kikoozi
JF-Expert Member
- Jun 24, 2015
- 2,030
- 2,929
Habarini za siku ndugu zangu, poleni na majukumu ya hapa na pale,
Baada ya kuleta uzi kuusiana na maswahiba ya mpenzi wangu kubadilika ghafla, na kwa upande wangu kujaribu kujua kinachomtatiza ila yeye ananiambia yupo sawa tu wakati kihualisia namuona amebadilika kabisa kabisa.
Baada ya kusoma michango yenu ikanibidi nimtafute huyu mpenzi wangu wa kike, kwa nia ya kutaka kujua tu nini kipo nyuma ya pazia cha kumfanya awe katika hali ile, nilimbana sana mwishoni aliongea sentence hii " kuna shida sehemu ila nipe muda siwezi kukuambia leo, niache nipe muda kwanza"--hapa ndipo nilipozidi kumbana ili nijue shida ipo wapi, ila ndugu zangu sikufanikiwa maana alisimamia kauli yake hiyo hiyo kuwa atakuja kuniambia mbeleni, nimekaa nae miaka 4 sikumzoea hivyo alivyo sasa, amebadilika ghafla
Baada ya kuona amekataa sana kunieleza nilimuambia kauli mbili
1. Nilimuambia kama anashindwa kuniambia tatizo nini mimi kama mpenzi wake, basi sitoweza kuwa na amani na haya mahusiano.
2. Nilimuambia ombi lake la kutaka nimpe muda nimelikubali, " nakuacha uende, siku ukiona unaweza niambia utanitafuta, ukiona hauwezi niambia nakutakia kila la kheri huko uendako"
Baada ya kauli hiyo nimefuta mawasiliano yake kila sehemu.
Ni siku ya tano leo "hajanitafuta kabisa, baada ya kumuambia hivyo"
Nilipanga nimuoe mwakani, ila ndio ndege ameshapeperuka, nilimpenda na ninampenda kutoka moyoni hata hapa naumia ila sitarudi nyuma kwenye haya maamuzi
Asanteni kwa mawazo yenu, Mungu awabariki sana
Baada ya kuleta uzi kuusiana na maswahiba ya mpenzi wangu kubadilika ghafla, na kwa upande wangu kujaribu kujua kinachomtatiza ila yeye ananiambia yupo sawa tu wakati kihualisia namuona amebadilika kabisa kabisa.
Baada ya kusoma michango yenu ikanibidi nimtafute huyu mpenzi wangu wa kike, kwa nia ya kutaka kujua tu nini kipo nyuma ya pazia cha kumfanya awe katika hali ile, nilimbana sana mwishoni aliongea sentence hii " kuna shida sehemu ila nipe muda siwezi kukuambia leo, niache nipe muda kwanza"--hapa ndipo nilipozidi kumbana ili nijue shida ipo wapi, ila ndugu zangu sikufanikiwa maana alisimamia kauli yake hiyo hiyo kuwa atakuja kuniambia mbeleni, nimekaa nae miaka 4 sikumzoea hivyo alivyo sasa, amebadilika ghafla
Baada ya kuona amekataa sana kunieleza nilimuambia kauli mbili
1. Nilimuambia kama anashindwa kuniambia tatizo nini mimi kama mpenzi wake, basi sitoweza kuwa na amani na haya mahusiano.
2. Nilimuambia ombi lake la kutaka nimpe muda nimelikubali, " nakuacha uende, siku ukiona unaweza niambia utanitafuta, ukiona hauwezi niambia nakutakia kila la kheri huko uendako"
Baada ya kauli hiyo nimefuta mawasiliano yake kila sehemu.
Ni siku ya tano leo "hajanitafuta kabisa, baada ya kumuambia hivyo"
Nilipanga nimuoe mwakani, ila ndio ndege ameshapeperuka, nilimpenda na ninampenda kutoka moyoni hata hapa naumia ila sitarudi nyuma kwenye haya maamuzi
Asanteni kwa mawazo yenu, Mungu awabariki sana