Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 361,100
- 831,745
Baada ya miezi miwili na ushee ya kupost mada za ubunifu kwenye majukwaa mbalimbali hasa jukwaa la makazi na ujenzi na kidogo ujasiriamali.. Hatimaye picha zimeanza kupungua sasa
Dhima ya hizi mada ilikuwa kuamshq udadisi, kuchagiza ubunifu na kusherehesha sanaa ya ubunifu kwenye majukwaa tajwa.. Lakini zaidi ilikuwa ni kuondoa mazoea ya kupost mada zilezile wakati wote na kwa vitu vilevile... Nje ya hayo ilikuwa kutengeneza database ya bank ya picha za ubunifu kwa kutumia malighafi za kawaida ikiwemo zilizokwisha tumika na kuwekwa kwenye kundi la uchafu..
Hii haikuwa kazi ndogo bali ilikuwa kazi ngumu nzito iliyohitaji muda, utulivu na nyenzo.. Ilikuwa ni rahisi zaidi kubuni kichwa cha habari kuliko kupata maudhui yake ambayo kwa asilia miamoja yalikuwa ni picha.. Lingine ilikuwa ni uchaguzi sahihi wa picha zinazoendana na kichwa cha habari
Kuna wakati hapa na pale nilifanya makosa kwa kuchanganya picha lakini kwakuwa ufuatiliaji wa wanajukwaa ulikuwa mdogo niliweza kugundua na kurekebisha mwenyewe wakati mwingine kwa kuchelewa kidogo
Mwitikio wa wanajukwaa kwa baadhi ya post ulikuwepo lakini kadiri mapicha yalivyozidi kuporomoka weengi waliichoka mada haraka..
Hili halikuwa tatizo sana kwakuwa muktadha haukuwa uchangiaji bali kutengeneza database, hivyo ilihitajika kupost picha nyingi kwelikweli na hayo majukwaa yakaanza kupata uhai zaidi
Baada ya kuanza kupata mwitikio mzuri ndio nikaja sasa na mada ya wabunifu wa JF ..
Hii ilikuwa sasa ni kwa ajili ya kuwavuta wote kwa pamoja na kuona kama tunaweza kufanya kitu kwanza kwa nadharia na pili kwa vitendo! Hapa mwtikio ukawa ni wa kawaida hivyo nikaishia kupost mapicha randomly
Kuna feedback nilizipata lakini ni members waliotaka kuwa na baadhi ya picha kwa matumizi yao wenyewe! Mirejesho ya waliotaka kufanya ubunifu katika uhalisia wake ulikuwa ni almost sifuri!
Bado sijakata tamaa kwakuwa tayari mbegu imeshapandwa na kuanza kuchipuka! Hatua ijayo ni mada za ubunifu lakini hatua kwa hatua mpaka kitu kikamilike. Yaani kama ni kutengeneza kinyago cha mpapure ni maelezo ya hatua kwa hatua kuanzia vitendea kazi, malighafi mpaka vipimo..
Kwenye mapicha mengi ya ubunifu, baadhi ya bunifu zilikuwa za kijinga😁 kama ile ya njiti za viberiti,.. Lakini kwakuwa ubunifu hauna mipaka basi sio kesi..
Haya ndio machache na kwa ufupi yaliyotokana na mada za ubunifu... Naamini sasa mmeanza kupata picha
Asanteni sana,, siku hizi sirogi tena😁
www.jamiiforums.com
Dhima ya hizi mada ilikuwa kuamshq udadisi, kuchagiza ubunifu na kusherehesha sanaa ya ubunifu kwenye majukwaa tajwa.. Lakini zaidi ilikuwa ni kuondoa mazoea ya kupost mada zilezile wakati wote na kwa vitu vilevile... Nje ya hayo ilikuwa kutengeneza database ya bank ya picha za ubunifu kwa kutumia malighafi za kawaida ikiwemo zilizokwisha tumika na kuwekwa kwenye kundi la uchafu..
Hii haikuwa kazi ndogo bali ilikuwa kazi ngumu nzito iliyohitaji muda, utulivu na nyenzo.. Ilikuwa ni rahisi zaidi kubuni kichwa cha habari kuliko kupata maudhui yake ambayo kwa asilia miamoja yalikuwa ni picha.. Lingine ilikuwa ni uchaguzi sahihi wa picha zinazoendana na kichwa cha habari
Kuna wakati hapa na pale nilifanya makosa kwa kuchanganya picha lakini kwakuwa ufuatiliaji wa wanajukwaa ulikuwa mdogo niliweza kugundua na kurekebisha mwenyewe wakati mwingine kwa kuchelewa kidogo
Mwitikio wa wanajukwaa kwa baadhi ya post ulikuwepo lakini kadiri mapicha yalivyozidi kuporomoka weengi waliichoka mada haraka..
Hili halikuwa tatizo sana kwakuwa muktadha haukuwa uchangiaji bali kutengeneza database, hivyo ilihitajika kupost picha nyingi kwelikweli na hayo majukwaa yakaanza kupata uhai zaidi
Baada ya kuanza kupata mwitikio mzuri ndio nikaja sasa na mada ya wabunifu wa JF ..
Hii ilikuwa sasa ni kwa ajili ya kuwavuta wote kwa pamoja na kuona kama tunaweza kufanya kitu kwanza kwa nadharia na pili kwa vitendo! Hapa mwtikio ukawa ni wa kawaida hivyo nikaishia kupost mapicha randomly
Kuna feedback nilizipata lakini ni members waliotaka kuwa na baadhi ya picha kwa matumizi yao wenyewe! Mirejesho ya waliotaka kufanya ubunifu katika uhalisia wake ulikuwa ni almost sifuri!
Bado sijakata tamaa kwakuwa tayari mbegu imeshapandwa na kuanza kuchipuka! Hatua ijayo ni mada za ubunifu lakini hatua kwa hatua mpaka kitu kikamilike. Yaani kama ni kutengeneza kinyago cha mpapure ni maelezo ya hatua kwa hatua kuanzia vitendea kazi, malighafi mpaka vipimo..
Kwenye mapicha mengi ya ubunifu, baadhi ya bunifu zilikuwa za kijinga😁 kama ile ya njiti za viberiti,.. Lakini kwakuwa ubunifu hauna mipaka basi sio kesi..
Haya ndio machache na kwa ufupi yaliyotokana na mada za ubunifu... Naamini sasa mmeanza kupata picha
Asanteni sana,, siku hizi sirogi tena😁
JF all creators: Jukwaa mahususi la wabunifu wa JamiiForums
Ni weekend nyingine ya mwezi wa pili mwaka 2025 inaishia.. Wenye kazi zao wako kwenye maandalizi ya kuwahi kesho kazini.. Tusio na kazi kesho ni siku nyingine ya upweke na simanzi nyingine..😪 Niwatie moyo sana na tusikate tamaa.. Elimu tulipata itusaidie tuweze kujimudu kimaisha kupitia...