuviandaa kama sehemu muhimu ya kukamilisha tukio hilo..?

Nitafurahi endapo nitapata mwongozo kutoka kwenu.. Hasa kwa wanaozifahamu taratibu za wasukuma wa sengerema.
 
- Kitenge cha shangazi
- Kikoi cha babu
- Koti la baba
- Zawadi ya mama
Mahari huwa haimalizwi usukumani
 
- Kitenge cha shangazi
- Kikoi cha babu
- Koti la baba
- Zawadi ya mama
Mahari huwa haimalizwi usukumani
Ahsante kwa dondoo ndugu. Kwanini umesema huwa haimalizwi..?
 
Wasukuma hatunaga mbwembwe nyiiingi..tunataka ngombe zamiguu au za hela..so jipange mkuu..
 
ngombe wawili wa maziwa au shilingi milioni mbili
 
Mjulisheni na ng’ombe zisizo za miguu kwa sasa ni shilingi ngapi thamani ya ng’ombe mmoja! Last time dada yangu ameolewa ilikuwa ng’ombe 16. 10 za miguu (really cows) na 6 zilikuwa za hela (cows converted to money) so that time ng’ombe mmoja ilikuwa ni elfu hamsini - therefore ng’ombe unazotaka kutoa kwa hela unapiga hesabu kila ng’ombe elfu hamsini. But I’m sure bei itakuwa imeongezeka maana kitambo sipo Tanzania na sijaongea na wasukuma wenzangu juu ya current price!
 
Ahsante kwa dondoo ndugu. Kwanini umesema huwa haimalizwi..?
Tunaamini ukimaliza mahari yote ni sawa na tumekuuzia mtoto. So mfano tukakwambia mahari million 2 na wewe ukatoa nusu yani millioni 1 hiyo nyingine haina ulazima uimalize yote unaweza toa laki 4,5,6,7 ingine ukapotezea lakini hiyo ni kwa wanyantuzu siongelei wote!..
 
Tunaamini ukimaliza mahari yote ni sawa na tumekuuzia mtoto. So mfano tukakwambia mahari million 2 na wewe ukatoa nusu yani millioni 1 hiyo nyingine haina ulazima uimalize yote unaweza toa laki 4,5,6,7 ingine ukapotezea lakini hiyo ni kwa wanyantuzu siongelei wote!..
Ahsante kwa ufafanuzi Mkuu.
 
Back
Top Bottom