Heshima kwenu wakuu wa kazi,<br />
Nashukuru kwa maoni yenu mengi ya msaada. Nafurahi kuwajulisha kwamba pc imepona na sasa inapiga kazi kama kawaida. Nilichofanya? Hakuna!! Ila jana baada ya kuhangaika kwa muda mrefu bila mafanikio, nliamua tu kuiacha hiyo pc ili leo niishughulikie. Kusema kweli hata haijanisumbua kama nlivokuwa nimeiandaa. Nimeiwasha ikawaka vizuri tu na scanner pia ikafanya kazi. Nahisi ilichanganyikiwa kidogo ikawa inahitaji muda wa kujipanga upya. Labda na mimi nilikurupuka tu, hata celewi!!! <br />
Anyway..... Asanteni tena & nawatakia siku njema.<br />
FK