ndyoko
JF-Expert Member
- Nov 2, 2010
- 4,971
- 1,649
"Nilipanga hiyo hela nimsaidie ili aongezee mtaji afungue saluni ya kike. Kabla ya kumpatia hiyo pesa ikaja taarifa ya kuuguliwa na binamu yangu. Kutokana na umuhimu wake kwangu, nikaamua pesa, nilopanga kumpa yeye ili aanzishe mradi wake wa saluni, niipeleke kwenye matibabu ya binamu yangu aliye mgonjwa sana.
Akadai eti simpendi vinginevyo ningempa yeye kwanza halafu nifanye mpango wa kutafuta nyingine ili nimtibie huyo ndugu yangu kwani yeye alikuwa wa kwanza. Hadi leo ni wiki imepita amenuna na akipigiwa simu hapokei, na wala hajakuja kumuona wifi yake mtarajiwa. Mwanzoni niliona kama ni mwanamke anayeweza kuwa mke wa maana lakini ktk hili nimeanza kuwa na wasiwasi juu ya upendo wake kwa ndugu zangu. Iweje ameshindwa kuona umuhimu wa kutibu ugonjwa ili kuepusha kifo? Je mchumba dizaini hii kweli kuishi na ndugu wa mume kweli achilia mbali kuwasaidia wakati wa shida?".
Kadhia hii imemkuta mtu wangu wa karibu na ameomba nimshauri la kufanya juu ya huyu 'kishtobe' wake alokuwa akimpa nafasi ya kuwa mkewe siku za usoni.
Jamaa ameboreka hasa kutokana na tabia iliyoonyeshwa na huyu 'kishtobe' wake. Bado anajishauri aendelee na mpango wa kumuoa au amteme jumla jumla kwa sababu ya dalili hii mbaya aloionyesha mapema?
Akadai eti simpendi vinginevyo ningempa yeye kwanza halafu nifanye mpango wa kutafuta nyingine ili nimtibie huyo ndugu yangu kwani yeye alikuwa wa kwanza. Hadi leo ni wiki imepita amenuna na akipigiwa simu hapokei, na wala hajakuja kumuona wifi yake mtarajiwa. Mwanzoni niliona kama ni mwanamke anayeweza kuwa mke wa maana lakini ktk hili nimeanza kuwa na wasiwasi juu ya upendo wake kwa ndugu zangu. Iweje ameshindwa kuona umuhimu wa kutibu ugonjwa ili kuepusha kifo? Je mchumba dizaini hii kweli kuishi na ndugu wa mume kweli achilia mbali kuwasaidia wakati wa shida?".
Kadhia hii imemkuta mtu wangu wa karibu na ameomba nimshauri la kufanya juu ya huyu 'kishtobe' wake alokuwa akimpa nafasi ya kuwa mkewe siku za usoni.
Jamaa ameboreka hasa kutokana na tabia iliyoonyeshwa na huyu 'kishtobe' wake. Bado anajishauri aendelee na mpango wa kumuoa au amteme jumla jumla kwa sababu ya dalili hii mbaya aloionyesha mapema?