Keynez
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 3,621
- 6,510
Marekani amekuwa anaiwaza na kujipanga na vita dhidi ya Iran kwa miaka zaidi ya 40 sasa.
Siku zimekwenda, nyakati zimefika, na vita nayo imefika. Pande zote mbili zipo kwenye "theater of war" wanatwangana.
Marekani ana play "a long game" kwa kumfanya Iran awe "desperate" na aonyeshe kadi zake zote. Wakati huo huo, Iran anaonyesha mbinu zake na kile alichokuwa amejiandaa nacho mfano matumizi ya drones ambazo kwa bahati mbaya kwa Iran, Marekani alishaona akizitumia kwa hiyo hazijamshangaza sana madhara yake.
Wengi wanaodai Iran ameshinda au anashinda hii vita wanasahau kitu kimoja. Marekani mpaka sasa hajaonyesha silaha yoyote mpya katika vita hii ambayo unaweza kuita ni "game changer". Ina maana kwamba kwa tathmini ya Marekani, bado vita inaenda kwa jinsi wanavyotaka kwa hiyo hawajaona umuhimu wa kuonyesha turufu yao mpya. Unadhani Marekani ajiandae kwa vita na wewe kwa miaka 40 halafu ategemee tu silaha zilezile za siku zote ndiyo zimuokoe? Yale marobot mpaka sasa hayajaingizwa vitani na hatujui kipi kingine walichonacho.
Iran anaenda kuishiwa stock ya makombora, huku uwezo wa kuzalisha makombora mapya katika mazingira ya sasa ni mgumu sana. Pia uchumi wake unaenda kuanguka maana hana uwezo tena wa kuuza mafuta wala kufanya biashara nyingine ya maana na dunia.
Siku zote wazee wa vita wanajipanga kwanza kwenye uchumi wao (na jinsi watakavyoumiza uchumi wako) kabla hata risasi moja haijarushwa.
Kwa kumalizia, msilinganishe vita hii na tuvita twingine kama tule twa Israel na Waarabu, vita inapiganwa siku 6 imeisha, kila mtu anarudi kwake na labda Israel ameteka vipande vya ardhi. Hii vita ni ya kuondoa utawala ulio madarakani kwa zaidi ya miaka 40 uliojijengea ushawishi Palestina, Lebanon hadi Yemen. Ni vita inayoenda kubadili siasa nzima za Mashariki ya Kati.
Siku zimekwenda, nyakati zimefika, na vita nayo imefika. Pande zote mbili zipo kwenye "theater of war" wanatwangana.
Marekani ana play "a long game" kwa kumfanya Iran awe "desperate" na aonyeshe kadi zake zote. Wakati huo huo, Iran anaonyesha mbinu zake na kile alichokuwa amejiandaa nacho mfano matumizi ya drones ambazo kwa bahati mbaya kwa Iran, Marekani alishaona akizitumia kwa hiyo hazijamshangaza sana madhara yake.
Wengi wanaodai Iran ameshinda au anashinda hii vita wanasahau kitu kimoja. Marekani mpaka sasa hajaonyesha silaha yoyote mpya katika vita hii ambayo unaweza kuita ni "game changer". Ina maana kwamba kwa tathmini ya Marekani, bado vita inaenda kwa jinsi wanavyotaka kwa hiyo hawajaona umuhimu wa kuonyesha turufu yao mpya. Unadhani Marekani ajiandae kwa vita na wewe kwa miaka 40 halafu ategemee tu silaha zilezile za siku zote ndiyo zimuokoe? Yale marobot mpaka sasa hayajaingizwa vitani na hatujui kipi kingine walichonacho.
Iran anaenda kuishiwa stock ya makombora, huku uwezo wa kuzalisha makombora mapya katika mazingira ya sasa ni mgumu sana. Pia uchumi wake unaenda kuanguka maana hana uwezo tena wa kuuza mafuta wala kufanya biashara nyingine ya maana na dunia.
Siku zote wazee wa vita wanajipanga kwanza kwenye uchumi wao (na jinsi watakavyoumiza uchumi wako) kabla hata risasi moja haijarushwa.
Kwa kumalizia, msilinganishe vita hii na tuvita twingine kama tule twa Israel na Waarabu, vita inapiganwa siku 6 imeisha, kila mtu anarudi kwake na labda Israel ameteka vipande vya ardhi. Hii vita ni ya kuondoa utawala ulio madarakani kwa zaidi ya miaka 40 uliojijengea ushawishi Palestina, Lebanon hadi Yemen. Ni vita inayoenda kubadili siasa nzima za Mashariki ya Kati.