Mgeni wa Jiji
JF-Expert Member
- Jul 27, 2017
- 7,919
- 13,394
Habari wana jamvi
Leo ni wiki ya kwanza tangu tuanze matumizi ya kinga 'condom' katika ndoa yetu, kama mtakumbuka mwaka jana nilileta uzi kuhusu jambo hili, labda nikumbushe kuwa nia yangu ya kuanza matumizi ya kinga katika ndoa ni kujikinga na maradhi kama ukimwi!
Usishituke ndiyo 'ukimwi' baada ya kukaa na kutafakari sana niliona kuwa ni rahisi kuupataukimwi ndani ya ndoa kuliko hata nje ya ndoa (amini usiamini hili ni wazi) basi mimi nikaona kwanini hili linikute kirahisi hivyo nikaamua kuja na mbinu za kiafya kabisa kujilinda
Nikiri tu haikuwa jambo rahisi hata kidogo ila nililifanikiwa baada ya maongezi marefu na kuoneshamsimamo wangu juu ya umuhimu wa afya yangu na yake pia, bila ugomvi tulikubaliana
Siku ya kwanza:
Sikutoa taarifa za kuanza kutumia kinga basi mimi nilizinunua nkazileta nyumbani, bahati mbaya au nzuri niliziweka mahali pasipo wazi sana basi mke akaziona, akazichukua akaziweka kwenye meza ndogo ya kitanda hamadi nikazikuta na swali juu 'Umetoa wapi hizi!!?' Siku panic nikajibu hizi za kwetu, aisee haikuwa jambo jepesi hata kidogo
Siku ya pili:
Tulizitumia na tendo tukalifurahia
Siku ya tatu:
Akanikumbusha kuhusu kinga, sasa sijajua ni kunitega au kujilinda pia nikaona poa tu nikaamua nunua bokisi kabisa
Siku ya nne:
Utani ukarudi, mke akaanza kunitania juu ya kinga tukataniana sana juu ya hicho kitu kinga, basi tukafurahia pamoja mapenzi yetu mapya ya kutumia kinga
Siku ya tano hadi sasa:
Mapenzi yetu yameimarika zaidi sasa tunayafurahia zaidi na zaidi kwa kweli nimefarijika na mke anafurahia hali yetu hii mpya
Nawasihi waungwana wenzangu kinga ni bora kuliko tiba mbaya zaidi hii kitu haina tiba, TUTUMIE KINGA HADI NDOANI WAUNGWANA.
Leo ni wiki ya kwanza tangu tuanze matumizi ya kinga 'condom' katika ndoa yetu, kama mtakumbuka mwaka jana nilileta uzi kuhusu jambo hili, labda nikumbushe kuwa nia yangu ya kuanza matumizi ya kinga katika ndoa ni kujikinga na maradhi kama ukimwi!
Usishituke ndiyo 'ukimwi' baada ya kukaa na kutafakari sana niliona kuwa ni rahisi kuupataukimwi ndani ya ndoa kuliko hata nje ya ndoa (amini usiamini hili ni wazi) basi mimi nikaona kwanini hili linikute kirahisi hivyo nikaamua kuja na mbinu za kiafya kabisa kujilinda
Nikiri tu haikuwa jambo rahisi hata kidogo ila nililifanikiwa baada ya maongezi marefu na kuoneshamsimamo wangu juu ya umuhimu wa afya yangu na yake pia, bila ugomvi tulikubaliana
Siku ya kwanza:
Sikutoa taarifa za kuanza kutumia kinga basi mimi nilizinunua nkazileta nyumbani, bahati mbaya au nzuri niliziweka mahali pasipo wazi sana basi mke akaziona, akazichukua akaziweka kwenye meza ndogo ya kitanda hamadi nikazikuta na swali juu 'Umetoa wapi hizi!!?' Siku panic nikajibu hizi za kwetu, aisee haikuwa jambo jepesi hata kidogo
Siku ya pili:
Tulizitumia na tendo tukalifurahia
Siku ya tatu:
Akanikumbusha kuhusu kinga, sasa sijajua ni kunitega au kujilinda pia nikaona poa tu nikaamua nunua bokisi kabisa
Siku ya nne:
Utani ukarudi, mke akaanza kunitania juu ya kinga tukataniana sana juu ya hicho kitu kinga, basi tukafurahia pamoja mapenzi yetu mapya ya kutumia kinga
Siku ya tano hadi sasa:
Mapenzi yetu yameimarika zaidi sasa tunayafurahia zaidi na zaidi kwa kweli nimefarijika na mke anafurahia hali yetu hii mpya
Nawasihi waungwana wenzangu kinga ni bora kuliko tiba mbaya zaidi hii kitu haina tiba, TUTUMIE KINGA HADI NDOANI WAUNGWANA.