Mnyooshaji nchi upo wapi?

Mnyooshaji nchi upo wapi?

Lituye

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2015
Posts
1,864
Reaction score
5,697
Tafadhali salamu zetu mashetani zikufikie popote ulipo Ndugu Mnyoshaji nchi yetu hii ya kusadikika.

Tangu utuambie unanyoosha hii nchi mambo tunaona yanazidi kupinda tuu wala hayanyooki ndugu mnyoshaji.

Bei ya Sukari inazidi kupaa, Sembe na dona bei hazishikiki tena machozi ya wanachuo waliokosa Ada yanatulowesha Abiria tunao kaa nao ktk siti za vyombo vya usafiri kila siku.

Halafu hali ya usalama kwa mashetani Wa nchi hii ni mbaya. Kuna aina ya Mashetani mabaya yamezuka hivi karibuni hapa ktk kaya yetu.

Mashetani haya mabaya yakikuvagaa mwilini unajikuta upo ktk mfuko wa Sandarusi ukiwa na mawe mazito ndani ya mto fulani ukipumua kwa shida sanaa.

Ulituomba tukuombee Dua Ndugu mnyoshaji sisi mashetani tukaomba usiku na mchana, tukaweka mpaka mikono ya Baraka ktk ile sanamu yako lakini mambo tunaona magumu. Sasa sijui tukuwekee miguu huenda ahueni ikapatikana.

Ndugu Mnyoshaji hebu jaribu kuwa na huruma japo kidogo kwa sisi mashetani japo tuachiepo hata ka Uhuru ka kukutana na kutoa maoni yetu huku tukipiga miayo ya njaa.
 
We mwache tu, hapo kinasubiriwa kitu kidogo tu kitakacho trigger machafuko makubwa kama yale yaliyotokea uarabuni
 
vumilia tu kijana lazima tufanye kazi kweli kweli kuendana na kasi ya raisi wetu mpendwa"hapa kazi tu"
 
Mlizoea kupiga dili sasa hivi mianya imezibwa mnajiita mashetani,na bado mpaka mtajiita nyumbu ,kenge,swala,majina yote mtayamaliza hapa kazi tu hakuna ujanja ujanja mtafungwa
 
Mnyoosha hata kuwa hajui ananyoosha kuelekea wapi au ajui ananyoosha nn. Kiazi ni kiazi tu
 
Watetea mafisadi wa ufipa hata wangepewa miaka 20 kuisoma hiyo sheria wasingekubali kupitisha sheria ambayo itakuja kuwabana wapotoshaji, waongo, wanafiki ,wachawi na mafisadi wenzao wa hapo ufipa
 
Back
Top Bottom