Mrejesho juu ya kesi yangu

scientificall

JF-Expert Member
Jun 4, 2015
454
314
Kwanza nimushukuru Mungu kwa kuonesha haki na kutenga ukweli na uongo.

Nichukue pia fursa hii kuwashukuru wanajamvi wote hasa waliotoa mawazo, ushauri na kutoa pridiction juu ya kesi yangu. Mawazo yenu na ushauri nimeutumia kwa 100% mpaka kushinda kesi.


Kabla sijatoa nlilokusudia ngoja ntoe maelezo kiufupi juu ya kesi iiyokuwa ikinikabili......
" toka mwezi wa 3 mwaka huu. Kuna jirani alinituhumu kuwa nilimuibia computer na simu 2 jumla gharama ya tsh 950000/-

Uongozi wa chuo ulinitishia sana ili nikubali tuhuma niweze kulipa na mwisho kufukuzwa chuo kwani mshitaki alidai alinishuhudia mimi usiku nikiwa na wenzangu tuna muibia. Kwa kudhani angeweza kulipwa harakaharaka kutokana na vipesa nilivyokuwa ninavyo vya mkopo.

Mwisho mbele ya mwanasheria wa chuo nilikana na kesi yangu ikapelekwa polisi na kuwekwa mahabusu siku 4 na kisha kupandishwa kizimbani katika mahakama ya mwanzo.


Kesi hii iliniathiri sana kisaikolojia kwani hata mtaani iliniaribia sifa kwani mshitaki alikuwa akintangaza kuwa mimi ni mwizi. Iliniuma sana mpaka ikapelekea mimi kuumwa na kuharibika kwa ratiba zangu za masomo kipindi chote cha kulindima kwa kesi.
Kesi ilichukua miezi 2.5 kuisha mpaka 1.6.2018 kesi ilihukumiwa kama ifuatavyo

" mshitaki umeshindwa kuithibitishia mahakama juu ya mshitakiwa, hivyo mahakama imejiridhika kuwa mshitakiwa huna hatia yoyote, hivyo basi kuanzia sasa mshitakiwa uko huru"........hapo ndo tulitoka nje na kuondoka.



USHAURI WENU:
1.Ni vipi ninaweza kufungua mashitaka ya kuomba fidia maana huyu mtu kanifanya niishi na stress ambazo sijawahi zipata.
2. Je akikata rufaa kwa kukosa kwake ushahidi inaweza mfanya ashinde kesi? .



Naombeni ushauri kwani huyu mtu kansababishia madhara ya kiakili na ghara zisizo za lazima.
 
Kwanza nimushukuru Mungu kwa kuonesha haki na kutenga ukweli na uongo.

Nichukue pia fursa hii kuwashukuru wanajamvi wote hasa waliotoa mawazo, ushauri na kutoa pridiction juu ya kesi yangu. Mawazo yenu na ushauri nimeutumia kwa 100% mpaka kushinda kesi.


Kabla sijatoa nlilokusudia ngoja ntoe maelezo kiufupi juu ya kesi iiyokuwa ikinikabili......
" toka mwezi wa 3 mwaka huu. Kuna jirani alinituhumu kuwa nilimuibia computer na simu 2 jumla gharama ya tsh 950000/-

Uongozi wa chuo ulinitishia sana ili nikubali tuhuma niweze kulipa na mwisho kufukuzwa chuo kwani mshitaki alidai alinishuhudia mimi usiku nikiwa na wenzangu tuna muibia. Kwa kudhani angeweza kulipwa harakaharaka kutokana na vipesa nilivyokuwa ninavyo vya mkopo.

Mwisho mbele ya mwanasheria wa chuo nilikana na kesi yangu ikapelekwa polisi na kuwekwa mahabusu siku 4 na kisha kupandishwa kizimbani katika mahakama ya mwanzo.


Kesi hii iliniathiri sana kisaikolojia kwani hata mtaani iliniaribia sifa kwani mshitaki alikuwa akintangaza kuwa mimi ni mwizi. Iliniuma sana mpaka ikapelekea mimi kuumwa na kuharibika kwa ratiba zangu za masomo kipindi chote cha kulindima kwa kesi.
Kesi ilichukua miezi 2.5 kuisha mpaka 1.6.2018 kesi ilihukumiwa kama ifuatavyo

" mshitaki umeshindwa kuithibitishia mahakama juu ya mshitakiwa, hivyo mahakama imejiridhika kuwa mshitakiwa huna hatia yoyote, hivyo basi kuanzia sasa mshitakiwa uko huru"........hapo ndo tulitoka nje na kuondoka.



USHAURI WENU:
1.Ni vipi ninaweza kufungua mashitaka ya kuomba fidia maana huyu mtu kanifanya niishi na stress ambazo sijawahi zipata.
2. Je akikata rufaa kwa kukosa kwake ushahidi inaweza mfanya ashinde kesi? .



Naombeni ushauri kwani huyu mtu kansababishia madhara ya kiakili na ghara zisizo za lazima.
.
 
Back
Top Bottom