Nebuchadinezzer
JF-Expert Member
- Oct 1, 2018
- 1,403
- 2,550
Ni matumaini yangu mmeamka salama kama Mimi. Mlioamka vibaya, Mungu awasimamie siku yenu iwe nzuri.Bila kupoteza wakati naanza kutiririka yaliyomo moyoni mwangu.
Siku chache zilizopita nilileta Uzi humu nikielezea jinsi nilivyomkumbuka X wangu Hajir ambae tuliachana kisa linimzaba kofi moja la kikurya baada ya kumkuta anachati na jamaa. Nashukuru watu wengi walinishauri niongee nae ikiwezekana tuyajenge ili hali yetu irudi kama zamani. Kwa kuwa nampenda Hajir, niliamua kumtafuta hadi kwenda kwao ili niweze kuyajenga nirudishe furaha yangu. Yaliyonikuta huko kwao mpaka kesho sitasahau...kumbe wanawake ni ny*k* kiasi hicho!
Huyu mjinga si amechumbiwa na ndoa yake mwezi wa kumi. Yaani nilipoambiwa hivyo na brother wake Ali nilijihisi kama vile nimefungiwa mzigo mzito mdomoni. Sikuwa na la kuzungumza zaidi ya kuchuruzikwa na machozi ya hasira. Mbaya zaidi nasikia anaolewa na Kei.
Kei ndo wa kunifanyia hivyo Mimi? Kei mshikaji wangu nimepiga naye O level. Na ndiye aliyekuwa ananambia kuwa Hajir ni kama vile hajatulia. Ndo Kei huyu huyu mtoto wa mama Kei. Ambaye nilikuwa na msaidia kwenye masomo. Dah, watu hawanashukurani hata kidogo!!
Sasa nimeamua kumove on na maisha yangu. Nahisi kwa sasa nahitaji mtoto tu; sitaki kuishi na kiumbe anayeitwa mwanamke. Maana nikiishi na mwanamke yeyote ntakuwa najidanganya tu maana Hajir peke yake ndiye mwanamke ninaempenda japokuwa kanitenda. Anyway, kwenye ndoa yake nimepanga kumpelekea zawadi kupitia kwa rafiki yake Aisha. Naamini akiipata hiyo zawadi, atajua Mimi pekee ndiye ninae mpenda kuliko hata mama yake anavyompenda.
Asanteni muwe na Siku njema.
Siku chache zilizopita nilileta Uzi humu nikielezea jinsi nilivyomkumbuka X wangu Hajir ambae tuliachana kisa linimzaba kofi moja la kikurya baada ya kumkuta anachati na jamaa. Nashukuru watu wengi walinishauri niongee nae ikiwezekana tuyajenge ili hali yetu irudi kama zamani. Kwa kuwa nampenda Hajir, niliamua kumtafuta hadi kwenda kwao ili niweze kuyajenga nirudishe furaha yangu. Yaliyonikuta huko kwao mpaka kesho sitasahau...kumbe wanawake ni ny*k* kiasi hicho!
Huyu mjinga si amechumbiwa na ndoa yake mwezi wa kumi. Yaani nilipoambiwa hivyo na brother wake Ali nilijihisi kama vile nimefungiwa mzigo mzito mdomoni. Sikuwa na la kuzungumza zaidi ya kuchuruzikwa na machozi ya hasira. Mbaya zaidi nasikia anaolewa na Kei.
Kei ndo wa kunifanyia hivyo Mimi? Kei mshikaji wangu nimepiga naye O level. Na ndiye aliyekuwa ananambia kuwa Hajir ni kama vile hajatulia. Ndo Kei huyu huyu mtoto wa mama Kei. Ambaye nilikuwa na msaidia kwenye masomo. Dah, watu hawanashukurani hata kidogo!!
Sasa nimeamua kumove on na maisha yangu. Nahisi kwa sasa nahitaji mtoto tu; sitaki kuishi na kiumbe anayeitwa mwanamke. Maana nikiishi na mwanamke yeyote ntakuwa najidanganya tu maana Hajir peke yake ndiye mwanamke ninaempenda japokuwa kanitenda. Anyway, kwenye ndoa yake nimepanga kumpelekea zawadi kupitia kwa rafiki yake Aisha. Naamini akiipata hiyo zawadi, atajua Mimi pekee ndiye ninae mpenda kuliko hata mama yake anavyompenda.
Asanteni muwe na Siku njema.