Mpenzi wako akifa ndani kwako utafanyaje?

Mpenzi wako akifa ndani kwako utafanyaje?

kingkongtz

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2019
Posts
1,059
Reaction score
3,646
Wakuu kwema?

Huwa najiuliza sana mfano imetokea umekuwa na mahusiano na mwanamke halafu baada ya wiki akaja kwako kulala halafu asubuhi unamuamsha unataka uingie mishe mishe unashangaa haamki, unamtikisa unaona hatikisiki, unammwagia maji haamki. Unahamaki kuona anatokwa povu mdomoni, unamgusa unakuta wabaridi

Unagusa kifuani unashtuka mapigo ya moyo hayadundi. Je, utatoka nje uwajuze majirani? Wataamini vipi kama ni bahati mbaya

Je, utatoroka?? Hapa utakuwa umejivua utu na itaonekana kama ulikusudia

Ukibaki tena ni msala tena msala kwelikweli

Je, utafanyaje??
 
Hapo chakufanya we hama mtaa asubuh acha kila kitu ndani ondoka na vya thaman kiasi sepa kusikojulikana,ila mtaani hakikisha huna identity au any ligacy!

Zama zako nanjirinji huko katafte maisha ya shamba kwa miaka 10 then rudi town!

Kipindi icho muombee kwa mungu marehemu aliyekufa bila kukusudia chumbani kwako na uombe toba kwa kutenda dhambi ya uongo kwa kuikimbia maiti yako!
 
Nenda kwa mjumbe mpe taarifa.

Wewe na mjumbe mtaenda polisi kutoa taarifa.

Maiti itapelekwa hospitali. Wewe utakuwa mshukiwa namba moja hivyo utawekwa rumande na kuchukuliwa maelezo.

Mwili utafanyiwa autopsy ili kujua chanzo cha kifo. Lengo ni kujua kama ni natural death au kuna foul play.

Kama ni natural death hiyo kesi inakua haina locus standi kufunguliwa mahakamani so utaachiwa. Ikionekana kuna foul play mfano sumu hapa sasa show itakua ndefu.

NB. Usione naandika hivi ukadhani na askari wataenda step by step kama mimi unaweza shangaa upo gerezani kutumikia adhabu na mahakamani hukuwahi kwenda.

So you can just throw the whole ghetto away and elope to the nearest forest while figuring your next move.
 
Nilikuwa Tanga demu akaanza kuumwa tumbo usiku hadi analia hapo mie wala sijamgusa. Kusema kweli niliogopa sana na nilikuwa najiuliza huyu akifa hapa ndiyo nafanyaje?
Yule mrembo tulipendana sana na nilijua atakuwa mke wangu. Penzi letu lilisababisha ugomvi mkubwa kati ya dada yake na shemeji yake. Dada mtu ambaye alikuwa akiniona mimi kijana wa maana sana hadi kunisifia kwa wadogo zake wa kike baada ya kujua tu mdogo wake ni mpenzi wangu akanichukia vibaya sana hadi akaanza vitisho kwangu kwamba ataniroga 😂😂😂😂wakati mie nimeweka pamba masikioni. Shemeji alikuwa ananifagilia kwamba atuache na penzi letu hatimaye nao wakaanza kugombana kisa penzi letu. Dada mtu ndiyo akaamua kumhamishia binti Tanga kama vile Tanga na Dar umbali wake ni mbingu na ardhi 😂😂


wakuu kwema


huwa najiuliza sana mfano imetokea umekuw na mahusiano na demu alafu baada ya week akaja getho kulala

asubuh unamuamsha unataka uingie mishe mishe unashangaa haamki,unamtikisa unaona hatikisiki ,unammwagia maji haamki.unahamaki kuona anatokwa povu mdomoni,unamgusa unakuta wa baridii

unagusa kifuan unashtuka mapigo ya moyo hayadundi.


je utatoka nje uwajuze majiran?? wataamin vipi kama n bahat mbaya

je utatoroka?? hapa utakuw umejivua utu na itaonekana kama ulikusudia

ukibak tena ni msala tena msala kwel kwel

wakulungwa leo tupige story hii inshu ikitokea we utafanyaje japo hatuombei itokee.
 
Mheshiwa jiwe mwenyewe alikufa akiwa na wasaidizi pembeni
Ni issue ya protocol tuu wala usiogope kijana
 
Back
Top Bottom