Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni; Bravo JK


Kwangu mimi pesa sio jambo la msingi sana, kwani hizo zinatafutwa tu na Tanzania ilivyotajiri tunazo, na kwa kweli kama Mungu angetufunulia kujua ni mabilioni mangapi yameibiwa TZ tungusema na kuthibitisha kuwa EPA ni cha mtoto. Jambo la msingi ambalo watanzania wengi walilitegemea ni hatua za kisheria. Kikwete kushindwa kuwapeleka wezi wa EPA mahakamani kama ambavyo wezi wa kuku wanavyopelekwa ni kielelezo tosha kuwa jamabo la EPA limemshinda. Kwa kweli mimi bado sijaona kama amefanya kitu mpaka sheria ichukue mkondo wake. Wapelekwe mahakamani hata kama hakuna hata shs 1 iliyorudishwa ili liwe fundisho kwa wengine. Kama hawa watarudisha kisha kusamehewa je wakitokea wengine wa namna hiyo itakuwaje? Bwana Pundamilia kuwa mzalendo halisi na uache ushabiki tu.

Historia itakuja kutuhukumu.
 

mzee makamba karibu jf
 

Sisi wote tunaona, tunasikia na tunatafakari, hebu nieleze ni wapi katika hotuba ya Mh. Rais amesema kuwa amewasamehe waliohusika na wizi wa fedha za EPA? Alichosema kuwa amewapa hadi Novemba 1, kuwa wawe wamerudisha hizo fedha na hayo yamo katika ushauri aliopewa katika report ya wasaidizi wake yaani ya akina Mwanyika. Kama ambavyo nimeeleza hapo awali kuwa si kila kitu kilichomo ndani ya ile report aliyokabidhiwa Mh. Rais ni kwa ajili ya matumizi ya Public. Kama sisi ni waelewa wazuri hatuna budi kuiona kazi nzuri iliyokwisha fikiwa hadi sasa. Hajasamehewa mtu kwa mujibu wa ile hotuba, kama ulifuatilia vizuri hati zao za kusafiria zimeshikiliwa ikiwa ni pamoja na vitu vingine. Maamuzi ya Rais juu ya EPA bado yapo katika awamu za utekelezaji, tusubiri baada ya Novemba 1.
 
mzee makamba karibu jf

Sincerely, nimecheka kidogo kusoma ka-ujumbe kako.
Lakini hata hivyo viatu vya yule Mzee ni vikubwa sana kwangu. Mzee makamba anavaa size sawa na Shaqil O'neal ukilinganisha na tumiguu twangu kama vya watoto wa kichina
 


mzee makamba karibu jf
 
Vilevile ni wazi kuwa hatuwezi kusomewa ripoti nzima ya akina Mwanyika kwani huenda kuna mapendekezo mengine kwa sababu maalum hayawezi kutolewa kwenye public kwani yanaweza kuathiri mwenendo mzima wa kukamilisha yale yanayotarijiwa.


Hapo ndipo mashabiki wa JK mnaponiachaga hoi kwa kudhania JK ana uwezo na akili ya ziada sema hajaamua tu!!!!!!!! Historia inatuambia huyu jamaa hajawahi kuaccomplish chochote iwe kwenye uwaziri au huo urahisi.

Pia ukumbuke IMF hao hao pamoja na WB walikuwa ni one of the main forces katika kuiingiza IPTL in the making in Tanzania. Je IPTL imetufikisha wapi??????

Your guy is a failure period.
 

Acha uzushi, hiyo report umeiona wapi?..naomba uthibitishe kuwa unayo ongea una-data zake na si porojo tu za uzushi.
 

Issue hapa ni jinsi alivyoweza kuhandle issue ya EPA na siyo IPTL, sorry!!!
 
Acha uzushi, hiyo report umeiona wapi?..naomba uthibitishe kuwa unayo ongea una-data zake na si porojo tu za uzushi.

Ripoti nimeiona wakati akikabidhiwa.

Nitajie ni lipi ambalo nimeandika hapa kuwa ni porojo?
 
PUNDAMILIAO7
Ukiona umesifiwa na IMF pia ukakaribishwa IKULU YA BUSH (White house) jua nchi imeshauzwa yote.

