Mwachiluwi
JF-Expert Member
- Mar 10, 2022
- 17,796
- 32,148
HANDSOME BOYS...
SONGA NAYO...........
"Maisha yangu yamekuwa ya mapito mateso na furaha pia, vyote vimekuwa vikichukua nafasi katika maisha yangu na kunifanya niwe imara na kuwa na furaha za kuwa mpambanaji Zaidi katika maisha yangu, ukiwageni umeishi maisha ya vipindi tofauti tofauti yaani Leo uzuni kesho furaha hayo tunasema Ni maisha.
Kwa majina naitwa Edna nyerere mtoto wa pekee kabisa kwa mama yangu na baba yangu, Mungu aliwajaalia mtoto mmoja tu, lakini pia akatupatia maisha ya kawaida mno sio matajili, lakini pia alitufungulia njia ya kipato kidogo ambacho kilikuwa kikikidhi maitaji yetu madogo madogo, nakumbuka wimbo mkubwa kwa mama yangu ilikuwa Ni Edna soma sana hauna urithi, nimekuwa na malezi ya upande mmoja baada ya baba yangu kufariki nikiwa darasa la nne, lakini hiyo haikuwa sababu ya mama kukata tamaa kwasababu aliamini kuwa Mimi Niko upande wake, lakini pia hakuitaji Tena kuolewa au kuanzisha mahusiano mengine mama alikuwa allimpenda Sana baba angu.
Nakumbuka ilikuwa 2019 matokea ya kidoto Cha sita yalipotoka, nilikuwa jikoni nikipika mama akaja na kunikumbatia kwa nyuma uku machozi yakimtoka sana niliogopa niliwaza mama amepatwa na nini, niligeuka haraka na kumuuliza
"Kuna Nini mbona unanitisha ..??"
"Silii kwa uzuni nalia kwa furaha Edna hiko kichwa Ni Cha baba yako kabisa ingawa alifariki na elimu yake bila kupata kazi lakini naimani wewe utashika Hadi nafasi zake, hongera sana mwanangu umefauru kwenda chuo kikuu Tena kwa ufahuru mzuri kabisa "
Nyie nilikuwa na akili flani hivi ya kijinga yaani akili yangu ilikuwa Moto Sana sikumkumbatia mama Wala Nini nilitoka nje nikiwa napiga kelele Kama nimechangayikiwa, mbele ya nyumba yetu Kuna kiwanja kikubwa tu kina michanga ya kutosha SI unajua Tena jiji la dar kwa michanga, nilitoka nje na kuanza kuruka ruka nikipiga kelele nikalala chini na kugalagala uku na uku sikujali ya kuwa nachafuka au laah! Nilikuwa na furaha ambayo aielezeki, uswazi Ni uswazi tu watu walijaa na kuanza kunishangaa nikigalagala kila mtu aliongea lake
"Au amepandisha mashetani maana huyu mtoto nae"
"Amechanganyikiwa au??"
Kila mtu alisema analolijua sikuwa nikiwasikiliza mie nikabaki kushangilia ushindi wangu.
Mama akatoka ndani haraka akaona Sasa nataka kuwa chizi maana sio kwa ushangiliaji ule
"Haya inatosha amka hapo"
Nilistuka hatari na kuinuka, nilipokuwa nagalagala pale chini sikuwa nikiwaona vizuri Nyie nilipoinuka walikuwa wengi niliona aibu ya hatari nikainuka na kurudi ndani haraka, nikaingia bafuni na kuoga, Kisha kurudi jikoni.
Siku ziliendelea kusonga huku nikiqgaikia Mambo ya mikopo kwaajili ya chuo, na kwakuwa nilisoma ST. KAYUMBA kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato Cha sita ilinisaidia sana kupata mkopo, na nilifanikiwa kuchaguliwa kwenye chup kikuu Cha dar es salaam yaani UDSM furaha ikangezeka nilikuwa nakitaka Sana hiko chuo nilikuwa na wenge la kuanza chuo tu.
Mama alikuwa ameifadhi pesa zake akanipatia nikafanye shopping ya nguo Kama mjuavyo kile chuo kwa mavazi kama wako kwenye mashindano, nikafanya shopping yangu uchwara pale ya kawaida kwani haikuwa pesa kubwa Sana hivyo nyingi zilikuwa za mtumba, nilichojali kuwa Ni nguo mpya na pesa nimepewa na mama yangu.
Siku ya kuanza chuo iliwadia ilikuwa ni siku ya usajili kila mtu alikuwa mwenyewe isipokuwa Mimi ambaye nilikuja na mama yangu maana mama alitoa ahadi kuwa siku yangu ya kwanza chuoni lazima atanipeleka, mwanzo wanafunzi wengine walijua kuwa mama Ni mwanafunzi SI unajua elimu aina mwisho, lakini walipokuja kujua kuwa Ni mama yangu amenileta walicheka sana na kisema kuwa Mimi Ni mtoto wa mama, nilijisikia vibaya lakini mama alikuwa pale na kunifanya nione kuwa ni Mambo ya kawaida Sana niwaache waongee tu.
Usajili ulikamilika na kulikuwa na wiki Moja ya orientation, baada ya wiki hiyo kuisha rasmi tukaingia kwenye masomo, kwakuwa nilikuwa nikijua darada langu Ni lipi haikunipa shida Moja kwa Moja nikaingia kwenye darasa langu, nilikutana na watu tofauti tofauti wamependeza na wengi walionekana kuwa na maisha mazuri, niliingia nakukaa
SONGA NAYO...........
