Msaada - interview ofisi ya bunge

Msaada - interview ofisi ya bunge

Holota

Senior Member
Joined
Feb 20, 2022
Posts
114
Reaction score
91
"Habari za kila mtu, naomba msaada wenu. Nimeona mwezi wa 5 kuna watu walifanya usaili wa nafasi ya Afisa Usimamizi wa Fedha Daraja la II kwenye Ofisi ya Bunge. Je, mtu anaweza kunipa ufafanuzi au kushiriki uzoefu wake kuhusu mtindo wa usaili, maswali au maandalizi yanayohitajika? Asanteni mapema!"
 
Hiyo ni normal tu jiandae kulingana na nafasi kutoboa ni uhakika.
Vp mkuu we ulifanya nipate tu hints za written interview inakuaje kwa upande wa maswali ni mfumo ule wa apptitude test au coverage ya masomo husika eg finance
 
Maandalizi kwa sasa ni kujuana.
Wanaita "connection"
Umeifunga mada mkuu.

Mwezi wa 6 kama sikosei, ililetwa taharuki ya ajira za 'Fire' hapa mkoani!

Vijana wakaunga tela la interview, rukishwa sana vichura na mabio ya masafa marefu, watu kama 500'iv!

Kuja kusikia kumbe alikuwa anatakiwa mmoja tu, ndonikachoka kabisa mie😀😀😁.

Na aliyechaguliwa ni mtu wao, ona sasa!

Yaani kuhalalisha nafasi moja mpaka iwatoe jasho wengine 499!

Kwa kweli tulipofikia sasa, bila connection mtoto wako hata usomesheje, hafiki popote.
 
Back
Top Bottom