Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,252
- 11,648
Ndugu zangu wapendwa,
Bado siku saba kamili kufikia kilele cha siku ya wamama wote duniani. Ingawa hapa Bongo ni jambo geni, siyo vibaya kukamatana nalo kwa vile ni jema, tena jema sana!
Kwa mwaka huu, naomba nichukue nafasi hii ya kipekee (in advance) kuwatakia heri wanawake wawili ambao hawana mtu wa kulinganisha naye katika maisha yangu. Hawa ni Bibi DC ambaye siku hiyo atakuwa anasherehekea pia siku yake ya kuzaliwa na Mama mzazi wa DC ambaye atakuwa anatimiza umri wa miaka kama 90 hivi!! Hawa wamama wawili ndio ambao wamemfanya babu DC huyu huyu awe kama mnavyomwona! Nina deni kubwa kwenu mama zangu (mazazi na mlezi wa ukubwani)!
Naomba pia kuwapongeza wanawake wote ambao wanaendelea kujitoa kwa kiwango cha hali ya jukuu kushiriki tendo tukufu na takatifu la kuleta uhai katika dunia hii. Mungu awabariki sana na awape faraja katika kutimiza majumu yenu ya umama!
Pia tuwaombee wanawake wote ambao wamejaribu sana kupata nafasi hiyo ya umama ila wameshindwa. Mungu aendelee kuwapigania!
Kwa ufupi sana, hakuna kama mama ila jukumu hilo na sifa za umama zina gharama kubwa ambayo wengi wenu mmeikubali pasipo kuukimbila msalaba!
I wish you a very happy mothers' day 2014!
Babu DC!!
Bado siku saba kamili kufikia kilele cha siku ya wamama wote duniani. Ingawa hapa Bongo ni jambo geni, siyo vibaya kukamatana nalo kwa vile ni jema, tena jema sana!
Kwa mwaka huu, naomba nichukue nafasi hii ya kipekee (in advance) kuwatakia heri wanawake wawili ambao hawana mtu wa kulinganisha naye katika maisha yangu. Hawa ni Bibi DC ambaye siku hiyo atakuwa anasherehekea pia siku yake ya kuzaliwa na Mama mzazi wa DC ambaye atakuwa anatimiza umri wa miaka kama 90 hivi!! Hawa wamama wawili ndio ambao wamemfanya babu DC huyu huyu awe kama mnavyomwona! Nina deni kubwa kwenu mama zangu (mazazi na mlezi wa ukubwani)!
Naomba pia kuwapongeza wanawake wote ambao wanaendelea kujitoa kwa kiwango cha hali ya jukuu kushiriki tendo tukufu na takatifu la kuleta uhai katika dunia hii. Mungu awabariki sana na awape faraja katika kutimiza majumu yenu ya umama!
Pia tuwaombee wanawake wote ambao wamejaribu sana kupata nafasi hiyo ya umama ila wameshindwa. Mungu aendelee kuwapigania!
Kwa ufupi sana, hakuna kama mama ila jukumu hilo na sifa za umama zina gharama kubwa ambayo wengi wenu mmeikubali pasipo kuukimbila msalaba!
I wish you a very happy mothers' day 2014!
Babu DC!!