Mrejesho: Tayari nimeshatoa maamuzi

Mrejesho: Tayari nimeshatoa maamuzi

JembePoli

JF-Expert Member
Joined
Jul 14, 2015
Posts
1,324
Reaction score
999
Habari wanajamvi pendwa MMU,

Naomba niwashukuru wote mlionichangia ushauri kwenye kisa changu cha kweli "njia panda (nimuoe yupi anaenipenda au ninaempenda?) Jana ndio ilikuwa siku ya maamuzi saa7:00 usiku nilipoamua kufanya maamuzi,Niliwashilikisha watu wazima na kuwasimulia kama nilivyoileta kwenu na wakapenda wawepo wakati wa tukio.

Kaka na mzee mmoja jirani yake pamoja na mzee Limo ambae ni jirani yangu walikuwa tayari wapo ndani ya sebule yangu kusikiliza nitakavyotoa maamuzi kuhusu yupi nimeamua nimuoe.Nakumbuka mpenzi wangu wa kwanza alifika 7:20 alishanga kuona ugeni pale kwani sio kawaida lakini nilimtoa wasi wasi na wa pili alifika 7:31 kama sijakosea,(mapigo ya moyo wangu hapa yalibadilika mno)

Lakini nilishangaa kidogo baada ya kuona hakushtuka (ikumbukwe hakuna aliekuwa akijua ameitiwa nini)
Suprise ilikuwa ikini suprise mwenyewe.Nakumbuka ni mzee Limo alieanza kuwambia wale mabinti (wapenzi wangu) kwa kuwauliza 'Nyie walembo mnajua mualiko wenu unahusu nini?

Kwa pamoja walijibu hawajui akawapa swali tena nyie huyo 'huku akininyoshea mkono' ni nani yenu? Hapo walisita na kutizamana kwa pamoja wakajibu ni rafiki yetu.Mzee akawapa tena,rafiki yenu kivipi kwani nyinyi mnajuana?
Hapo majibu ndio yalinivuruga kwani iko hivi.Wa kwanza alianza kusimulia.

Nimemjua jembepoli miaka 3 iliyopita ni mpenzi wangu tangu 2012 lakini alikuja kubadilika mwaka 2013 mwanzoni japo kila nikimuuliza sababu za kubadilika alikuwa akinijibu wasi wasi wangu tu yeye yuko sawa,lakini kwa sababu mimi namfahamu vizuri nikajua kuna tatizo nikaanza kumfuatilia kwa uchunguzi wa kimya kimya nikaja kugundua amempata msichana mwingine,'iliniumiza kwa kweli' lakini kwa kuwa nikataka kujua zaidi sikutaka kumuuliza nikapanga nimtafute msichana mwenzangu ili nae niongee nae kupata uhakika,jembepoli hakubadilika alikuwa akinipa mapenzi moto moto kila ninalotaka alinipa.

Nakumbuka ilikuwa 2014 mwezi wa 7 nilipofanikiwa kukutana na mke mwenzangu pale alipokuwa anatoka kazini kwa kweli alikuwa mstaarabu na nikamueleza kuhusu mahusiano aliyonayo kuwa tunashere mume akaniomba achunguze kama ni kweli nikampa namba yangu ya simu kwa kweli alikuwa ananipa ushilikiano kwani nilikuwa najua uko wapi nae anajua kama uko kwangu 'hapa alinitazama kwa mala ya kwanza tangia aanze kusimulia,kwa aibu mwanaume nikakwepa na kujiinamia)

Basi tukapanga mimi na (alitaja jina) mke mwezangu tukutane tuongee na ndio tukakubaliana siku moja tumuite tuongee nae na achague mmoja Kati yetu kwani mwenzangu alidai amejaribu kumkasirikia ili awe mbali nae lakini ameshindwa na kujikuta anaumia na kushindwa kufanya kazi na mambo yake na hapa naomba niwaweke wazi kuna siku waligombana mimi nikaenda kwa(akataja jina) mke mwenzangu alikuwa mnyoge na kama anaumwa hivi ikabidi tukubaliane mimi na mke mwenzangu tu.