"Maisha yangu yamekuwa ya mapito mateso na furaha pia, vyote vimekuwa vikichukua nafasi katika maisha yangu na kunifanya niwe imara na kuwa na furaha za kuwa mpambanaji Zaidi katika maisha yangu, ukiwageni umeishi maisha ya vipindi tofauti tofauti yaani Leo uzuni kesho furaha hayo tunasema Ni maisha.
Kwa majina naitwa Edna nyerere mtoto wa pekee kabisa kwa mama yangu na baba yangu, Mungu aliwajaalia mtoto mmoja tu, lakini pia akatupatia maisha ya kawaida mno sio matajili, lakini pia alitufungulia njia ya kipato kidogo ambacho kilikuwa kikikidhi maitaji yetu madogo madogo, nakumbuka wimbo mkubwa kwa mama yangu ilikuwa Ni Edna soma sana hauna urithi, nimekuwa na malezi ya upande mmoja baada ya baba yangu kufariki nikiwa darasa la nne, lakini hiyo haikuwa sababu ya mama kukata tamaa kwasababu aliamini kuwa Mimi Niko upande wake, lakini pia hakuitaji Tena kuolewa au kuanzisha mahusiano mengine mama alikuwa allimpenda Sana baba angu.
Nakumbuka ilikuwa 2019 matokea ya kidoto Cha sita yalipotoka, nilikuwa jikoni nikipika mama akaja na kunikumbatia kwa nyuma uku machozi yakimtoka sana niliogopa niliwaza mama amepatwa na nini, niligeuka haraka na kumuuliza
"Kuna Nini mbona unanitisha ..??"
"Silii kwa uzuni nalia kwa furaha Edna hiko kichwa Ni Cha baba yako kabisa ingawa alifariki na elimu yake bila kupata kazi lakini naimani wewe utashika Hadi nafasi zake, hongera sana mwanangu umefauru kwenda chuo kikuu Tena kwa ufahuru mzuri kabisa "
Nyie nilikuwa na akili flani hivi ya kijinga yaani akili yangu ilikuwa Moto Sana sikumkumbatia mama Wala Nini nilitoka nje nikiwa napiga kelele Kama nimechangayikiwa, mbele ya nyumba yetu Kuna kiwanja kikubwa tu kina michanga ya kutosha SI unajua Tena jiji la dar kwa michanga, nilitoka nje na kuanza kuruka ruka nikipiga kelele nikalala chini na kugalagala uku na uku sikujali ya kuwa nachafuka au laah! Nilikuwa na furaha ambayo aielezeki, uswazi Ni uswazi tu watu walijaa na kuanza kunishangaa nikigalagala kila mtu aliongea lake
"Au amepandisha mashetani maana huyu mtoto nae"
"Amechanganyikiwa au??"
Kila mtu alisema analolijua sikuwa nikiwasikiliza mie nikabaki kushangilia ushindi wangu.
Mama akatoka ndani haraka akaona Sasa nataka kuwa chizi maana sio kwa ushangiliaji ule
"Haya inatosha amka hapo"
Nilistuka hatari na kuinuka, nilipokuwa nagalagala pale chini sikuwa nikiwaona vizuri Nyie nilipoinuka walikuwa wengi niliona aibu ya hatari nikainuka na kurudi ndani haraka, nikaingia bafuni na kuoga, Kisha kurudi jikoni.
Siku ziliendelea kusonga huku nikiqgaikia Mambo ya mikopo kwaajili ya chuo, na kwakuwa nilisoma ST. KAYUMBA kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato Cha sita ilinisaidia sana kupata mkopo, na nilifanikiwa kuchaguliwa kwenye chup kikuu Cha dar es salaam yaani UDSM furaha ikangezeka nilikuwa nakitaka Sana hiko chuo nilikuwa na wenge la kuanza chuo tu.
Mama alikuwa ameifadhi pesa zake akanipatia nikafanye shopping ya nguo Kama mjuavyo kile chuo kwa mavazi kama wako kwenye mashindano, nikafanya shopping yangu uchwara pale ya kawaida kwani haikuwa pesa kubwa Sana hivyo nyingi zilikuwa za mtumba, nilichojali kuwa Ni nguo mpya na pesa nimepewa na mama yangu.
Siku ya kuanza chuo iliwadia ilikuwa ni siku ya usajili kila mtu alikuwa mwenyewe isipokuwa Mimi ambaye nilikuja na mama yangu maana mama alitoa ahadi kuwa siku yangu ya kwanza chuoni lazima atanipeleka, mwanzo wanafunzi wengine walijua kuwa mama Ni mwanafunzi SI unajua elimu aina mwisho, lakini walipokuja kujua kuwa Ni mama yangu amenileta walicheka sana na kisema kuwa Mimi Ni mtoto wa mama, nilijisikia vibaya lakini mama alikuwa pale na kunifanya nione kuwa ni Mambo ya kawaida Sana niwaache waongee tu.
Usajili ulikamilika na kulikuwa na wiki Moja ya orientation, baada ya wiki hiyo kuisha rasmi tukaingia kwenye masomo, kwakuwa nilikuwa nikijua darada langu Ni lipi haikunipa shida Moja kwa Moja nikaingia kwenye darasa langu, nilikutana na watu tofauti tofauti wamependeza na wengi walionekana kuwa na maisha mazuri, niliingia nakukaa