Mashaurijr
JF-Expert Member
- Oct 8, 2016
- 639
- 1,020
Wakuu nakuja tena kwenu nikiwa nimechoka sana. Ngoja ninywe hata juice nipate nguvu ya kuwasimulia yaliyonikuta na yanayoendelea kunikuta.
Ilikuwa mwaka jana mwezi wa 11 nilipokutana na mwanamke mmoja mrembo sana. Kwa hakika kila idara alijaliwa, makalio, hipsi, sura hakuna mwanaume ambaye asingetamani kuwa naye.
Alikuwa maeneo ya karibu na biashara zangu akiuza kiduka alichodai ni cha mama yake mkubwa. Kila siku nilijaribu kumweka karibu ila tatizo likawa sio mimi peke yangu niliyekuwa namfukuzia yule mrembo.
Ila mwisho wa siku nikaibuka mshindi mrembo akanasa, na siyo kidogo, akanasa kweli kweli kufikia hatua ya kuwa na wivu wa hali ya juu, hakutaka kabisa nikaribiwe na mwanamke mwingine yeyote.
Nilijiona mjanja sana na mwenye bahati hapo hata kumwonja mrembo ilikuwa bado. Ni kama kuna hisia zilikuwa zinanikatalia kumpeleka maskani nikajipongeze baada ya kuhangaika sana kumpata mrembo.
Nilifikiria sana kwanini naingia kibaridi na kiwoga cha ajabu kila ninapotaka kumpeleka mrembo maskani ila nikakosa jibu. Maana siyo mara yangu ya kwanza kutoka na mrembo mkali kama yeye useme ni kiwewe.
Zilikatika siku nyingi tukiwa wapenzi akionesha kabisa matamanio ya kupekwa maskani tukafanye yetu lakini mwamba bado nilizuiwa na hisia, nikikwepa kwepa kwa visingizio vidogo vidogo.
Siku ya mwaka mpya nilikunywa sana, sasa mrembo akafanya kunisindikiza akiwa na rafiki yake baada ya kukaribia maskani. Rafiki yake akamwambia anifikishe yeye anaongea na simu kidogo atamkuta, bila mimi kujua walikuwa wameshapanga tayari.
Basi mrembo akanifikisha mpaka maskani nikijua ataishia nje lakini wapi aliingia maskani, tukalala, nikampiga kimoko cha kilevi asubuhi game ndio ikachezwa haswaa. Licha ya kibaridi cha asubuhi wote tukawa tunatoka jasho mithili ya mtu anayelima kwenye jua kali.
Siku hiyo tulichelewa kufungua biashara mpaka tukazua minongono mtaani. Wakijiuliza na kujijibu wenyewe angali sisi wenye majibu kamili tukiwepo.
Sasa baada ya hapo ikatokea mtafaruku upande wake baada ya mume wa mama yake mkubwa kuanza kulazimisha mapenzi kwa mrembo bila yeye kutaka, vitendo hivyo vilimfikia mama mkubwa wake na kuamua mrembo arudi kijijini. Tena akimfukuza usiku na mrembo hakuwa na kwakwenda akaniomba aje alale kesho yake aondoke.
Kweli mrembo alikuja lakini hakuondoka tena, akakaa na mimi mwezi wa kwanza ukaisha salama japokuwa nilianza kumgundua ana mambo ya giza ndani yake, tuseme mapepo, ila sikuamini kama ni mchawi.
Mpaka juzi mdogo wangu alipougua nikashtuka sana, nikaanza kuwa mtu tofauti, nikaanza kumwomba Mungu. Hapo ndio nilipoanza kuoneshwa matendo ya ajabu ya mrembo niliyeishi naye kama mke.
Alikuwa na mizimu ya kichawi ndani yake, alikuwa akifanya mengi kwa kutumia uchawi wake bila mimi kujua. Hata usiku nikishalala yeye hubaki kama boshen tu ila nafsi yake huondoka kwenda kwenye vikao vya wachawi usiku.
