MOI Wajiunga Tena na MGOMO


masaburi yanakusumbua nyau wewe.
 
Hata kama JK na serikali yake ina kiburi, kitu kimoja ambacho kinatoa faraja ni kuwa wako sleepless kwa zaidi ya wiki.
Na hapa bado bajeti zake za wizara mbalimbali hazijakwamishwa.
 
Acheni upotoshaji,

Hakuna mgomo wa madaktari.
inakusaidia nini kukaa na utu uzima wako ukaanza kutuandikia uongo humu? haya mambo sio ya utani fisi wewe, mtu anaweza akakuamini akamtoa mgonjwa wake kutoka mbagala mpaka moi usiku wa manane akafika MOI akakuta hakuna kazi, na mgonjwa wake akamfia! bora umuache na ukweli ili at least ajipange angalau kumpeleka private moja kwa moja! SIO VIZURI KUPOTOSHANA WENYEWE KWA WENYEWE! UKOMEEEEEE!!!
 
tupunguze jazba wakuu,aliyefika MOI asubuhi hii atupe updates
 
Kwani afya ya Ulimboka ni muhimu sana kuliko afya za wagonjwa walioko hapo muhimbili?
Watanzania siasa zinatudanganya. Hivi kwa mawazo yako, kama kuna ajali imetokea hospitalini, daktari na mgonjwa asiye daktari, unadhani jitihada za uokozi zitaelekezwa wapi? Jeshini wakati wa vita tunasema ni aheri kupoteza askari 1000 kuliko kumpoteza brigade commander mmoja, na ni aheri kupoteza raia 100 kuliko kupoteza askari mmoja. Hapa thamani ya binadamu inapimwa katika uwezo wa kupigana na kupiganisha. Na katika tiba, thamani ya ubinadamu hupimwa katika uwezo wa uokoaji wa maisha. Katika uhalisia, ni aheri kupoteza wagonjwa 100 kuliko daktari mmoja. Kuokoa maisha ya daktari mmoja ni kuokoa maisha ya raia wengine zaidi ya 1000, lakini kuokoa maisha ya mgonjwa mmoja ni kuokoa maisha ya mtu mmoja.
 
well put
 
Kwani afya ya Ulimboka ni muhimu sana kuliko afya za wagonjwa walioko hapo muhimbili?

Afya ya ulimboka sawa na afya ya wengine, tofauti ipo kwenye mchango wake katika tasnia ya afya amekuwa akipigania maslahi ya watu wote wa wizara ya afya hivyo utumwa wa ubinafsi ameushinda
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…