SIKU chache kupita tangu kuibuka kwa Mjumbe wa Baraza Kuu UVCCM Taifa, MRISHO GAMBO, kumtaka aliyekuwa Mwenyekiti wa (UVCCM), James Millya kurudisha fedha za SACCOS ya jumuiya hiyo, Sh. Milioni 2, Katibu wa Umoja huo amekanusha madai hayo na kusema UVCCM haijawahi kuw ana mradi wa SACCOS.
Katibu wa Umoja wa Vijana Mkoa wa Arusha, Abdallah Mpokwa, amesema hayo jana mjini hapa alipokuwa katika kikao cha kamati ya utekelezaji Baraza Kuu la UVCCM, Mkoa wa Arusha, kilichojumuisha Wenyeviti na Makatibu wa wilaya zote za Mkoa wa Arusha.
Mpokwa pia alikanusha suala la Millya kutakiwa kukabidhi ofisi mara alipoondoka na kujiunga na CHADEMA ambapo alisema Millya, kisheria hakuwa na ofisi ila alikuwa na kazi ya kufungua mikutano na vikao ila kikanuni za umoja wao Mtendaji na mwenye ofisi ni KATIBU, hivyo tuhuma hiyo haimuhusu Millya.
Ninachosema haya matamko yanatolewa na watu tusiowatambua katika UMOJA wetu, huyu GAMBO alishafukuzwa katika kikao chetu tulichofanya LONGIDO na hatumtabui anatoa matamko kama nani,alihoji MPOKWA.
Katibu wa Umoja wa Vijana Mkoa wa Arusha, Abdallah Mpokwa, amesema hayo jana mjini hapa alipokuwa katika kikao cha kamati ya utekelezaji Baraza Kuu la UVCCM, Mkoa wa Arusha, kilichojumuisha Wenyeviti na Makatibu wa wilaya zote za Mkoa wa Arusha.
Mpokwa pia alikanusha suala la Millya kutakiwa kukabidhi ofisi mara alipoondoka na kujiunga na CHADEMA ambapo alisema Millya, kisheria hakuwa na ofisi ila alikuwa na kazi ya kufungua mikutano na vikao ila kikanuni za umoja wao Mtendaji na mwenye ofisi ni KATIBU, hivyo tuhuma hiyo haimuhusu Millya.
Ninachosema haya matamko yanatolewa na watu tusiowatambua katika UMOJA wetu, huyu GAMBO alishafukuzwa katika kikao chetu tulichofanya LONGIDO na hatumtabui anatoa matamko kama nani,alihoji MPOKWA.