Mpaka Rais atoke Dar kuzuia Chakula cha Msaada Misenyi

Mpaka Rais atoke Dar kuzuia Chakula cha Msaada Misenyi

Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli amezuia serikali kupeleka chakula cha msaada wilayani Misenyi mkoani Kagera kwa madai kuwa wilaya hiyo haina sababu ya kukumbwa na tatizo la njaa.

Rais Magufuli amekataa serikali kupeleka chakula cha msaada katika wilaya hiyo na kusema haikubaliki kwa eneo hilo lenye mvua za kutosha na hali nzuri ya kilimo na kwamba haiwezekani kulia njaa wakati kuna uwezekano wa kuzalisha kwa ajili ya chakula.

Wakati akisema haya kuna viongozi wengi tu wapo wilayani na Mkoani Kagera.
Kama ni hivyo basi tunaomba atumbue DC Kwa kukiuka agizo lake.

Kaka watu wanaogopa kufanya maamuzi ya aina yoyote
1: Mmoja kasema kuna Zika kafutwa kazi
2:Mmoja kaogopa kuripoti mambo ya Kipindupindu Kafutwa kazi
3: Mramba Kasign Barua ya kuomba ongezeko la bei ya umeme, na EWURA wakaizinisha hiyo bei, Aliyeomba Kafukuzwa na walikubali na kupitisha hiyo bei wanapeta
 
Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli amezuia serikali kupeleka chakula cha msaada wilayani Misenyi mkoani Kagera kwa madai kuwa wilaya hiyo haina sababu ya kukumbwa na tatizo la njaa.

Rais Magufuli amekataa serikali kupeleka chakula cha msaada katika wilaya hiyo na kusema haikubaliki kwa eneo hilo lenye mvua za kutosha na hali nzuri ya kilimo na kwamba haiwezekani kulia njaa wakati kuna uwezekano wa kuzalisha kwa ajili ya chakula.

Wakati akisema haya kuna viongozi wengi tu wapo wilayani na Mkoani Kagera.
Kama ni hivyo basi tunaomba atumbue DC Kwa kukiuka agizo lake.

Kaka watu wanaogopa kufanya maamuzi ya aina yoyote
1: Mmoja kasema kuna Zika kafutwa kazi
2:Mmoja kaogopa kuripoti mambo ya Kipindupindu Kafutwa kazi
3: Mramba Kasign Barua ya kuomba ongezeko la bei ya umeme, na EWURA wakaizinisha hiyo bei, Aliyeomba Kafukuzwa na walikubali na kupitisha hiyo bei wanapeta
 
Hivi na watoto nao wanatakiwa kulima chakula? Hivi na wazee na wagojwa nao wanatakiwa kulima chakula chao. Kuruhusu watu wafe kwa njaa kwa sababu ya msimamo wa kuwanyosha watanzania ni uharifu dhidi ya ubinadamu. Labda kama hakuna njaa na watu wanatafuta kupiga kwa kusingizia njaa,
Umesema kweli kabisa. Kuna wazee, watoto, walemavu ambao ukame huo wa migomba kunyauka umewaathiri na wao jee kuwanyima chakula ndio suluhisho?
Huu ni uhalifu dhidi ya binadamu na hauna tofauti na ule wa yule wa Sudan aliokuwa anafanya kule Darful na akaishia kushtakiwa The Hague. Tusisubiri watu wafe kama nzige waliomwagiwa dawa huko Misenyi ndi tuseme bali watu na waseme sasa na kuacha unafiki. Njaa hiyo hata hao CCM wanao muunga mkono kwa kila kitu watakufa.
Hakuna sababu ya sisi Watanzania wengine kula ugali na kusaza wakati wengine Misenyi wanapata dhiki baada ya migomba kunyauka kwa vile mtu mmoja tuu (hata awe nani) ameamua hivyo.
 
Uchaguzi ukifika atautafuta ulimi mzuri tu
Kigamboni aliwaambia wapige mbizi, wakati wauchaguzi alisema alikuwa anawatania watani wake. Wasukuma wana utani na makabila yote ya Tanzania?

Kwa mwaka 2020 hataitaji kujieleza. Amri itatumika zaidi.
 
Watoto wanakula kwa Wazazi wao, Wazee wana watoto wanatamba tu mjini hapa na kelelele kumbe wazee wao njaa kali. Wahaya ni watu hovyo sana
. Kwanini mtu uwe mjinga kiasi hiki...akili za mendé hazimtosh binadamu jameni!!huwez tukana mababu mpaka vichanga kijinga namna hii.
 
Naona Magufuli anawalizimisha watu kutumia akili zao kupata chakula, malazi, na mafanikio.

Tungeomba na Serikali iwe mfano kwa kukutana misaada yote inayotoka nje. Itumie akili kupata maendeleo, uchumi bora etc .
Point
 
Jicho hilohilo analotumia magufuli kuwatazamia wana Misenyi ndilo hilo hilo wanalotumia wafadhili wa nje kututizamia! Magufuli anahoji kwa nini kuwe na njaa wakati kuna hali nzuri ya hewa!! Ni sawa na mimi ninavyojiuliza kwa nini serikali iliamua kutumia misaada tuliyoitoa kwa wahanga wa tetemeko wakati serikali ina vyanzo vingi vya mapato? Ni kama tu mataifa mengine yanavyotushangaa kwa nini hii nchi ni fukara wakati ina rasilimali rundo? Kwenye nyumba yenye msiba ni kawaida kutoa rambirambi! Hiyo ndiyo kawaida,hata kama familia ya marehemu ni tajiri.
 
Back
Top Bottom