Mkuu inategemea kwanza unahtaji dagaa wa aina gani kuna wale wasiokuwa na mchanga pia wanakuwa wanaanikwa kwenye vichanja au sehem nyingine ambapo kunakuwa na miamba hawawezi kutengeneza chanja wanakuwa wanaanika kwenye nyasi. pili kuna wale wa mchanga wanakuwa wanaanikwa chini kwenye mchanga na pia wapo wa kukaanga. uzito kwa gunia huwa inategemeana na aina ya dagaa kuna ambao debe moja ni wastan wa {kg 4.2 had 4.2} hawa ni wakutoka visiwa vya bukoba kama vile Gozba, Lushonga NK.. na pia wapo Wakutoka visiwa vya mwanza na mialo ya nchi kavu kama vile ukerewe, bwiro, mchangani, kijiweni NK... hawa kwa wastani uzito wake huwa ni kuanzia {kg 3.8 had 4.2} kwa hiyo uzito kwa gunia hutegemea sanasana aina ya gunia au ujazoHabari za majukumu wakuu, naomba kufahamu bei ya gunia la dagaa wakavu toka mwanza, musoma au bukoba na gunia ilo lina kg ngapi. Biashara hii nataka kuifanya iringa hivyo naomba kujua na gharama za usafirishaji