Kuwa kwa kuwa tumegundua JembePoli Hana mtu mwingine zaidi yetu basi tuache mpaka mwenyewe atakapoamua itakavyokuwa kwani hakuna tunachokosa kwake tukawa marafiki bila mume wetu kujua kuwa tunajuana,nakumbuka kuna siku alishtuka kuona tumevaa nguo sare lakini hakujua kuwa ule ni mpango ambao sisi tuliupanga kuona nini anawaza (niliwahi kuileta mada hii hapa Jf kwa bandiko.sijui wamejuana wameshona sare)
Lakini naona mwenzetu hakugungua hivyo ndivyo ilivyo baba Angu.

Akamaliza kusimulia wa kwanza na mzee Limo akamgeukia mpenzi wangu wa pili ambae alikuwa amejiinamia na kumuuliza eti ni kweli mamaa aliinua kichwa na kuona ni jinsi gani alivyokuwa analia kimya kimya (hata mimi nilijisikia vibaya) ndio ni kweli mzee! Alijibu.Mzee Limo alitugeukia sisi na kutuuliza/kuniuliza jamani nyie mnasemaje.

Bro bila kupepesa akasema hapa hakuna cha tunasemaje aseme anamtaka yupi na tuende tukapose maana tabia wameshajuana kaka angu yupo na umri kama 40+ mjeshi kwa hiyo amri ni kawaida.Kwa upole nikajibu nawapenda wote lakini kwa kuwa ni la zima nioe mmoja basi Nikamchagua mpenzi wangu wa pili lakini nikawa nimepiga magoti kwa mpenzi wangu wa kwanza anisamehe kwa yote pamoja na uamuzi wangu.

Kabla hajasema lolote mzee Limo pamoja na mzee aliekuja na bro wakamuuliza mchumba wangu wa pili unasemaje?
Mchumba wangu aliomba apewe muda akajifikilie kwani ni kweli ananipenda sana lakini anashindwa kutoa maamuzi kwa muda ule pale.Nashukuru mpenzi wangu wa kwanza alinisamehe kwani niliomba msamaha kwa kumaanisha mzee nilipiga magoti huku mchozi ukitililika mbele ya kikao.

Leo mpaka saivi sijaamka na sijui mpenzi wangu niliemchagua kama atakuja na jibu la kukubali au kukataa lakini nimejiandaa kwa yote na pia bro kasema Mahari yote atalipa yeye(japo mimi sijashindwa)Nawashukuru sana kwa ushauri wenu ulionijenga.Ndefu lakini isome tu.
 
The Bible says "You shall know truth n the Truth shall set You Free" hapo umemaliza Utata. Hongera Jamaa. Ila Ujifunze kutulia Ukipata MTU Anaekupenda na Uliyempenda kwa Dhati.. Who knows next tym Unaweza ukapoteza Wote.
 
The Bible says "You shall know truth n the Truth shall set You Free" hapo umemaliza Utata. Hongera Jamaa. Ila Ujifunze kutulia Ukipata MTU Anaekupenda na Uliyempenda kwa Dhati.. Who knows next tym Unaweza ukapoteza Wote.

Ahsante mkuu,
Saivi nimeshaamua naoa kabisaa na natulia Kujenga mustakabali wa maisha yangu na mke wangu mtarajiwa.
 
Ahsante mkuu,
Saivi nimeshaamua naoa kabisaa na natulia Kujenga mustakabali wa maisha yangu na mke wangu mtarajiwa.

ukiuwa kwa upanga utakufa kwa upanga. Nakuapia jinsi ulivomzalilisha huyo dada kwa kwanza mbele ya watu ivo ivo sio leo au kesho au kesho kutwa utakuja kulia mara mia hadharani.

Kwanza wewe ni mjinga sana yaani uliona haitoshi ikabidi umkane mbele ya watu ulishindwa nn kumwambia mwenyewe? Mjinga mkubwa yaan ulijua kuwa unachaguo lako ukaone umzalilishe ivo? Mshenzi kweli kweli

. Baada ya mwaka tutaona uzi wa machozi hapa.
 
ukiuwa kwa upanga utakufa kwa upanga. Nakuapia jinsi ulivomzalilisha huyo dada kwa kwanza mbele ya watu ivo ivo sio leo au kesho au kesho kutwa utakuja kulia mara mia hadharani.

Kwanza wewe ni mjinga sana yaani uliona haitoshi ikabidi umkane mbele ya watu ulishindwa nn kumwambia mwenyewe? Mjinga mkubwa yaan ulijua kuwa unachaguo lako ukaone umzalilishe ivo? Mshenzi kweli kweli

. Baada ya mwaka tutaona uzi wa machozi hapa.

