Movie hii ni kichefuchefu!!!

Movie hii ni kichefuchefu!!!

Salathiel m.

Senior Member
Joined
Mar 12, 2011
Posts
185
Reaction score
41
Hii muvi inaitwa CID,ni ya kibongo yani inakatisha sana tamaa hvi inamaana hua hawa jamaa hawaangalii kazi za wenzao wa nje? hadi nikaona aibu kwa maana wenzetu wa nchi zingine wakiona watatudharau sana,kwasababu kuna action zingine hata mtoto humdanganyi alafu hata continuety ni hovyo ingawa kabla haijatoka waliisifia nadhani ni kwakua kuna matumiz ya siraha ambazo walikua wanaonekana wanapigapiga kama ile michezo ya watoto na pisto za maji!! jifunzeni kwa kuangalia kaz za WENZENU WA NJE KAMA AMUWEZ ENDELEENI NA MUVI ZENU ZA MAPENZI!!!
 
Another calamity hapa nchini ni bongo movies!! Puuuuuuuuuuuu, huwa sipotezi muda wangu ku-watch hiyo makitu!
 
Bongo movie,bongo lala sanaa isiyo vigezo na ubongo hautumiki
 
wameshashauriwa hawa watu lakini hawauzingatii huo ushauri. Movie za kibongo zinatia kinyaa. Mara nyingi hizi movie zinapendwa kuangaliwa na watoto, wanafunzi pamoja na wanawake hasa wa uswahili.
Wakiulizwa kwa nini wanatengeneza movie kama hizi wanasingizia teknolojia upumbavu tu
 
Nikiwaga kwenye basi kama nasafiri huwa natupiaga macho hizo muvi za kibongo..Mbali na hapo naonaga tuu zinapangwa kwa bara bara..
 
wameshashauriwa hawa watu lakini hawauzingatii huo ushauri. Movie za kibongo zinatia kinyaa. Mara nyingi hizi movie zinapendwa kuangaliwa na watoto, wanafunzi pamoja na wanawake hasa wa uswahili.
Wakiulizwa kwa nini wanatengeneza movie kama hizi wanasingizia teknolojia upumbavu tu


kichaa au mweneakili punguani ndo anaweza kufuraishwa na muvi hizi
 
Mie naona ni upuuzi tu no seriousnes ya ku improve bongo movies. hakuna na hii inaonekana wazi kabisa. hawa watu hawajifunzi namna nzuri au mpya ya kubadilika. watumiaji ambao ni watazamaji wamesha badilishwa na wadau wengine wa nje kwa sababu ya mitandao na TV za nje. ila wao wameachwa mbali. time is not with them. If you dont change you remain where you where.
 
Tv nyingi hapa Tz zinaonyesha Telenovela nzuri sana za South America zenye visa vilivyopangika kiasi cha kukuondolea Stress ie India Love Story ukiiangalia huwezi amini wameigiza Wabrazil. Bongo Movie wanashindwa nini kuiga nao watunge story kama hizo? Nendeni Brazil mkajifunze kuigiza.
 
Hii muvi inaitwa CID,ni ya kibongo yani inakatisha sana tamaa hvi inamaana hua hawa jamaa hawaangalii kazi za wenzao wa nje? hadi nikaona aibu kwa maana wenzetu wa nchi zingine wakiona watatudharau sana,kwasababu kuna action zingine hata mtoto humdanganyi alafu hata continuety ni hovyo ingawa kabla haijatoka waliisifia nadhani ni kwakua kuna matumiz ya siraha ambazo walikua wanaonekana wanapigapiga kama ile michezo ya watoto na pisto za maji!! jifunzeni kwa kuangalia kaz za WENZENU WA NJE KAMA AMUWEZ ENDELEENI NA MUVI ZENU ZA MAPENZI!!!
hapo kwenye red inabidi ukumbuke kitu kimoja, kujifunza kuna mawili: kuelewa au kutoelewa! Anayejifunza akaelewa maana yake ni kuwa ana akili na hao huwa ni wachache bali wasioelewa (wasio na akili) ndio wengi.
Hawa wenzetu ukiangalia wengi wanaoingia huko ni wale waliokwishapoteza mwelekeo wa maisha (STD VII failure, Form IV failure) na tutegemee wengi zaidi kama Dr. Kawambwa atatekeleza azima yake ya kuwa mtu akifail FORM II mara mbili anafukuzwa kabisa.
Lakini, nao sio makosa yao bali ni mfumo mbovu tuliojenga wa nchi wa kuzalisha wajinga wengi ili watawalike kirahisi badala ya waelevu ambao wanaweza kudai haki zao
 
tena bora kuangalia walau muvi za kina mzee majuto au kina bambo sababu unaweza hata kutabasamu kwa misemo yao kuliko hizi zingine...unaishia kuchambua makosa tu badala ya kutizama...hell!!
 
