Mothers' day 2014

Dark City

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2008
Posts
16,252
Reaction score
11,648
Ndugu zangu wapendwa,

Bado siku saba kamili kufikia kilele cha siku ya wamama wote duniani. Ingawa hapa Bongo ni jambo geni, siyo vibaya kukamatana nalo kwa vile ni jema, tena jema sana!

Kwa mwaka huu, naomba nichukue nafasi hii ya kipekee (in advance) kuwatakia heri wanawake wawili ambao hawana mtu wa kulinganisha naye katika maisha yangu. Hawa ni Bibi DC ambaye siku hiyo atakuwa anasherehekea pia siku yake ya kuzaliwa na Mama mzazi wa DC ambaye atakuwa anatimiza umri wa miaka kama 90 hivi!! Hawa wamama wawili ndio ambao wamemfanya babu DC huyu huyu awe kama mnavyomwona! Nina deni kubwa kwenu mama zangu (mazazi na mlezi wa ukubwani)!

Naomba pia kuwapongeza wanawake wote ambao wanaendelea kujitoa kwa kiwango cha hali ya jukuu kushiriki tendo tukufu na takatifu la kuleta uhai katika dunia hii. Mungu awabariki sana na awape faraja katika kutimiza majumu yenu ya umama!

Pia tuwaombee wanawake wote ambao wamejaribu sana kupata nafasi hiyo ya umama ila wameshindwa. Mungu aendelee kuwapigania!

Kwa ufupi sana, hakuna kama mama ila jukumu hilo na sifa za umama zina gharama kubwa ambayo wengi wenu mmeikubali pasipo kuukimbila msalaba!

I wish you a very happy mothers' day 2014!

Babu DC!!
 
nampenda sana mama yangu.
naungana na wasanii mbalimbali ktk kuwasimia mama zetu:

Bon Mwaitege "MAMA NI MAMA"
2PAC "Dear Mama"
TILDA " Sweet Mother"

Hakuna kama mama!
 
Kwan kuna mtu anayemchukia mama yake?lete thread yenye akili...loading error...
 
nampenda sana mama yangu.
naungana na wasanii mbalimbali ktk kuwasimia mama zetu:

Bon Mwaitege "MAMA NI MAMA"
2PAC "Dear Mama"
TILDA " Sweet Mother"

Hakuna kama mama!

Ni kweli mkuu...nina jamaa zangu ambao wameishia kuwa kama vichaa kwa kuwatelekeza mama zao.

Nimekuwekea baadhi ya hizo nyimbo


 
Last edited by a moderator:
Hakika hakuna kama mama,nami nawapongeza wanawake wote dunian,tusichoke na tusikate tamaa Mungu yupo nasi,familia yatutegemea,jamii yatutegemea,nyumba za ibada zatutegemea na taifa kwa ujumla latutegemea.

Dedication: God bless women by Lucky Dube.
 
Ni kweli mkuu...nina jamaa zangu ambao wameishia kuwa kama vichaa kwa kuwatelekeza mama zao.

Nimekuwekea baadhi ya hizo nyimbo


asante mkuu kwa nyimbo. be blessed!
may my mother's soul rest in peace!
 
Last edited by a moderator:
Shida mama yangu bandidu, ukimwambia happy mothers day anakwambia kwani KUNA POSHO?

Basi nakausha, najisemea kimoyomoyo
 
Upuuzi mtupu, yaani munapenda mama zenu mwaka mara moja ?

Waafrika acheni kuiga Wazungu. 👠
 
Upuuzi mtupu, yaani munapenda mama zenu mwaka mara moja ?

Waafrika acheni kuiga Wazungu. 

Hahahahahahaahah,

Hivi unaelewa unachoandika wewe?

Nani kasema anampenda mama siku moja kwa mwaka tu?

Kama huna cha maana cha kuchangia, kwa nini usipite tu?
 
Nakuombea kwa Mola akupe uhai mrefu mama yangu!
Nawapenda na kuwaheshimu kina mama wote!
 
pongezi kwa aliyekuzaa kwa kumkumbuka,mama hafananishwi,kwani kama watoto wote wangekuwa wanajua jinsi mama zao wanavyoumia siku ya kuwaleta duniani sidhani kama kungetokea mtoto ambaye angemdharau mama yake!! NAKUPENDA SANA MAMA.
 
Nakuombea kwa Mola akupe uhai mrefu mama yangu!
Nawapenda na kuwaheshimu kina mama wote!


Natamani watu wote wangechukua walau muda katika maisha yao kuwaonesha mama zao upendo. Mama ni zaidi Mzazi...ni rafiki, mlezi, mwalimu, mfariji na kimbilio lenye uhakika usio na shaka.

Hata vibaka waonaochomwa moto, mama zao huwalilia sana!

Proud to see Mama in her old age!
 
pongezi kwa aliyekuzaa kwa kumkumbuka,mama hafananishwi,kwani kama watoto wote wangekuwa wanajua jinsi mama zao wanavyoumia siku ya kuwaleta duniani sidhani kama kungetokea mtoto ambaye angemdharau mama yake!! NAKUPENDA SANA MAMA.

Safi sana Mkuu,

Nafarijika kukutana na watu wanao-appreciate mchango wa mama zao katika maisha yao!

Ila kuna jamaa yangu alimtelekeza mama yake hadi akaaga dunia bila msaada wakati alikuwa na uwezo wa kumsaidia kwa kiwango kikubwa!
 
Babu kwanza nimekumiss.pili nimekununia!

Ila nimekusamehe kwa kuleta hili sredi!
Mi mamangu ndo Dah!ila najua alipo she is proud of me!
Kwa wanaosababisha niitwe mama,kisses kwao mingi!
They are my rocks!
 
Nakupenda mama yangu,nakushukuru sana kwa kunileta duniani,kunilea vizuri sana na kunifikisha hapa nilipo,siwezi kukulipa mama,nakuombea kwa Mola maisha marefu ya baraka tele!Hamna kama mama!

Nawapongeza wamama wote kwa malezi ya watoto wenu na kuzilea familia zenu!Mungu Awabariki sana!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…