Mrudishe mahabuba ngamani

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,850
Reaction score
831,121
Angalizo: Sifundishi watu ndumba kila mtu ana uhuru wake na wote tu watu wazima ninachofanya ni kushiriki ninachokifahamu.

Mapenzi ni kitu kinachoendesha dunia kwenye ulimwengu wa roho na hisia. Mtu asiye na mapenzi ni kama zimwi litishalo si mnyenyekevu hana huruma hana utu hana hisia ni katili na mwenye rohombaya.

Kuna wakati wapendwa wetu tunaowapenda sana na kuwathamini hutekwa na kuchukuliwa na wengine kwa njia za kishetani huyu waweza mrudisha kwenye himaya yako.

Kivipi?Kama una hakika umeporwa Chanda chako kwa ndumba fanya hiviTafuta mafuta ya mzeituni mzizi au jani la mkafiri

i

Unyoya wa tausi au chiriku chumvi ya mabonge kitambaa cha cotton cheusi na chekundu uzi mweusi au mwekundu chungu kidogo picha nguo au chochote cha umpendae.

Changanya vyote pamoja kisha pondaponda pamoja na chungu chake funga kwenye vitambaa cheusi na chekundu kwa kamba na pini katupe mtoni kwenye maji ya alfajiri huku ukinuizia.
 
Duu hii mbinu kama itafanya kazi ngoja nikamuopoe Rihanna ananiumiza kichwa kishenzi

Hahahaaa inafanya kazi tu kwa mwenye mahusiano ya kimahaba nawe
 
Nnahakika pm Leo zitakuhusu sana hapa, maana wabongo kwa kuamini mambo hayo hatujambo
 
kuna mheshimiwa bungeni namzimia hataree na picha zake zilivyozagaa kwenye magazeti loh!
 
Changanya vyote pamoja kisha pondaponda pamoja na chungu chake funga kwenye vitamba cheusi na chekundu kwa kamba na pini katupe mtoni kwenye maji ya alfajiri huku ukinuizia

Umetisha mkuu
 
Haa haa ya leo kariiii...mi kuna mtu namzimikia kinoma ila hayuko hapa nchini, nafanyaje mkuu?
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…