Habari zenu wadau wa MMU, jana nilileta mada ya kutaka ushauri jinsi ya kumtokea mtoto mmoja hivi aliekuwa anauumiza mtima wangu baada ya kusoma ushauri wa wachangiaji waliotoa mawazo yao sasa huu ndio mrejesho niliowaahidi kuuleta baada ya kukamilisha zoezi.
Baada ya kusoma maoni mbalimbali ya wadau nikachukua uamuzi wa kumuandikia kimemo ambacho nimeambatanisha na namba yangu ya simu. Mwanaume baada kumaliza shughuli zangu za kila siku nikashika njia kurejea home huku nikiwa na Kimemo changu mfukoni nikafika maeneo ya yule bint anapoishi daah bahati mbayanikakuta shazi nje kwaona yeye akiwepo watu km wanne hv akiwemo dada yake pamoja na mzee mmoja wa makamo basi ikabidi nipitilize nikaishia kutoa salamu tu, moyo ukaniuma sana nikasema haiwezekani hata njia hii inishinde km vipi subiri nikajilipue km mbwai mbwai tu.....nikaenda kwanza mpaka home nikachange Nguo nikasema subiri nirudi hata km akiwa na ndugu zake ntamuita pembeni nimkabidhi alaf nisepe....nikaanza safari ya mafanikio moyo wa uwoga nikauto nikafika eneo la tukio Mungu si athuman nikakuta shazi limepunguaa akawa amebaki yeye na bint mmoja mdogo nadhani ni mtoto wa dada yake mwanaume kufika pale nikamsalimu nikamwambia dada samahani nina ujumbe wako, bint akashtuka mimi? nikamwambia ndio huku natoa kimemo changu mfukoni nikamkabidhiakapokea kidume huyo sikutaka hata kusubiri nikasepa huku nikiwa najiona nimetua bonge la mzigo kichwani kweli mapenzi balaa.........
Sasa basi wadau kufika mida flani hivi naiti napiga story na wanafamilia wangu home mara sms inaingia kuangalianamba ngeni....
Mambo...
nikajibu Poa....
ujumbe wako nimeupata...nikamwambia fresh hii ndio namba yako?.......kanijibu ndio...basi baada ya hapo story nyingine ziliendelea kidogo tukaagana.
Kwa hiyo mazee mdau wenu sijawaangusha nimetekeleza jambo mtoto sasa yupo kiganjani hapa sasa mimi tu kama samaki ndo nshamvua chaguo langu nimkaange, nimbanike, nimuunge supu au mchuzi wa chukuchuku.
AHSANTENI SAAAAAAAAAAAAAAANAAAAAAAAAA[/QUOT
Wasiwas wangu mkuu asijekuwa member wa JF akajua karata nzima mkuu! Anyway kila la kheri mkuu! Safar moja huanzisha nyingine!