Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Rais wa Heshima wa Klabu ya Simba SC, Mohammed Dewji (Mo), amesema dhamira yake ya kuijenga Simba kuwa klabu bora barani Afrika haijabadilika, huku akibainisha kuwa tayari amewekeza zaidi ya Sh bilioni 87 ndani ya klabu hiyo tangu mwaka 2017.
"Simba bado ipo kwenye hatua ya ujenzi. Roho ya ushindi haijawahi kuyumba. Tunajipanga upya kwa msimu ujao na kipaumbele kitakuwa kwenye usajili wa kimkakati na kuimarisha benchi la ufundi," amesema Mo.
Ameongeza kuwa mbali na uwekezaji wa mishahara, maandalizi ya timu na matumizi ya uendeshaji, pia ametoa mabilioni kama msaada wa dharura kwa klabu, jambo ambalo halipaswi kupotoshwa au kubezwa.
"Tangu mwaka 2017 hadi sasa, nimetumia Sh bilioni 22 kwa mahitaji ya dharura pekee. Kauli kwamba Mo haitoi hela ni upotoshaji wenye malengo ya chuki," alisisitiza.
Mo pia ametoa wito kwa wanachama na mashabiki wa Simba kuachana na maneno ya chuki na badala yake wajikite katika mshikamano, kushirikiana na kujenga klabu kwa pamoja.
"Nimewekeza muda, jasho, damu na fedha Simba. Sio kwa sababu nyingine, bali kwa mapenzi ya dhati kwa klabu hii na kwa taifa letu. Doto yangu haijabadilika," amesema.
je, unadhani Mo ameingiza kiasi gani tangu 2018?