Mafyangula
JF-Expert Member
- Jan 16, 2025
- 505
- 887
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kinondoni kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma(CHAUMMA), Moza Ally amesema akichaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo atahakikisha anasimamia huduma ya mama na mtoto kuwa bure kikamilifu kama ambavyo inatakiwa.
Moza ameyasema hayo leo Septemba 29, 2025 akizungumza na wananchi wa eneo la Kigogo akisema "kwenye afya tuliambiwa huduma ya Mama na mtoto ni bure, nitakwenda kusimamia kama walivyosema huduma ya mama na mtoto ni bure nitasimamia hii huduma ikawe bure kweli kweli bila kupepesa macho" amesema Moza.
Moza ameyasema hayo leo Septemba 29, 2025 akizungumza na wananchi wa eneo la Kigogo akisema "kwenye afya tuliambiwa huduma ya Mama na mtoto ni bure, nitakwenda kusimamia kama walivyosema huduma ya mama na mtoto ni bure nitasimamia hii huduma ikawe bure kweli kweli bila kupepesa macho" amesema Moza.