Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni

Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni

Tabby unatatizo kidogo,
Jiulize haya Masawali kuhusu report ya Mwakyembe iliyomgoa Waziri Mkuu Lowasa
1.Mwakembe alisema Richmond ilikuwa ni Kampuni Feki ambayo haikusajiliwa sehemu yoyote Duniani.Je ilikuwa kweli?
2.Je umejiuliza kama Richmond ilikuwa feki Symbion ameinunua Richmond kutoka Kwa Nani?
3.Je waziri wa Mambo ya nje wa Marekani alipokuja kuzindua hiyo mitambo Richmond/Symbion alizindua kitu feki-Wamarekani ni wa hovyo wanaweza kufanya Biashara na Kampuni Feki.
3.Je Hiyo Symbion kama alimnunua Richmond ni kiasi gani cha Pesa alitoa?
5.Je Serikali ilipata Kodi Kiasi gani kutokana na Hayo Mauzo?
Ukiweza kupata majibu ya haya maswali ndio unaweza kutambua watanzania tunavyobuluzwa na Mataifa ya Nje.Wametuvuruga kupitia wanasiasa mpaka Serikali ikakubali Tukampoteza Waziri wetu Mkuu Lowasa,Mataifa ya Magharibi yakachukua Mitambo kirahisi.Na sasa wantuuzia umeme kutoka kwenye Mitambo yetu wenyewe tuliyoikataa.

Kwa style hiyo hiyo wanataka kuichukua IPTL kwa kupitia Wanasiasa Uchwara.

Da kaka unmetoa data vizuri sana, kwani suala hili la Escro watu wanadhani kuwa haya maamuzi ndiyo yatakuwa mwarobaini wa rushwa na ufisadi nchini, kama nchi ni lazima tukaechini na tujitafakari kuweza kuona ni nini cha kufanya na tuache kusolve mambo magumu kwa majibu mepesimepesi na ya harakaharaka ya kisiasa....Hivi kwenye hii nchi nani ambaye siyo mwizi?......
 
Tabby unatatizo kidogo,
Jiulize haya Masawali kuhusu report ya Mwakyembe iliyomgoa Waziri Mkuu Lowasa
1.Mwakembe alisema Richmond ilikuwa ni Kampuni Feki ambayo haikusajiliwa sehemu yoyote Duniani.Je ilikuwa kweli?
2.Je umejiuliza kama Richmond ilikuwa feki Symbion ameinunua Richmond kutoka Kwa Nani?
3.Je waziri wa Mambo ya nje wa Marekani alipokuja kuzindua hiyo mitambo Richmond/Symbion alizindua kitu feki-Wamarekani ni wa hovyo wanaweza kufanya Biashara na Kampuni Feki.
3.Je Hiyo Symbion kama alimnunua Richmond ni kiasi gani cha Pesa alitoa?
5.Je Serikali ilipata Kodi Kiasi gani kutokana na Hayo Mauzo?
Ukiweza kupata majibu ya haya maswali ndio unaweza kutambua watanzania tunavyobuluzwa na Mataifa ya Nje.Wametuvuruga kupitia wanasiasa mpaka Serikali ikakubali Tukampoteza Waziri wetu Mkuu Lowasa,Mataifa ya Magharibi yakachukua Mitambo kirahisi.Na sasa wantuuzia umeme kutoka kwenye Mitambo yetu wenyewe tuliyoikataa.

Kwa style hiyo hiyo wanataka kuichukua IPTL kwa kupitia Wanasiasa Uchwara.

Nimekukubali mkuu.
 
