Mpasuko mkubwa mwingine waja UKAWA/ CHADEMA

Mpasuko mkubwa mwingine waja UKAWA/ CHADEMA

Tatizo mnajifanya nyie ni kina "kj".....

mnyika akitoka hamjui majimbo mawili mshayakosa?

ama hamjui la ubungo mshalikosa tayari?

Naona umerithi cheo cha Shekh Yahaya.CDM sio MTU Bali ni taasisi imara ya watz wote
 
Hizo ni siasa za abunuasi chuki juu ya EL, basi kama mnadai yy ni fisadi basis no zao la chama cha mafisadi, maaana anawiki mbili tuu ukawa/ Cdm na ndo maana Dr Slaa aliifananisha sisihumu na choo
 
Tatizo la Maccm ni kuwa, baada ya kufilisika kisiasa, baada ya kuona kweli sasa hayapendwi yameingia kuchafua amani kwa kupandikiza chuki wazi wazi kati ya wananchi.
Hizo ndizo siasa mufilisi. Mkiisha pandikiza migogoro katika vyama vingine, hao wanachama wenu wanawatosha?? Si hao hao mnaowafitinisha ndo watakuja kuwa wanachama wenu?? Yaani kweli "Wapumbavu" ndio sasa wanajidhihirisha. Waswahili wanasemaga; Ukipanda bangi, huwezi kuvuna mchicha. Mnapanda uchokozi mmtauvuna uchokozi tuuu.
Kama kwa miaka 54+ mlijichimbia katika kuwaibia wananchi, mnategemea kujisafisha kwa hizi siku 48 zilizobakia?? Bado mpaka sasa mnaendelea kutoa ahadi?? Chama tawala miaka yoote hiyo bado hamna uwezo wa kusema tulifanya nini?? Bado mnaomba mtupe tena ahadi hewa za miaka 5 mingine ati mmepata tingatinga??? Kweli, ukistaajabu ya Musa, njoo uone ya Magufuli. Hilo tingatinga mmelileta kutoka sayari gani??? Mh. JK, leta tena kamusi mpya ya ahadi hewa. Hii, mhhhh. Imebuma. CCM ishakufia mikononi. Hapa, hutokiiiii

jana mgombea wao bwana pombe, kawatisha watu wa morogoro. Heti wasichague UKAWA nchi isije kuwa kama libya.

Huku ni kufilisika kisiasa kabisa utaifananishaje nchi ya kidemokrasia na nchi ya kidikteta?

Au ndio ile kauli ya sumaye kwamba ccm ni chama kilicho vaa koti la vyama 2?
 
Hivi umekaa kabisa ukatafakari na kumuona EL ikulu? Labda huko Monduli, mkamjengee state house, lakini pia mnaitwa kuchangia kampeni za UKAWA.. pesa imekata!!

Mwaka huu ccm chaliii, Lowasa atosha
 
Jambo moja tu lakupasa kutambua kua chama chochote cha siasa sio mtu bali ni taasisi. Kwamaana hiyo niwatu wengi sana zaidi yaunavyo fikilia. Kwakifip tu usitegemee kuondoka kwamtu ktk taasis basi taasis hiyo inaanguka. Pole kwakutokuchambua mambo.
 
Baada ya Dr. Slaa kuleta sintofahamu kubwa kwenye UkIwa/Chadema na fisadi wao papa Lowassa, sasa katika kipindi cha wiki mbili kutatokea 'exodus' kubwa kama ile aliyoimba hayati Bob Marley. Wanaotajwa kusumbuliwa sana na nafsi zao kama Dr. Slaa ni John Mnyika pamoja na Mabere Marando. UKAWA walisubirie hili pigo kubwa ambalo liko njiani.


Kama ccm wamebaki na idadi kubwa ya mafisadi lakini inachukuliwa kuwa ni chama bora kuliko CHADEMA iliyompokea Lowassa basi nadhani watanzania watakuwa hawajafikia hatua/kiwango cha kuwa binadamu kamili...
Labda bado 3/4 yao ni Sokwe...
 
