Qatif
JF-Expert Member
- Dec 16, 2014
- 379
- 859
Rais wa Heshima wa Klabu ya Simba Sports, Mohammed Dewji Mo, kwa mara ya kwanza amezungumzia mahusiano yake na aliyekuwa msemaji wa klabu hiyo Haji Manara na kudai kuwa Manara amekuwa akimtukana na anaendelea kumtukana lakini yeye hana kinyongo naye huku akibainisha kuwa amemsamehe na kwamba amemuachia Mungu.
"Turudi kwa huyu ndugu yetu tumefanya naye kazi vizuri, najua kwamba alikuwa akinutukana na anaendelea kunitukana"
"Lakini Mimi nimemsamehe, kwani maisha ni mafupi, yamepita na hata akiendelea kunitukana mimi namsamehe na siyo yeye kuna wengine pia ambao wananisema vibaya na kunitukana"
"Mimi ni aina ya mtu ambaye siweki chuki ndani ya moyo wangu, Mungu amenijalia vitu viwili, kwanza sina wivu na mtu, pili sibaki na kinyongo, maanake ikitokea jambo mimi nasamehe namwachia mwenyezi Mungu".
Amesema haya MO kwenye sehemu ya mahojiano kuhusu Klabu ya Simba Sports.
"Turudi kwa huyu ndugu yetu tumefanya naye kazi vizuri, najua kwamba alikuwa akinutukana na anaendelea kunitukana"
"Lakini Mimi nimemsamehe, kwani maisha ni mafupi, yamepita na hata akiendelea kunitukana mimi namsamehe na siyo yeye kuna wengine pia ambao wananisema vibaya na kunitukana"
"Mimi ni aina ya mtu ambaye siweki chuki ndani ya moyo wangu, Mungu amenijalia vitu viwili, kwanza sina wivu na mtu, pili sibaki na kinyongo, maanake ikitokea jambo mimi nasamehe namwachia mwenyezi Mungu".
Amesema haya MO kwenye sehemu ya mahojiano kuhusu Klabu ya Simba Sports.