Itaendelea sehemu ya pili...
Muendelezo sehemu ya pili soma hapa
Ilikuwa mwaka jana mwezi wa 11 nilipokutana na mwanamke mmoja mrembo sana. Kwa hakika kila idara alijaliwa, makalio, hipsi, sura hakuna mwanaume ambaye asingetamani kuwa naye.
Alikuwa maeneo ya karibu na biashara zangu akiuza kiduka alichodai ni cha mama yake mkubwa. Kila siku nilijaribu kumweka karibu ila tatizo likawa sio mimi peke yangu niliyekuwa namfukuzia yule mrembo.
Ila mwisho wa siku nikaibuka mshindi mrembo akanasa, na siyo kidogo, akanasa kweli kweli kufikia hatua ya kuwa na wivu wa hali ya juu, hakutaka kabisa nikaribiwe na mwanamke mwingine yeyote.
Nilijiona mjanja sana na mwenye bahati hapo hata kumwonja mrembo ilikuwa bado. Ni kama kuna hisia zilikuwa zinanikatalia kumpeleka maskani nikajipongeze baada ya kuhangaika sana kumpata mrembo.
Nilifikiria sana kwanini naingia kibaridi na kiwoga cha ajabu kila ninapotaka kumpeleka mrembo maskani ila nikakosa jibu. Maana siyo mara yangu ya kwanza kutoka na mrembo mkali kama yeye useme ni kiwewe.
Zilikatika siku nyingi tukiwa wapenzi akionesha kabisa matamanio ya kupekwa maskani tukafanye yetu lakini mwamba bado nilizuiwa na hisia, nikikwepa kwepa kwa visingizio vidogo vidogo.
Siku ya mwaka mpya nilikunywa sana, sasa mrembo akafanya kunisindikiza akiwa na rafiki yake baada ya kukaribia maskani. Rafiki yake akamwambia anifikishe yeye anaongea na simu kidogo atamkuta, bila mimi kujua walikuwa wameshapanga tayari.
Basi mrembo akanifikisha mpaka maskani nikijua ataishia nje lakini wapi aliingia maskani, tukalala, nikampiga kimoko cha kilevi asubuhi game ndio ikachezwa haswaa. Licha ya kibaridi cha asubuhi wote tukawa tunatoka jasho mithili ya mtu anayelima kwenye jua kali.
Siku hiyo tulichelewa kufungua biashara mpaka tukazua minongono mtaani. Wakijiuliza na kujijibu wenyewe angali sisi wenye majibu kamili tukiwepo.
Sasa baada ya hapo ikatokea mtafaruku upande wake baada ya mume wa mama yake mkubwa kuanza kulazimisha mapenzi kwa mrembo bila yeye kutaka, vitendo hivyo vilimfikia mama mkubwa wake na kuamua mrembo arudi kijijini. Tena akimfukuza usiku na mrembo hakuwa na kwakwenda akaniomba aje alale kesho yake aondoke.
Kweli mrembo alikuja lakini hakuondoka tena, akakaa na mimi mwezi wa kwanza ukaisha salama japokuwa nilianza kumgundua ana mambo ya giza ndani yake, tuseme mapepo, ila sikuamini kama ni mchawi.
Mpaka juzi mdogo wangu alipougua nikashtuka sana, nikaanza kuwa mtu tofauti, nikaanza kumwomba Mungu. Hapo ndio nilipoanza kuoneshwa matendo ya ajabu ya mrembo niliyeishi naye kama mke.
Alikuwa na mizimu ya kichawi ndani yake, alikuwa akifanya mengi kwa kutumia uchawi wake bila mimi kujua. Hata usiku nikishalala yeye hubaki kama boshen tu ila nafsi yake huondoka kwenda kwenye vikao vya wachawi usiku.
Itaendelea sehemu ya pili...
Muendelezo sehemu ya pili soma hapa