Mpasuko Tume ya Taifa ya Uchaguzi vs Wakurugenzi

Mpasuko Tume ya Taifa ya Uchaguzi vs Wakurugenzi

Sexer

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2014
Posts
8,513
Reaction score
8,276
Wanajamvi hivi sasa hali katika tume ya taifa ya uchaguzi si shwari kwa upende mmoja na nishwari kwa upande mwingine, ifahamike katika uchaguzi tume ya taifa hujumuisha pia maafisa wa serikali kama vile wakurugenzi wa halmashauri, nk.

Sasa kilichotokea katika tume hiyo limeibuka kundi ndani ya tume hiyo wakiwemo maafisa wa juu wa tume na wengi wa wakurugenzi ambao wasimamizi wa chaguzi ngazi ya wilaya wakidai na kusisitiza safari hii hakuna kupokea maelekezo yoyote kutoka kwa mwanasiasa.

Kundi hilo linataka kwamba kura zikishahesabiwa na matokeo kujulikana, basi mshindi atangazwe mara moja. Ila kuna baadhi ya maofisa ndani ya tume wanapinga sana wazo hilo jema.

Tusubiri tuone.
 
Tunachoomba Matokeo Yatangazwe instantly Kura Zikimaliza Kuhesabiwa na Kujumlishwa na Hii Itaepusha FUJO .
 
kama wanataka amani iwepo wasifanye mchezo kama matokeo yakitoka wafanye hima watangaze
 
huu mwaka unahitaji busara sana kwa mwenye akili yeyote ni muhimu sana kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ya kazi yake otherwise watakuwa wanajitafutia kuwa miongoni mwa watu ambao hawatasahaulika kama nchi hii itaingia kwenye shida yeyote iliyosababishwa na mambo ya uchaguzi. watendaji wa mwaka huu wanapaswa kufanya kazi huku wakitambua wao watakuwa miongoni mwa watu watakao ingia katika historia ya Taifa hili ni jukumu lao kuamua historia iwakumbuke na kuwahukumu kwa namna gani wema au ubaya ni wao ndo waamue.

Mkuu naona wengi wa wanatume wameshaliona hilo na ndo maana wanasisitiza hakuna kupokea maelekezo ya wanasiasa
 
Kwenye kuhesabu kura tu ndio penye utata ni bora kura zote 3 zitangazwe kwenye kituo husika
 
Hao wanaotaka matokeo yasitangazwe palepale ni nini, au ndo goli la mkono lenyewe?
 
...mvutano wao usutuharibie nchi, ujinga mdogo tu patachimbika. Haki wanaijua wajibu wao wanaujua waige mfano wa Nigeria...
 
Hao wanaotaka matokeo yasitangazwe palepale ni nini, au ndo goli la mkono lenyewe?

Walizoe matokeo yakishatoka wanawapa kwanza mambwana zao kule serikalini ndo waruhusu kama yatangazwe vile yalivyo au ifanyike namna nyingine
 
chereko chereko chereko

DIRECT VOTES RESULT ZITOLEWE HARAKA SANA KUEPUSHA GHASIA NCHINI MWETU!!!

mfupa huu ukawa ya zamani ingeliuweza???
 
washikilie hilo vurugu zitawatoa ngeu-kura zihesabiwe na kubandikwa vituoni . anayehusika kutangaza atangaze majumuisho siku hiyohiyo mambo ya Dodoma ya kufungia store mkome
 
Back
Top Bottom