Zanzibar walifanya mapinduzi matukufu mwaka 1964 walikuwa wanampindua nani? Tanganyika ilipata uhuru wake mwaka 1961 ikiwa ni pamoja na hilo eneo la 10 km za Pwani ya bahari ya hindi. Uhuru ulitolewa na Mwingereza pale shamba la bibi kila mtu anajua. Ikulu ya Mwingereza iko pale Magogoni nasi kama Watanganyika hatujawahi kujenga Ikulu, kila mtu anafahamu. Kenya ilipojinyakulia uhuru wake mwaka 1963 ni pamoja na eneo la 10 km za Pwani ya bahari ya Hindi na ili kuondoa shaka ni pamoja na mji wote wa Mombasa hadi huko Lamu, kila mtu alijua hilo; Leo Zanzibar kuanza kudai 10 km, hoja hii inatoka wapi? Je Mapinduzi yao ya 1964 yalijumuisha ukombozi wa miji ya Mtwara, Dar es Salaam, Tanga, Mombasa na Lamu?Hakika mfa maji haachi kutapa, kama Wazanzibar mnapenda eneo hilo endeleeni kukaa ndani ya muungano na Jumuia ya Afrika Mashariki ili mfaidi matunda ya pwani. Wakati huu wa Global warming visiwa vingi vinazama kutokana na kuongezeka kwa maji katika bahari kunakosababishwa na uyeyukaji wa barafu katika milima mirefu duniani. Visiwa hivi vikizama mtaelekea wapi ninyi wavivu wa kufikiria?Hivi sasa population ya Zanzibar ni around 1,500,000 na eneo la visiwa vyenu ni km za mraba 2,650 sawa na mita za eneo 2,650,000,000 ukigawanya kijihesabu hiki kirahisi utapata jawabu kuwa mtu mmoja hawezi kumiliki zaidi ya mita za eneo 1,767 sawa na eneo lenye upana wa mita 42 kwa 42 ambacho ni kiwanja cha medium density au Low density, kwa sasa hali ndiyo hii, je itakuwaje miaka 50 ijayo?; mwenye macho ya kuonea na aone na mwenye masikio ya kusikilia na asikie.Mkitaka kuvunja muungano ruksa! Ingawa sidhani kama hili litafanikiwa katika kipindi hiki mzee Mwinyi akiwa hai maana muungano ukivunjika pensheni yake itakoma mara moja; Tanganyika hawatambua kama rais mstaafu wala Zanzibar hawatambua pia labda kwa mbali kama rais mstaafu wa Zanzibar.Muungano ni hiari, mkitaka kuondoka, nendeni kwa amani.