kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 16,247
- 16,169
Adui namba moja wa uchumi wa Marekana ni Ulaya iliyoungana na sarafu ya euro. Marekani inakasirishwa na upanuzi wa umoja wa ulaya kuelekea Mashariki. Upanuzi huu wa ulaya unaibana Marekani kwa upande mmoja na China kwa upande mwingine na baadae BRICS kwa upande uleee.
Uingereza kujitoa kwenye umoja wa ulaya ilikuwa moja ya mikakati hiyo. Vita ya Ukraine ni mpango mwingine wa kuisambaratisha EU kiuchumi hasa baada ya kaka mkuu wao Ujerumani kuanguka kiuchumi baada ya kukata upatikanaji wa gesi rahisi kutoka Urusi.
Baada ya ulaya kususia gesi na mafuta ya Urusi, hii imeinufaisha India na China ambazo sasa zinafaidika na rasilimali za Urusi hivyo kuchechemua uchumi wao kwa gharama nafuu. Hii inaitisha Marekani vibaya sana kiasi kwamba inaona ni ujinga mkubwa kuzikosa rasilimali rahisi za Urusi kwasababu ya kijinga ya vita ya Ukraine ambayo imeshindikana kuishinda Urusi inayotegemea ushirika wake na China na India. Kumbuka lengo kuu la vita ya Ukraine ilikuwa kuzipora rasulimali za Urusi na Ukraine lakini lengo hilo linaonekana kama vile liko mbali sana na uhalisia.
Marekani wamebadili gia angani na kuachana na vita ya Ukraine na kuamua kuisogelea Urusi kibiashara badala ya kivita. Ukweli hata huu mkutano wa Trump na Putin huko Alaska haukuwa kwaajili ya Ukraine, bali kwaajili ya kuombana radhi na kuendelea na uhusiano wa kibiashara kati ya Urusi na Marekani. Kama ukimsikia Rais Putin na Makamu wake JD Vance utagundua sasa hivi wanauacha mzigo wa Ukraine kwa umoja wa ulaya pekee ili wazidi kufilisika na hatimaye kuwa dhaifu kiuchumi kiasi cha kuhitaji kuitegemea tena marekani. Ndiyo maana unaona hata baada ya mazungumzo na Trump lakini Putin anaendelea kuitwanga Ukraine bila Trump kusema lolote.
Marekani wamegundua kuwa hawawezi kuishinda Urusi inayoungwa mkono na China, ndiyo maana sasa hivi inataka kurudisha Marekani viwanda vyake vyote kutoka Asia. Iko karibu hata Taiwan itakuwa haina umuhimu tena kwa Marekani.
Vita ya Ukraine imekwisha.
Uingereza kujitoa kwenye umoja wa ulaya ilikuwa moja ya mikakati hiyo. Vita ya Ukraine ni mpango mwingine wa kuisambaratisha EU kiuchumi hasa baada ya kaka mkuu wao Ujerumani kuanguka kiuchumi baada ya kukata upatikanaji wa gesi rahisi kutoka Urusi.
Baada ya ulaya kususia gesi na mafuta ya Urusi, hii imeinufaisha India na China ambazo sasa zinafaidika na rasilimali za Urusi hivyo kuchechemua uchumi wao kwa gharama nafuu. Hii inaitisha Marekani vibaya sana kiasi kwamba inaona ni ujinga mkubwa kuzikosa rasilimali rahisi za Urusi kwasababu ya kijinga ya vita ya Ukraine ambayo imeshindikana kuishinda Urusi inayotegemea ushirika wake na China na India. Kumbuka lengo kuu la vita ya Ukraine ilikuwa kuzipora rasulimali za Urusi na Ukraine lakini lengo hilo linaonekana kama vile liko mbali sana na uhalisia.
Marekani wamebadili gia angani na kuachana na vita ya Ukraine na kuamua kuisogelea Urusi kibiashara badala ya kivita. Ukweli hata huu mkutano wa Trump na Putin huko Alaska haukuwa kwaajili ya Ukraine, bali kwaajili ya kuombana radhi na kuendelea na uhusiano wa kibiashara kati ya Urusi na Marekani. Kama ukimsikia Rais Putin na Makamu wake JD Vance utagundua sasa hivi wanauacha mzigo wa Ukraine kwa umoja wa ulaya pekee ili wazidi kufilisika na hatimaye kuwa dhaifu kiuchumi kiasi cha kuhitaji kuitegemea tena marekani. Ndiyo maana unaona hata baada ya mazungumzo na Trump lakini Putin anaendelea kuitwanga Ukraine bila Trump kusema lolote.
Marekani wamegundua kuwa hawawezi kuishinda Urusi inayoungwa mkono na China, ndiyo maana sasa hivi inataka kurudisha Marekani viwanda vyake vyote kutoka Asia. Iko karibu hata Taiwan itakuwa haina umuhimu tena kwa Marekani.
Vita ya Ukraine imekwisha.