Hahahahah umeandika kwa hasira.

Baadhi ya wanaume ndio walivyo nilishawahi kukutana nayo hii ya kuachwa mbele ya wazazi wa mwanaume na kumchagua wa pili, hadi navyoandika hapa jitu linalia lia hovyo kwa ndugu zangu eti turudiane.

Inaumiza sana kwa kweli, hapa ni kusamehe tu na kumuacha Mungu atende yake
 
What a man! Yaani ilibidi uwaite wote wawili ndo utoe maamuzi? Uneitwa wewe na mume mwenzio kisha ukaibuka wewe kidedea ingejisikiaje? Uwiiii mbuuuuraaaa!
 
Duuh after 3 good years she shared with you and this how you paid her back . Remember she refused to have other men because she believed you were the one . How can you do that to her ? She must be broken now even though you said she forgave you . Dear you had a chance to talk to her private soon after you knew where your heart was . I have really learn something here ( That don't date a man for too long ). Dear just remember what goes around always comes around . Thanks .
 
Naona kama uliyemchagua nae atakuja na jibu la kukutosa.....maana ukiwa na mwingine utamuacha yeye na kumchukua wa tatu.......
 
Aisee mwanaume ni mdhalilishaji mno wat u did for her itakurudia
 
Hivi hii ni kweli au? Binadamu hatupaswi kufanyiana hivi unless useme umri wako ni mdogo kiasi usiwe na maamuzi tena unaishi kwa wazazi. Na hata kama umri wako ni mdogo kwa nini ulijiingiza kwenye mapenzi? (hapa najaribu kujijibu mwenyewe) man what you did was unfair mdada atakua kajifeel bad sana
 
Yaani hapo maamuzi yalikuwa ni nani awe njia kuu ya kudumu na nani awe mchepuko wa kudumu.
 
Hongera ila kibongo bongo sijui kama utaachana na huyo number 1. Unaweza kuta ndo mchepuko wako sasa

Hapana sitajihusisha na hiyo kitu kwa sasa ni ndoa tu na mustakabali wa maisha yangu mapya.
Mkuu
 
Mkuu kwa vile hao walifahamiana muda mrefu na wanaongea kama marafiki,
hivyo tegemea jibu la kukataliwa kwani hatoweza kujisikia vizuri kwa kumsaliti mwenzake kwa mipango yao.
 
ukiuwa kwa upanga utakufa kwa upanga. Nakuapia jinsi ulivomzalilisha huyo dada kwa kwanza mbele ya watu ivo ivo sio leo au kesho au kesho kutwa utakuja kulia mara mia hadharani.

Kwanza wewe ni mjinga sana yaani uliona haitoshi ikabidi umkane mbele ya watu ulishindwa nn kumwambia mwenyewe? Mjinga mkubwa yaan ulijua kuwa unachaguo lako ukaone umzalilishe ivo? Mshenzi kweli kweli

. Baada ya mwaka tutaona uzi wa machozi hapa.

Najua kwa Hali ya kawaida nitakuwa nimewaudhi watu wengi hasa wanawake ndio maana hata msamaha wangu sikupenda niuombe tukiwa wawili tu,
Kuomba msamaha mbele ya watu unaowaheshimu inaleta maana unajutia kosa lako ndio maana hata muhusika alikubali kusamehe.
Plz nisamehe pia kama nimekuudhi kwa maamuzi yangu kwa mwanamke mwenzio.
 
Hahahahah umeandika kwa hasira.

Baadhi ya wanaume ndio walivyo nilishawahi kukutana nayo hii ya kuachwa mbele ya wazazi wa mwanaume na kumchagua wa pili, hadi navyoandika hapa jitu linalia lia hovyo kwa ndugu zangu eti turudiane.

Inaumiza sana kwa kweli, hapa ni kusamehe tu na kumuacha Mungu atende yake

Aisee pole bila shaka utusamehe huwa ni ngumu hata kwetu pia kimaamuzi lakini msamaha pekee
 
What a man! Yaani ilibidi uwaite wote wawili ndo utoe maamuzi? Uneitwa wewe na mume mwenzio kisha ukaibuka wewe kidedea ingejisikiaje? Uwiiii mbuuuuraaaa!

Haina jinsi muda mwingine ni vema kuukubali ukweli.
 
Back
Top Bottom