Mpinzani wa Obama nae aficha fedha zake Uswiss

Mpinzani wa Obama nae aficha fedha zake Uswiss

Obama naye ni mchovu vile vile si Romney peke yake. Ukiangalia uraisi wa Obama utaona kwamba ameikanya kanyaga ile katiba ya Marekani. Kafanya mengi tuu ambayo amekiuka katiba ya Marekani. Ameivamia Libya bila ya bunge kuhalalisha, ameandika executive orders(amri za raisi) kibao ambazo zinakiuka katiba. Yaani anatawala kidikteta kidkteta tuu. Huyu Romney naye ni mchovu mwingine maana anataka kuendeleza empire ya marekani (vita kila kona ya dunia) lakini hataki kuilipia yaani anakwepa kodi.

Marakani haikuvamaia Libya, ilishiriki kama sehemu ya NATO. Usihiriki wa marekani kijeshi kwenye operations za NATO ni jambo lililolahalishwa kisheria. Rais hawezi kwenda kuomba Congress kururhus jeshi la Marekani kushiriki kwenye operations za NATO; anaweza kufanya hivyo tu anapokuwa anataka kutangaza vita na taifa jingine kama ambavyo Bushi alivyfanya.
Uwezo wa rais wa marekani kutoa executive order umehalalishwa na katiba, kwa hiyo huwezi kusema kuwaalitoa excutive order inayokiuka Katiba.
 
Marakani haikuvamaia Libya, ilishiriki kama sehemu ya NATO. Usihiriki wa marekani kijeshi kwenye operations za NATO ni jambo lililolahalishwa kisheria. Rais hawezi kwenda kuomba Congress kururhus jeshi la Marekani kushiriki kwenye operations za NATO; anaweza kufanya hivyo tu anapokuwa anataka kutangaza vita na taifa jingine kama ambavyo Bushi alivyfanya.
Uwezo wa rais wa marekani kutoa executive order umehalalishwa na katiba, kwa hiyo huwezi kusema kuwaalitoa excutive order inayokiuka Katiba.

Si hivyo. Jambo lililohalalishwa kisheria ni pale mwanachama wa NATO anapovamiwa ndiyo wanaweza kujilinda. NATO wakiamua kufanya vingine lazima bunge lihalalishe. Na lazima ujue sheria za NATO haziingiliani na katiba. NATO ikisema wananchi wa nchi wanachama wanyang'anywe silaha kwa mfano, hiyo haitawezekana kwa sababu katiba ya Wamarekani inawapa wananchi haki ya kumiliki silaha. Upo hapo? Na raisi hana uwezo wa kutoa executive orders za kukiuka katiba. Mfano mwingine ni sawa na kusema Obama atoe executive order ya kunyang'anya wamarekani wote bastola. Hapo atakuwa anakiuka katiba.

Halafu hilo la Libya ni mfano mmoja tuu. Obama kafanya mengi sana ya kukiuka katiba. Unakumbuka jinsi yule myemeni Al Alawaki ambaye alipigwa drone? Alizaliwa marekani yule na katiba inampa haki kama wamarekani wengine. Ilikuwaje yeye Obama amuue bila kumpeleka mahakamani? Yaani kila mmarekani amepewa haki ya due process ndani ya katiba upo hapo? Obama yeye kaikanyaga kanyaga katiba halafu katoa executive order ya kumuua mwananchi wa marekani. Katiba ya marekani haimruhusu kufanya hivyo. Upo hapo?
 
Back
Top Bottom