Helo wana jamii amani iwe nanyi,mimi ni mwanaume ambaye nimekuwa katika mahusiano ya kimapenzi na binti mmoja kwa muda wa miaka 2, nampenda sana na December mwaka huu nilitaka kumwoa.Wiki tatu zilizopita alinieleza kuwa ni mjamzito na haikunipa shida maana niliona ni jambo la kheri.Lakini cha ajabu alinieleza msimamo wake kuwa anataka kutoa hiyo mimba na nilikataa kukubaliana nae na kumwambia kuwa akitoa asahau kuwa na mimi.Baada ya hapo alikubaliana nami kuilea,lakini baadae akawa hataki kuzungumzia chochote juu ya ujauzito wake pindi nilipotaka kujua maendeleo yake na ukafika wakati akawa hapokei simu yangu na akawa hapatikani na hata akipokea simu hunijibu kauli mbaya jambo lililonipa wasiwasi wa kuwa huenda ametoa.Wiki iliyopita alikuwa anakata simu na wakati wote simu ilikuwa inaita tuu jambo lililonipa hasira ya mimi kutomtafuta tena mpaka sasa ni siku ya 3 sijaongea naye na yeye hajanitafuta.Naomba ushauri wenu ili nijue kama bado au ametoa hiyo mimba maana mimi nipo Dar na yeye yupo Mwanza likizo.