Mpenzi wangu nimemkuta anabebwa na 'Beach Boy'

Mpenzi wangu nimemkuta anabebwa na 'Beach Boy'

Hivi mnakosaga wanawake wa kuoa? au hauna washauri wakukuongoza? mtoa mada jifikirie na jiulize je mkeo wazazi wako wamemuona na wanasemaje, umemchunguza vya kutosha? huna mke hapo achana nae
 
Shukuru kwa kuliona hilo mapema, Watu wanapoteza nguvu na rasilimali nyingi sana katika masuala ya mahusiano na kulalama baadae wakati wameshaingia katika ndoa.
Muache aende zake amekuonyesha mambo ambayo. baadae ndio angekua anayaleta ndani mwenu saa hio umeshalishwa limbwata..nk kila kitu wewe umo umo tu.
 
Shukuru kwa kuliona hilo mapema, Watu wanapoteza nguvu na rasilimali nyingi sana katika masuala ya mahusiano na kulalama baadae wakati wameshaingia katika ndoa.
Muache aende zake amekuonyesha mambo ambayo. baadae ndio angekua anayaleta ndani mwenu saa hio umeshalishwa limbwata..nk kila kitu wewe umo umo tu.
Aksante sana Kwa ushauri
 
Kipimo kikubwa cha uanamume sio tu kufanya maamuzi magumu bali ni pamoja na kusimamia maamuzi yako bila ya kujali msukumo wa moyo na ukakasi wa nafsi kwa manufaa ya maisha yako ya sasa na ya baadae......ukiishinda vita hii unatoka kuwa mwanaume na kuwa mwanaume kamili.....

Ukiivuka hatua hii utaishi maisha mazuri na yenye ustawi mzuri pasi na kuyumbishwa na mtu yoyote......
 
Beach Boys nakumbuka kule kwenye fukwe za Nungwi, ni vijana hatari sana.
Mkeo/girlfriend au mchumba akiwa na beach boy, huwa imekwisha hiyo.



Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Kipimo kikubwa cha uanamume sio tu kufanya maamuzi magumu bali ni pamoja na kusimamia maamuzi yako bila ya kujali msukumo wa moyo na ukakasi wa nafsi kwa manufaa ya maisha yako ya sasa na ya baadae......ukiishinda vita hii unatoka kuwa mwanaume na kuwa mwanaume kamili.....

Ukiivuka hatua hii utaishi maisha mazuri na yenye ustawi mzuri pasi na kuyumbishwa na mtu yoyote......
Umenena kiume, aksante sana. umenipa nguvu. manake niliona km nataka kupandwa kichwani. Nitasimamia uamzi wangu ambao ulikuwa sahihi. Japo baade alirudi home lkn akahama room lkn haoni km ana makosa.
 
badala ya kunipa majibu eti amefunga bag ameondoka home eti nimemuonea. Naombeni msaada nani ana makosa?
kuna kitu kapewa na beach boy ambacho wewe hua umpi, belive me.
 
Umenena kiume, aksante sana. umenipa nguvu. manake niliona km nataka kupandwa kichwani. Nitasimamia uamzi wangu ambao ulikuwa sahihi. Japo baade alirudi home lkn akahama room lkn haoni km ana makosa.
Nasikitika kusema kuwa kwa kufikia hapo umeshapoteza sehemu kubwa ya uanamume wako......ni dhahiri kuwa huyo binti anakuona mwanaume lakini haoni uanamume ndani yako......na uanaume unaonekana kwa matendo ya kiume.......na matendo ya kiume huonenakana pale unaporuhusu akili yako ifanye kazi badala ya moyo.......kwani moyo hupofusha akili ........

Think big take control of your destiny.....
 
Sasa na wewe umempa ruhusa ya kwenda beach sawa ilikuwaje na wewe ukaenda beach hiyo hiyo tena? Na pia kama unamuona yuko na beach boy kwanini na wewe usiende kumchukua msichana wako ukawa beach boy wake kwa mda huo acha ujinga siku nyingine usifanye makosa dawa ya moto ni moto
 
Back
Top Bottom