Lazima tutambue kwamba pamoja na matatizo yote ambayo yamekuwa yakiikabili IPTL, na vilevile pamoja na kwamba mitambo ya IPTL bado haijabadilishwa kutoka kutumia mafuta mazito kwenda kutumia gesi, ukweli ni kwamba IPTL imekuwa inauza Umeme kwa bei ya chini kuliko wazalishaji wengine binafsi hapa nchini. Umeme wa IPTL unauzwa US$ 1.06 kwa unit moja ya umeme, ukilinagnisha na Songas US$ 4.31 au Symbion US$ 4.99 au Aggreko US$ 5.70. Ukweli huu ni tofauti kabisa na propaganda iliyoeneza uongo kwamba mradi wa Umeme wa IPTL ndiyo umekuwa ukiwanyonya watanzania kwa kutoza bei kubwa ya Umeme kwa TANESCO

Hapa kuna kitu nimegundua, sasa mbona haya makampuni mengine hayajadiliwi bungeni, au mpaka maslahi ya watu flani yaguswe ndiyo tuanze kusikia sakata la "Songas", "Symbion" au "Aggrecco" kwani kama kweli ndivyo ilivyo basi na huko kunatatizo hivi haya wabunge wetu hawayajui au?...Hatulitendei haki Taifa letu kama ndo hivyo.
 
Hivi ni kitu gani kinachowafanya watu wang'ang'anie kwamba fedha zile ni za umma? Nashindwa kuelewa kabisa! CAG mwenyewe kwenye ripoti yake hajasema kwamba fedha zile ni za umma kwa sababu anajua ni malipo ya tozo ya gharama za uendeshaji wa mitambo ya IPTL. Ni vipi tena zikageuka kuwa za umma?
 
Hivi Watanzania wanafahamu kwamba katika kulinda maslahi ya Taifa na kuhakikisha Watanzania wanapata umeme wa uhakika na kwa bei nafuu kutoka IPTL, Wakati VIP wanauza hisa zao 3 kwa PAP waliweka masharti yafuatayo; PAP ibadilishe mitambo ya kufulia Umeme kutoka kwenye matumizi ya mafuta mazito ambayo ni aghali kwenda kwenye gesi ambayo ni bei nafuu na TANESCO wangekuwa wananunua unit moja ya Umeme kwa US$ cents 6 hadi 8 badala ya US$ 1.06; vilevile VIP iliwataka PAP iongeze uwezo wa kufua Umeme kutoka megawatts 100 hadi 500.
 
Hatuwezi kuendelea kudai kwamba fedha za escrow ni za umma mpaka itakapothibitishwa hivyo. Hata Waziri Mkuu Mizengo Pinda alipokuwa anahitimisha Bunge alisema kwamba Ripoti ya CAG imeacha OMBWE! Ni kwa sababu ripoti ya CAG imesema 'inawezekana kukawa na pesa za Serikali na inawezekana zisiwepo kwenye escrow account'; tofauti na tafsiri iliyochukuliwa na PAC. Kwa mantiki hiyo, sio haki kabisa kuihukumu VIP na Bw. Rugemalira kwamba wamechota pesa ya umma. Isitoshe VIP haikuhusika na mihamala ya Escrow account. VIP iliuza hisa zake kihalali kwa PAP, hata Mahakama ilibariki mauzo hayo, makosa ya VIP yako wapi?
 
Ni vema Watanzania wakakumbuka kwamba suala la deni linatathiminiwa kwa takwimu, sio hisia, propaganda au siasa. Ukiangalia PAC walihitimisha kwamba hela zilizokuwa kwenye Tageta Escrow Account zilikuwa ni za Serikali, lakini PAC haisemi ni kiasi gani cha fedha hizo ni za Serikali. VIP imejithibitishia kwa takwimu kwamba hela zote zilizokuwa kwenye Tageta Escrow Account ambazo ni US$ 122.0 million zilikuwa ni za IPTL na bado IPTL walikuwa wanaidai TANESCO takriban US$ 49.0 million, kitu ambacho TANESCO wenyewe hawapingi kwa sababu wanazo takwimu zinazoonyesha kweli walitumia Umeme wa IPTL kwa kiasi hicho.
 
Kuna uhakika gani kama kweli JK naye atatoa maamuzi ya uhakika kwani naye si ni binadamu kama hao wengine,tunahitaji uchunguzi gani tena hapa,kwanza nahisi hata huo uchunguzi unaofanywa kama kweli unafanyika. Hii nchi imejaa siasa nyingi tu ambazo hazina mwelekao kwenye maslahi ya taifa bali kwa wahusika wenyewe.
 
Back
Top Bottom