Msaada: Biashara ya viatu kwa mtaji wa laki

Msaada: Biashara ya viatu kwa mtaji wa laki

Deejay nasmile

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2011
Posts
5,817
Reaction score
5,403
Kwa tsh 100,000 naweza kufanya biashara ya viatu,sendo za wadada?

1. Nahitaji kuanza kufanya hii biashara kwa kuanzia na mtaji wa laki moja tu. Nipate viatu, sendo, simpo za wadada au wakaka niuze Kwa bei ya kawaida tu (chini ya elfu 7).

Kama kuna wauzaji humu wa bei ya jumla karibuni. Bidhaa ziwe nzuri na ambazo ziko sokoni(zinazotrend)

Bei iwe nzuri ili nikiuza nipate faida nzuri angalau nusu kwa nusu..

Nipo Dodoma
 
Kuna watu na Viatu...wewe unauza viatu vipi?
images%20(1).jpg
 
Ongeza mtaji kidogo...




Cc: mahondaw
Sawa mkuu niongeze kama shi ngapi...lakini lengo ni kulisoma soko kwanza ndio maana sikutaka kuweka mtaji mkubwa sana...pia sitategemea biashara hiyo..nataka nijazie hapa katika frem yangu ambayo inadili na biashara nyingine
 
Jumatatu mzigo huwa unafunguliwa kariakoo ule mtaa wa viatu, wanachangiana pieces wanachukua box

Ukienda pale unaweza kuchek kwa pesa uliyo nayo utapata pieces ngapi
 
Kwa mtaji ulionao kwa viatu vya mchina kidogo utapata pc chache sana mana bei ya pc 1 huwa shilingi elfu tatu au elfu moja na miatano ila kwa viatu unavyotaka kuuza wewe unatakiwa upate vile vya sh elfu tatu hadi elfu tatu na miatano ndio vizuri hivyo unatakiwa ujiongeze.

Ila mtaji huo huo unaweza kufanya biashala ya viatu vya mtumba ambavyo ukienda karume pale ni kupointi na bei huwa ni sh elfu moja hadi elfu na miatano na ndio biashala ambayo hata ukiwa na mtaji wa elfu hamsini unatoboa mana kile kimoja ukishakiweka sawa unauza hadi elfu 8 ndio biashala ambayo niliifanya mwaka jana mwanzoni ila kwa sasa nimeacha ila ni biashala ambayo ni ya uhakika si unaona pale mwenge wanauza mpka elfu 15 kiatu cha buku jero kalume
 
jumatatu mzigo huwa unafunguliwa kariakoo ule mtaa wa viatu,
wanachangiana pieces wanachukua box

ukienda pale unaweza kuchek kwa pesa uliyo nayo utapata pieces ngapi
Ubarikiwe dada mfano ukitaka kuchanga uchukue unatakiwa uwaone wa kina Nani na muda SAA ngapi
 
Nenda pale mtaa wa viatu vya mchina kariakoo kuna kina aina ya viatu new brands na bei zao ni reasonable kwa mkoani unaweza kuuza zaidi ya mara mbili yake.Zaidi njoo PM nina experience kidogo na biashara ya viatu vya spesho na mtumba pia.
 
Nenda mwenge kwa sapro maasai kiatu pair moja 4,500 vya kike vya kiume 6,500 vya watoto 3,000

Unaweza kuchukua vya kike 10 (4,500x10= 45,000)
Vya kiume 5 (6,500x5= 32,500)
Vya watoto 5 (3,000x5= 15,000)

TOTAL =92,500

Kwenye 100,000 inabaki 7,500 hiyo kianzio ya kutembea maji kidogo, nauli

Faida it depends na bei za wateja wako

Kama vya kike unaweza kuuza 10,000-7,000 faida kwenye 5,500 kwa 2,500 kwa pair 10 faida itakua kati ya 55,000 kwa 25,000

Vya kiume 15,000 kwa 12,000 faida 8,500 kwa 5,500

Vya watoto 7,000 kwa 5,000 faida 4,000 kwa 2,000

Nb: chukua vya kike vingi sababu wanawake ndio wanawanunua wengi usikopeshe kwasababu ndio unaanza hadi pale mtaji ukikaa sawa ndio unakopesha mtu analipa buku buku kila siku au unakopesha kwa week week

Au nenda kkoo mtaa wanaouza viatu vingiii ddc kwa mbele kidogo kuna maduka ya ndani ndaniii na chini kuna viatu vya jumla vingiii vizuri chagua vya sasa kuna vya 2,500/2,700/3,000 kuna vya 6,000/7,000 vya kichina lakini

Unamix vya bei ndogo na vya bei ya kati
 
Nenda mwenge kwa sapro maasai kiatu pair moja 4,500 vya kike vya kiume 6,500 vya watoto 3,000

Unaweza kuchukua vya kike 10 (4,500x10= 45,000)
Vya kiume 5 (6,500x5= 32,500)
Vya watoto 5 (3,000x5= 15,000)

TOTAL =92,500

Kwenye 100,000 inabaki 7,500 hiyo kianzio ya kutembea maji kidogo, nauli

Faida it depends na bei za wateja wako

Kama vya kike unaweza kuuza 10,000-7,000 faida kwenye 5,500 kwa 2,500 kwa pair 10 faida itakua kati ya 55,000 kwa 25,000

Vya kiume 15,000 kwa 12,000 faida 8,500 kwa 5,500

Vya watoto 7,000 kwa 5,000 faida 4,000 kwa 2,000

Nb: chukua vya kike vingi sababu wanawake ndio wanawanunua wengi usikopeshe kwasababu ndio unaanza hadi pale mtaji ukikaa sawa ndio unakopesha mtu analipa buku buku kila siku au unakopesha kwa week week

Au nenda kkoo mtaa wanaouza viatu vingiii ddc kwa mbele kidogo kuna maduka ya ndani ndaniii na chini kuna viatu vya jumla vingiii vizuri chagua vya sasa kuna vya 2,500/2,700/3,000 kuna vya 6,000/7,000 vya kichina lakini

Unamix vya bei ndogo na vya bei ya kati
Nataman nikutafte tuyajenge kuhusu business aisee , unaniruhusu nikuvae PM?
 
Back
Top Bottom