Chizi Maarifa
JF-Expert Member
- Jul 29, 2013
- 10,471
- 23,744
Meseji uliyonitumia mpwa nmeipata.unasema unataka kuja mjini. Mwaka jana ulisema hivyo nikakueleza kuwa subiri kwanza. Naona unasisitiza nikuelekeze home uje mjini.
USIJE MJINI. hizo picha unazoniona nmepiga na kurusha kule insta asilimia kubwa siyo maisha ninayoishi. Nielewe tu. Huku kazi hamna.makampuni mengi yamefungwa na mengine kupunguza wafanya kazi.
Unafahami bei ya mchele? Huku tunanunua kilo moja tsh 2400-2600. Sukari 2700 kwa kilo. Maharagwe tsh 2600-2800 kwa kilo. Nielewe naposema Usije mjini.
Unasema mbona akina Daimondi wamewini laifu kwa kuimba nawe unataka uje kuimba.maisha hayapo hivyo mpwa wangu. Huku Mjini hakuna raha. Usibabaike na picha za watu instagram na facebook.
Unakumbuka kipindi kile mnamsema yule mtoto wa mzee kubwanga alikuwa anaokota makopo kuwa ni chizi?sasa huku mjini kuokota makopo ni moja ya kazi kwa sasa.
Usilazimishe Mpwa.unaweza ukaja ukaolewa.shauri yako. Unaweza ukaja ukawa Chokoraa. Mimi sitokukaribisha home maana najua tutagombana tu. Kama unakuja njoo kwa issues zako mwenyewe.
Ila nakwambia kama hujajipanga USIJE MJINI. watakuoa maisha yakikugonga nawe unataka maisha mazuri.maana naona hata jina umebadilisha unajiita Chidman badala ya Rashid.
Wewe nisubiri ntakuja huko huko tupange jinsi ya kufanya kilimo. Mjini hakuna issue.huwa hatuwaambii tu tukija kuwatembelea. Tunakuwa tumejipanga mwaka mzima.sasa nyie mkituona tumekuja krismasi na magari na nini na nini mnadhani ndo maisha yetu ya kila siku. Nakusisitizia mpwa USIJE MJINI
USIJE MJINI. hizo picha unazoniona nmepiga na kurusha kule insta asilimia kubwa siyo maisha ninayoishi. Nielewe tu. Huku kazi hamna.makampuni mengi yamefungwa na mengine kupunguza wafanya kazi.
Unafahami bei ya mchele? Huku tunanunua kilo moja tsh 2400-2600. Sukari 2700 kwa kilo. Maharagwe tsh 2600-2800 kwa kilo. Nielewe naposema Usije mjini.
Unasema mbona akina Daimondi wamewini laifu kwa kuimba nawe unataka uje kuimba.maisha hayapo hivyo mpwa wangu. Huku Mjini hakuna raha. Usibabaike na picha za watu instagram na facebook.
Unakumbuka kipindi kile mnamsema yule mtoto wa mzee kubwanga alikuwa anaokota makopo kuwa ni chizi?sasa huku mjini kuokota makopo ni moja ya kazi kwa sasa.
Usilazimishe Mpwa.unaweza ukaja ukaolewa.shauri yako. Unaweza ukaja ukawa Chokoraa. Mimi sitokukaribisha home maana najua tutagombana tu. Kama unakuja njoo kwa issues zako mwenyewe.
Ila nakwambia kama hujajipanga USIJE MJINI. watakuoa maisha yakikugonga nawe unataka maisha mazuri.maana naona hata jina umebadilisha unajiita Chidman badala ya Rashid.
Wewe nisubiri ntakuja huko huko tupange jinsi ya kufanya kilimo. Mjini hakuna issue.huwa hatuwaambii tu tukija kuwatembelea. Tunakuwa tumejipanga mwaka mzima.sasa nyie mkituona tumekuja krismasi na magari na nini na nini mnadhani ndo maisha yetu ya kila siku. Nakusisitizia mpwa USIJE MJINI