Elias Msuya
Senior Member
- Dec 23, 2011
- 173
- 671
Mgombea urais kupitia chama cha ACT Wazalendo, Luhaga Mpina amepingwa kugombea urais baada ya Katibu Mwenezi wa ACT Wazalendo Mkoa wa Dar es Salaam na Naibu Waziri Kivuli wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Monalisa Joseph Ndala, kumwandikia barua Katibu Mkuu wa Chama hicho akipinga mchakato uliomteua Mgombea Urais wa chama hicho, Luhaga Mpina.
Hatua hiyo imekuja ikiwa ni siku moja tu baada ya Mpina kufika makao makuu ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) Ndejengwa jijini Dodoma kuchukua fomu ya kugombea urais baada ya kupitishwa na mkutano mkuu wa chama hicho Agosti 7, 2025.
Mpina alijiunga na chama hicho Agosti 5 na kutambulishwa rasmi Agosti 6, 2025, akitokea CCM.
Akizungumza na Jamii Forums leo Agosti 16, Monalisa amethibitisha kupeleka barua yake kwa Katibu Mkuu wa chama hicho akipinga Mpina kupitishwa kuwa mgombea.
Katika barua yake hiyo ambayo pia amewanakili Msajili wa Vyama vya Siasa na Mkurugenzi wa Tume Huru ya Uchaguzi (INEC), ameelezea namba vifungu namba 16 (4), (i),(iii) na (iv) vinavyomzuia kuwa Mgombea wa Chama hicho.
“Ni kweli nimewasilisha barua hiyo jana (Agosti 14, 2025),” amesema.
Kwa mujibu wa barua hiyo, ili mgombea Urais wa ACT WAZALENDO ateuliwe na Chama hicho, anatakiwa awe Mwanachama wa Chama hicho kwa siku 30 kabla ya kuteuliwa kwake kifungu ambacho Mpina kinamkataa.
Katibu Mkuu wa chama hicho, Ado Shaibu alipotafutwa kuulizwa suala hilo, amesema, “Kwa sasa nipo kwenye kikao, tutaongea baadaye,” amesema.
Monalisa amenukuliwa na vyombo vingine vya habari akisema yeye ni mwanachama wa chama hicho tangu kinaanzishwa na kwamba hayupo tayari kukiona chama hicho kikipoteza mwelekeo kwa kukiuka kanuni za uendeshaji wa Chama chao kama inavyoelezwa katika kanuni za uendeshaji wa Chama za mwaka 2015 na marejeo yake ya mwaka 2024.