uzinduzi wa kampeni za serikali za mitaa mkoa wa mara uliofanyika musoma mjini siku ya alhamisi ukiongozwa na mwenyekiti wa chadema mkoa wa mara(mbunge wa jimbo la musoma mjini) kamanda Vincent Nyerere akishirikiana na mbunge wa nyamagana kamanda Wenje,uzinduzi ulikuwa ni wa kipekee na wenye mapokezi makubwa kwani mpaka sasa pamoja na kwamba ccm wanatumia pesa na vitisho kwa wagombea wa upinzani lakini bado hali yao ni mbaya sana katika mkoa wa mara.Mpaka sasa ukawa ikiongozwa na kamanda Vincent Nyerere wamefanya mikutano isiyopungua mitatu kwa kila siku katika vijiji na wilaya mbalimbali za mkoa wa mara,wananchi wamesema kamwe hawatoweza kuvumilia na kukumbatia uzembe unaofanywa na serikali ya ccm na kwa pamoja watahakikisha ccm haipati kiongozi hata mtaa mmoja.Vijiji ambavyo vimeshapewa elimu ya uraia na kupiga kura ni kata ya Etaro kijiji cha rukuba,kamnyonge,kijiji cha busamba etaro,kata ya mkendo,mara sekondari,bukanga.kesho ni zamu ya wakazi wa kamnyonge kupewa elimu itafuata kibuyi,shirati,tarime,Serengeti,butiama,bunda.