Kituko
JF-Expert Member
- Jan 12, 2009
- 9,555
- 9,368
Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli amezuia serikali kupeleka chakula cha msaada wilayani Misenyi mkoani Kagera kwa madai kuwa wilaya hiyo haina sababu ya kukumbwa na tatizo la njaa.
Rais Magufuli amekataa serikali kupeleka chakula cha msaada katika wilaya hiyo na kusema haikubaliki kwa eneo hilo lenye mvua za kutosha na hali nzuri ya kilimo na kwamba haiwezekani kulia njaa wakati kuna uwezekano wa kuzalisha kwa ajili ya chakula.
Wakati akisema haya kuna viongozi wengi tu wapo wilayani na Mkoani Kagera.
Kama ni hivyo basi tunaomba atumbue DC Kwa kukiuka agizo lake.
Kaka watu wanaogopa kufanya maamuzi ya aina yoyote
1: Mmoja kasema kuna Zika kafutwa kazi
2:Mmoja kaogopa kuripoti mambo ya Kipindupindu Kafutwa kazi
3: Mramba Kasign Barua ya kuomba ongezeko la bei ya umeme, na EWURA wakaizinisha hiyo bei, Aliyeomba Kafukuzwa na walikubali na kupitisha hiyo bei wanapeta