Wakuu swali la nyongeza. Hivi dawa ya Amoeba inatibu pia minyoo Just in case nayo ipo tumboni?
Jamani mwenzenu kwa muda mrefu nimekuwa nikisumbuliwa na tumbo na kila nikipima naambiwa nina amoeba na madawa nimetumia aina zote lakini sijapata naafuu yoyote,msaada kwa anayejua tiba kamili nawasilisha.
sawaInawezekana kabisa huwa unapona huo ugonjwa baada ya kutumia dawa lkn baadaye unapata tena maambukizi mapya.Epuka kutumia kachumbali za kwenye bar au kwa mama ntilie kwani wao wanatumia maji yasiyo salama.Pia hakikisha kuwa unakunywa maji safi na salama sivyo utakuwa unatwanga maji kwenye kinu.Kuhusu dawa ili kukata mzizi wa fitna meza SECNIDAZOLE vidonge viwili kila siku kwa muda wa siku tatu.