Moshi vijijini hali ya barabara ni mbaya

Moshi vijijini hali ya barabara ni mbaya

SN.BARRY

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2012
Posts
4,048
Reaction score
8,991
Kutokana na ubovu wa barabara kuanzia zara Tours Bogini, Manosa, Kwa Elia hadi Kahe tunaomba msaada wa dharura kwa wahusika wote, Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa wilaya, Mbunge na Madiwani wanaohusika.

Tangu mvua zianze barabara hii imekuwa ni kero kubwa, kuna madimbwi makubwa katikati ya barabara yaani gari ndogo ikipita unaweza kudhani inazama.

Madiwani na mbunge wetu Anthony Komu mko wapi jamani? Igeni Moshi mjini Manispaa wanajenga barabara hadi vichochoroni nyie hata simu hampokei?

Huyo Diwani wa Mabogini ndio hopeless kabisa hata hajielewi ameshindwa hata kuhamasisha wananchi wake tuchangie(kama kweli Halmashauri haina hela) hali ni mbaya sehemu ya kutembea kwa dakika kumi kwa bajaji tunatumia saa nzima.

Jamani tusaidieni.
 
MH. MKUU WA MKOA MAMA MGHWIRA MSAADA WAKO TAFADHALI...
 
Kilimanjaro hatujui shida ndgondgo ka hizo
n kutokana na mvua za masika nyingi za gafla ndio maana,tutalitatua haraka
kumbuken Kilimanjaro lami IPO tangu kabla ya Uhuru hadi vichochoroni
cc chuma cha mjerumani
 
Inasikitisha sana, kuna watu wanachukulia poa..ila kwenye kampeni wakija utawasikia "nichagueni nitawawekea lami" ila akishapewa anahamia Dar...

Ujinga sana huu ndio maana wengine siasa tumezipotezea
We acha tu ndugu yangu..natamani aje mtu mwingine anayeifahamu hiyo barabara ya ipo ovyo kweli kweli na mamia ya watu wanaitumia kila siku..Anthony Komu Mungu anakuona..uliahidi makubwa umeingia ila umeingia mitini. Kama upo Moshi pita hiyo barabara uone.
 
Kilimanjaro hatujui shida ndgondgo ka hizo
n kutokana na mvua za masika nyingi za gafla ndio maana,tutalitatua haraka
kumbuken Kilimanjaro lami IPO tangu kabla ya Uhuru hadi vichochoroni
cc chuma cha mjerumani
Acha kudanganya watu, njoo huku shia gari haitembei full utelezi, nenda kirua, njoo sembeti ...... Hizo blah blah blah kadanganye wengine.
 
Inasikitisha sana, kuna watu wanachukulia poa..ila kwenye kampeni wakija utawasikia "nichagueni nitawawekea lami" ila akishapewa anahamia Dar...

Ujinga sana huu ndio maana wengine siasa tumezipotezea
Hiyo ni kanda gani awamu hii ni ya wanyonge kwani kaskazini kuna wanyonge
 
Magu anasomomeka hadi uarabuni ...teh, teh, teh hii sasa ni minyororo haswa na inakata hadi shingo
 
Kutokana na ubovu wa barabara kuanzia zara Tours Bogini, Manosa, Kwa Elia hadi Kahe tunaomba msaada wa dharura kwa wahusika wote, Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa wilaya, Mbunge na Madiwani wanaohusika.

Tangu mvua zianze barabara hii imekuwa ni kero kubwa, kuna madimbwi makubwa katikati ya barabara yaani gari ndogo ikipita unaweza kudhani inazama.

Madiwani na mbunge wetu Anthony Komu mko wapi jamani? Igeni Moshi mjini Manispaa wanajenga barabara hadi vichochoroni nyie hata simu hampokei?

Huyo Diwani wa Mabogini ndio hopeless kabisa hata hajielewi ameshindwa hata kuhamasisha wananchi wake tuchangie(kama kweli Halmashauri haina hela) hali ni mbaya sehemu ya kutembea kwa dakika kumi kwa bajaji tunatumia saa nzima.

Jamani tusaidieni.
Sasa hivi ujenzi wa barabara uko chini ya mamlaka maalumu, siyo mbunge wala diwani, Ila kwakuwa nia yako ilikuwa ni kumtukana diwani wako basi umeufurahisha moto wako.
 
Inasikitisha sana, kuna watu wanachukulia poa..ila kwenye kampeni wakija utawasikia "nichagueni nitawawekea lami" ila akishapewa anahamia Dar...

Ujinga sana huu ndio maana wengine siasa tumezipotezea
Ukiipotezea siasa maana yake umekubali kupelekeshwa....
 
Back
Top Bottom