Siku moja nikiwa ndo kwanza nimetoka kazini, nilipofika nyumbani sikumkuta mke wangu wala watoto wangu. Lakini chini ya mti wa mchungwa kulikuwa na beseni ambalo ndani yake palikuwa pamejaa maji na katika kutazama kwangu ndani ya hilo baseni, nikaona kulikuwa na mjusi. Nilipowaza sana kwa namna gani amefika ndani ya lile beseni, niliona hakuna uwezekano wa kuwa amefika mle kwa kuapnda kutokea chini, na nilipokuwa bado nawaza namna ambayo alifika ndani ya lile beseni, ndipo nilipotazama kwa upande wa juu wa beseni kulikuwa na matawi ya mti wa mchungwa, ndipo nilipogundua kuwa yule mjusi alianguka ndani ya lile beseni wakati alipokuwa katika harakati zake za kucheza. Na katika kutazama sana, niligundua ya kwamba, yule mjusi alikuwa wa kike, kumbe inawezekana kabisa ya kuwa alikuwa na mme wake wakiwa wanacheza ndipo alipoteleza na kuangukia ndani ya beseni. Na kipindi nilipomkuta yule mjusi, alikuwa amevimba tumbo kutokana na kumeza maji mengi sana hivyo alishindwa hata kutembea, nami nikaanza kuwaza namna ya kumtoa ndani ya lile beseni maana hakuwa na msaada baada ya mmewe kumkimbia, ndipo katika kuwaza namna ya kumtoa kwenye maji, nikafikiria niyamwage yale maji, lakini nikaona ya kuwa haitakua njia nzuri ya kumtoa. Ndipo nikiwa katika kuwaza nikapata wazo, nikatafuta mti ambao niliamua kuuingiza ule mti ndani ya beseni na katika hali ya utulivu kabisa ili yule mjusi asijue kama kuna kitu kipya ndani ya himaya yake, nilifumba macho yangu lakini kumbe ule mti ulisababisha mawimbi ambayo yalimsitua yule mjusi hivyo akaanza kutafuta chanzo cha mawimbi yale. Nikamuona akaanza kujivuta kwa shida kuelekea kwenye ule mti, n alipoufikia, nikamuona akianza kutupa mguu wake mmoja katika ule mti, baadaye akatupa na mguu wa pili baada ya hapo nikaona akaanza kujivuta kiwiliwili chake ili kiwe katika ule mti na alipofanikiwa akaanza kujivuta taratibu katika mti ule na hatimaye akawa amefanikiwa kujitoa ndani ya beseni na hatimaye akaangukia chini. Na alipofanikiwa kuanguka chini, taratibu akaanza kuangaza huku na kule ili kumtafuta aliyemuokoa, hatimaye akawa amekutanisha nami macho yake na aliponiona akajivuta karibu yangu na hatimaye akainua miguu yake ya mbele kama shukrani kwangu.
Kesho yake nikiwa nimeshasahau juu ya yule mjusi, nilifika nyumbani na nilipofungua tu mlango nikashangaa kumkuta mjusi ili hali si kawaida kukuta mjusi katika nyumba yangu, nami nilipomuona, nikamtazama sana ndipo nikamkumbuka kuwa ndiye yule mjusi wa jana yake naye alipogundua kuwa nimemkumbuka, alisogea karibu yangu na akainua miguu yake ya mbele kisha akacheka sana, na baada ya kucheka akakimbilia hadi chumbani kwangu na baadaye alipokuja mke wangu nilimuambia ya kwamba tumepata mgeni kwa hiyo akimuona mjusi ndani ya nyumba yetu asimuue.
Ndipo baada ya muda nilihamishwa kikazi, siku nahamisha mizigo yangu, nikiwa najiandaa kuiweka ndani ya gari, nilishangaa nilipomuona mjusi akikimbia kuelekea vyombo vyangu.
Kesho yake nikiwa nimeshasahau juu ya yule mjusi, nilifika nyumbani na nilipofungua tu mlango nikashangaa kumkuta mjusi ili hali si kawaida kukuta mjusi katika nyumba yangu, nami nilipomuona, nikamtazama sana ndipo nikamkumbuka kuwa ndiye yule mjusi wa jana yake naye alipogundua kuwa nimemkumbuka, alisogea karibu yangu na akainua miguu yake ya mbele kisha akacheka sana, na baada ya kucheka akakimbilia hadi chumbani kwangu na baadaye alipokuja mke wangu nilimuambia ya kwamba tumepata mgeni kwa hiyo akimuona mjusi ndani ya nyumba yetu asimuue.
Ndipo baada ya muda nilihamishwa kikazi, siku nahamisha mizigo yangu, nikiwa najiandaa kuiweka ndani ya gari, nilishangaa nilipomuona mjusi akikimbia kuelekea vyombo vyangu.