Nilifikiri nipo mwenyewe ninayeonaga kichefuchefu kwenye hizi muvi loh,
ni zaidi ya upuuzi, muvi ukiangalia kwa dakika 5-10 za kwanza unaweza kujua inaishia wapi...Continuity zero, missions za kufikia target ya muvi zero, subtitle zero...
Utakuta muvi inaanza vyema tu mfano "kuna jamaa anauza madawa ya kulevya, ana kikundi cha magaidi n.k....sasa nategemea nianze kuona harakati za kipelelezi ikiambatana na misukosuko yakutosha" chakushangaza unakuta jamaa kaenda kutubu kanisani "eti ndio akakamatwa"
Hawajui kujenga hata uhalisia wa maisha ya kawaida "kuna wasanii hawapendi ku-act kama wanamaisha ya hali ya chini...unashangaa mtu anaenda kuomba kazi restaurant lakini anaishi kwenye jumba la kifahari
Eti jamaa anapewa kazi ya kumtafuta mtu fulani tena aliyekimbilia katka jiji kubwa kama Dar es salaam....ningetarajia nione misheni za kutosha matumizi ya GPS ili kumtrace kwa mfano..lakini jamaa anatua Dar anauliza anaambiwa anaishi magomeni sekunde chache keshamkata,,,stupid!!
halafu wanatarajia wauze
 
From Bongo movie scine ''You are bogus, tena boga lenyewe lililooza'' Yaani ni kichefuchefu. Na hiyo ni movie ya super star wao aliyehai. Bahati nzuri nilikuwa kwenye bus nasafiri. Vitu vidogo vya lugha kama hivyo vinashindikana, camera trick zitawezekana kweli!! Bm ni big time kinyaa. Yaani acha tu.
 
Uwezo wa kuiga wautoe wapi? Upeo wa films hawana na hawatak kujifunza,sasa wategemea waproduce movie za viwango kwel? Sitazami the so called bongo movies kamwe!
Tv nyingi hapa Tz zinaonyesha Telenovela nzuri sana za South America zenye visa vilivyopangika kiasi cha kukuondolea Stress ie India Love Story ukiiangalia huwezi amini wameigiza Wabrazil. Bongo Movie wanashindwa nini kuiga nao watunge story kama hizo? Nendeni Brazil mkajifunze kuigiza.
 
ndo maana mwisho wa yote wanakuwa wabwia unga
hmna wanachokifanya zaidi ya ukahaba kwa mtu mwenye akili timamu sijui kama ana muda huo wa kuangalia!
 
Zitakuwaje nzuri, muvi ambazo zina majina ya kizungu lakini ndani story ni kiswahili, ukiangalia muvi inachezwa kwa mfano maeneo matatu tu sinema nzima, utakuta labda nyumbani kwa star, kanisani, hospitali basi yaani scene zote zinacheza maeneo hayohayo tu mpaka muvi inaisha. bila kusahahu kila muvi lazima iwe na party two:target::target:
uozo mtupu.
 
Wanakoelekea siko kabisa cz siku hizi ukiwa maarufu tu unaitwa kuigiza, mi binafsi huwa naita kuuza sura.
We fikiria mtangazaji siku hizi ni muigizaji na yeye anafilamu zake, mwanamuziki naye anatengeneza muvi zake kuna nini tena hapo zaidi ya kuuza sura, ili Global Publisher awaone awaandike kwenye magazeti wapate madeshee wa kuwalea, wenyewe wanakwambia muvi zinatuletea wanaume, kwa hiyo hawana wazo la kuenda kujiendeleza kwa sababu suala si la kutengeneza filamu bora ila ni kuuza sura.
 
Nilifikiri nipo mwenyewe ninayeonaga kichefuchefu kwenye hizi muvi loh,
ni zaidi ya upuuzi, muvi ukiangalia kwa dakika 5-10 za kwanza unaweza kujua inaishia wapi...Continuity zero, missions za kufikia target ya muvi zero, subtitle zero...
Utakuta muvi inaanza vyema tu mfano "kuna jamaa anauza madawa ya kulevya, ana kikundi cha magaidi n.k....sasa nategemea nianze kuona harakati za kipelelezi ikiambatana na misukosuko yakutosha" chakushangaza unakuta jamaa kaenda kutubu kanisani "eti ndio akakamatwa"
Hawajui kujenga hata uhalisia wa maisha ya kawaida "kuna wasanii hawapendi ku-act kama wanamaisha ya hali ya chini...unashangaa mtu anaenda kuomba kazi restaurant lakini anaishi kwenye jumba la kifahari
Eti jamaa anapewa kazi ya kumtafuta mtu fulani tena aliyekimbilia katka jiji kubwa kama Dar es salaam....ningetarajia nione misheni za kutosha matumizi ya GPS ili kumtrace kwa mfano..lakini jamaa anatua Dar anauliza anaambiwa anaishi magomeni sekunde chache keshamkata,,,stupid!!
halafu wanatarajia wauze


Naona hawakuuzi kama mimi uvaaji wa nusu uchi ndio kichefuchefu kabisa, na zile lugha zao za bebii bebii yaani nakereka vibaya
 
Movi gani hata glasi hawavunji

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
wacheza muvi wa kibongo nao wanaingia kwenye muziki na waimba muziki nao wanaingia kwenye movie. dah! full usanii!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom