Watoto wengi wa matajiri wanasoma sana lakini elimu yao haiwasaidii... according to my experience thouUkisoma PCB halafu ukaenda BCom in marketing hautaona maana ya dissection za vyura ulizofanya A level.
Hao ambao hawajasoma halafu wakawa Matajiri,wanahakikisha watoto wao wanasoma kweli kweli.
Tunasoma masomo 9 boss!! Na mitaala yetu ilivyo.. ni ngumu sana kufaidika na kile unachosoma.Unaipata mara nyingi tu sema shida yako ni kutoitambua. Ukijua purpose/ goal ya wewe kufundishwa hiyo equation na equations nyingine nyingi utaona zinavyokusaidia kwenye maisha.
Thamani ya X ni mafanikio, ambayo nilitarajia kuyapata kutokana na kusoma kwa bidii.Kiuhalisia nimegundua thamani ya X haipatikani kwa kusoma sana.Haaa... saman ya X unaitumia kila cku.. hata ulichoandika hapo ni saman ya X.. X inakupa nafas ya kufikiria sana.. kama ulivyoweza kufikiria kuandika hvyo vitu ... hii ni sawa na kusema kidole cha kati cha mguu wako hakina faida... sasa ebu siku kikatike ndio utajua....
Utoto huu .Tuchukulie mfano unafanyika utafiti leo hii.... ni vitu vingapi tulivyojifunza shule (ya msingi, sekondari O - level na Advance Level) vinatusaidia katika maisha ya kila siku?
Najaribu tu kuwaza kwa sauti... mpaka leo sijawahi kutumia Four Figure, wala logarithm, wala Calculus, wala Quadratic na nimejaribu sana kupata thamani ya X katika maisha... sijaipata.Daah!!
Nimetambua kuwa elimu niliyopata iliniandaa kuajiriwa na serikali na sio kujiajiri.Yaani mfumo mzima wa elimu umetengenezwa kukidhi mahitaji ya serikali na sio kukidhi mahitaji yangu.SMH!!
Hapo ndipo nakubaliana na bwana mmoja aliesema,"Tanzania wenye elimu wapo, lakini kati yao wasomi ni wachache sana" Eee si ndio... asa kumbe nini; watu wana degree zao na haziwasaidii chochote katika maisha.
Hivi: 'Marking scheme' inasaidia kupanua uwezo wa mwanafunzi kufikiri au inabana?
Unakumbuka kibao cha shuleni kwenu... kiliandikwaje?... Elimu ni ufunguo wa maisha / Elimu ni utajiri /Elimu ni urithi wa kweli n.k
Swali ni je, mwalimu masikini anaweza kukupa wewe mbinu za kufanikiwa katika maisha? Au mpaka sasa umeshawahi kufundishwa na walimu matajiri wangapi?
Wasomi wanaishia kuajiriwa na wasiosoma.Wasomi wana elimu sana, wasiosoma wana fedha nyingi.Yaani wale waliokuwa wanapata A darasani huwa wanaishia kuajiriwa na wale waliokuwa vilaza!!! Aisee yaani..Ni nadra sana kumkuta tajiri alieajiriwa.
Baba yako alikwambia soma sana uje kuwa na maisha mazuri,... mimi nasemaje; soma sana nije nikuajiri unisaidie kutafuta thamani ya X.
Let X be valuable papers(Money)Tumia "Pie" = 3.14!!!
Mimi.. ninashukuru.
Hujasema unasoma ili iweje kwa hiyo? Usiogope kuukubali ukweli kuwa... tunaposema mtu ana mafanikio kwa vyovyote vile hata ukwepe vipi lazima pesa ihusike.Acha unafiki mzee, nani alikwambia mafanikio ni PESA?? Unaesema elimu haina msaada mbona hata wanao utawapeleka shule tena za gharama wapate elimu hiyo hiyo? Elimu haipo kwa ajili ya kukupa hela na hakna ilipoandikwa kwamba education is MONEY. Tafakari upya
Kwanini nisome kitu ambacho sitakuja kukitumia maishani?Lengo la elimu hiyo ya awali ni kukufanya uwe na welewa wa jumla angalau wa kijuujuu wa mambo ya msingi hapa duniani, katika mazingira yako na hukooo katika malimwengu mengine. Ukitaka kuzama zaidi sasa ndiyo unaanza kujibana katika uwanja wako uliochagua katika shahada ya kwanza, unajibana zaidi katika Masters na unachagua kaeneo kadogo zaidi katika PhD.
Hisabati na hii x unayoilalamikia lengo lake ni kuimarisha uwezo wako wa kufikiri kidhahnia (abstract reasoning). Uwezo huu peke yake ndiyo unamtofautisha binadamu na wanyama wengine wote na ni uwezo wa muhimu sana kwa binadamu. Ndiyo maana karibu dunia nzima wanafunzi ni lazima angalau wafundishwe kidogo kuhusu udhahnia huu kupitia somo la Hisabati ambalo kulingana na akina Albert Einstein ndiyo "lugha ya Mungu!"
Kuhusu utajiri, elimu haina lengo la kumfanya aipataye atajirike. Lengo lake hasa ni kumwonyesha aipataye kuhusu mambo ya msingi katika dunia hii na kumfanya kuyatawala mazingira yake. Ni Afrika tu ambako elimu inaonwa haina faida na eti lengo lake ni kuufikia utajiri. Ukienda Ulaya na Marekani utagundua mapema sana kwamba kumbe profesa anaweza asimiliki hata gari na hategemewi kuwa tajiri. Profesa huyu huyu utamkuta anashinda lab mpaka siku moja anagundua kitu kinachosukuma mbele maarifa na ujuzi wetu hapa duniani. Sisi tumekazana kutajirika, wenzetu wamekazania maarifa na kuhakikisha kuwa kizazi kipya kinaandaliwa sawasawa. Tungeiacha elimu angalau ikafanya lengo lake badala ya kuivika hili joho chafu la ubinafsi na utajiri, pengine ingeweza kutusaidia katika ukombozi wetu. Tunazalisha wasomi wazuri sana lakini wote lengo lao ni kutajirika ndiyo maana haoo wanakimbilia kwenye siasa ili wakafisadike huko na kutajirika. Waafrika tuna matatizo. Hata tunavyofikiri ni matatizo tupu. Inasikitisha!!!
Na kama lengo kuu la elimu ni kutajirika, hakuna hata sababu ya kwenda shule!