Wewe ni mgeni wa mambo ya siasa, siku nyingine kama hona hoja ya msingi bora kaa kimya na kusoma za wenzio.

Baada ya Dr. Slaa kuleta sintofahamu kubwa kwenye UkIwa/Chadema na fisadi wao papa Lowassa, sasa katika kipindi cha wiki mbili kutatokea 'exodus' kubwa kama ile aliyoimba hayati Bob Marley. Wanaotajwa kusumbuliwa sana na nafsi zao kama Dr. Slaa ni John Mnyika pamoja na Mabere Marando. UKAWA walisubirie hili pigo kubwa ambalo liko njiani.
 
Marando ni insider
mwana kitengo....Mnyika siku zote ana misimamo yake
 
hamna mpasuko wowote slaa ashasahaulika na hajaleta impact yoyote watu washafanya maamuzi
 
Hivi umekaa kabisa ukatafakari na kumuona EL ikulu? Labda huko Monduli, mkamjengee state house, lakini pia mnaitwa kuchangia kampeni za UKAWA.. pesa imekata!!

Mimi sina chama...hata hao ukawa wakikosea nitaongea pia! Hivyo don't attack me personally!

Ila nakerwa na wana-ccm wa mitandaoni ambao kutwa kucha badala ya kusaidia kampeni kueneza sera za chama chao wanakaa kusema ya Lowassa na ukawa...nahisi ni kama mnawapiga kick!
 
Juzi na Jana nilikuwa katika moja ya kijiji ktk wilaya ya KARATU kuangalia IMPACT ya Dr kujitoa CDM. Kila kona ya Karatu ni Lowasa tu.

Ukweli ni kuwa hawana mpango na DR. tena, wako na MABADILIKO na zaidi sana Mgombea UBUNGE kwa tiketi ya CDM anasubiri kuapishwa.
 
Tulisha hamua....tunasonga mbele. Nyie wanunueni ndo mtajua wapiga kura ni sisi na wala sii mnyika wala dr blaa blaa na huyo marando unaemtaja. Hata mboe akichapa lapa maamuzi yapo kwetu watz . Bora nec ishampitisha lowasa basi. Tutasonga mbele.

Watu wakibadili upepo mnasema wamenunuliwa?

Ngoja tuendelee kuwanunua?
 
Five Billions loss on CCM books no impact. Are guys still thinking of incurring more losses.
Try other effective political strategies but buying the likes of Dr Slaa and Prof Lipumba is not working. Just a free piece of advise.
 
Kumbe humjui slaa, slaa anapenda kuwa mpinzani!! Kaona chadema inakaribia kuc hukua dola that's why kakimbilia ccm kwakuwa anajua ndo itakuwa kambi rasmi ya upinzani bungeni!!!!
 
Mugisher unatafuta kufungwa unamwita mtu fisadi una ushahidi au unaendekeza kuchafua jina la mtu tu.Hujui kua unavunja sheria?
 
Baada ya Dr. Slaa kuleta sintofahamu kubwa kwenye UkIwa/Chadema na fisadi wao papa Lowassa, sasa katika kipindi cha wiki mbili kutatokea 'exodus' kubwa kama ile aliyoimba hayati Bob Marley. Wanaotajwa kusumbuliwa sana na nafsi zao kama Dr. Slaa ni John Mnyika pamoja na Mabere Marando. UKAWA walisubirie hili pigo kubwa ambalo liko njiani.

Maneno ya mfa maji, hadanganyiki mtu. EL rais nyie bakini na bla bla zenu. hata nini kitokee hakuna kubadilika kamwe na nawaambia baada ya EL atakaefuata urais ni kamanda Mbowe, hapo ndipo WATZ watashuhudia sayansi ya uongozi wenye matokeo ya kweli na ndipo ukomo wa umasikini wetu utakapofikia.
 
Back
Top Bottom