Pundamilia nakushauri ujiunge na wana-CCM wanaompongeza kwa hotuba yake nzuri na maisha bora kwa kila MTZ wakati majumbani mwao hata kibaba cha unga hawana. Nenda kaandamane ndugu yangu, matokeo hatuhitaji kuambiwa na wewe wakati na sie tunamacho yetu
 



Ukiona umesifiwa na IMF pia ukakaribishwa IKULU YA BUSH (White house) jua nchi imeshauzwa yote.

Hiyo ni dhana kwani haina hata chembe moja ya ukweli juu ya hili tunaloliongelea, nithibitishie kwa kunipa ushahidi kuwa hilo unalodhania ni kweli.

Pundamilia nakushauri ujiunge na wana-CCM wanaompongeza kwa hotuba yake nzuri na maisha bora kwa kila MTZ wakati majumbani mwao hata kibaba cha unga hawana

Mimi si mwana-CCM wala CHADEMA. Inapofikia issue ya kitaifa sitaona aibu kutimiza wajibu kuitetea nchi yangu. Ikibidi kumpongeza Rais nitafanya hivyo kwa kujali utaifa wangu.
 
Mimi si mwana-CCM wala CHADEMA. Inapofikia issue ya kitaifa sitaona aibu kutimiza wajibu kuitetea nchi yangu. Ikibidi kumpongeza Rais nitafanya hivyo kwa kujali utaifa wangu.[/QUOTE]

Kwa hiyo unataka kusema hapo unaitetea nchi siyo? We acha bana. Mafisadi walishaiteka nchi hata Said Mwema alishasema hiko kitu. Hivi unawezaje kusema JK anstahili sifa kwa kuwasamehe mafisadi??? Hivi inaingia akilini kumkamata mwizi kisha kumwambia nirudishie ulichokwiba kisha kumwacha awe huru. Haijalishi kama wezi wa EPA wamerudisha kiasi gani, suala hapa ni kuwawajibisha kama wezi wengine. Nahis IMF ama nao hawajapata habari kamili au JK kawadanganya.Narudia tean, Kosa haliwezi kutokuwa kosa kwa vile mwizi kakurudishia alichokwiba. Hapo ndipo tunapokuona nawewe hujaatazama vizuri hii sakata la EPA, therefore JK hastahili pongezi. He should have done more than what he has done hata kama analinda sana haki za binadamu
 
unampongeza kwa lipi? kwa hili hapa chini?
View attachment 2205
 
Issue hapa ni jinsi alivyoweza kuhandle issue ya EPA na siyo IPTL, sorry!!!


Hii inaonyesha ni jinsi gani ulivyo na uwezo mdogo wa kuelewa mambo. Well kinachoongelewa hapa ni credibility ya hiyo IMF ambayo kwa akili yako ndogo ya kuchambua mambo unafikiri ikitoa tamko basi ni kama limetoka Mbinguni.

Your guy is a failure period.
 
Labda haya maneno ya mkulu hapa chini, yanaweza kutoa changamoto ya kuanzishwa kwa hii topic, na kutusaidia wale tunaoichangia :-

Quote: Pundamilia07

Lisemwalo lipo, malalamiko hayawezi kutoka from nowhere. Ninachosema ni kuwa kuna tatizo, tena ni tatizo la kiitikadi za kisiasa, hasa baina ya CHADEMA na CCM. Angalia kwa makini kuwa hoja yeyote ambayo ni pro-serikali ya chama tawala hapa JF haina maana hata kama ni nzuri. Na hoja yeyote inayohusu CHADEMA hata kama haina maslahi yeyote ya kitaifa basi itakuzwa na kutukuzwa.Sasa haya na mambo mengine ni vitu vya kuhoji kama hii Forum ina wenyewe na ni vipi baadhi ya wana-JF wanakuwa na sauti na mamlaka zaidi ya wengine, je ni kwa namna gani? hayo ndiyo mambo ambayo yamekuwa yakiumiza vichwa vya baadhi ya wana-JF.
Suluhisho siyo kuwafungia, busara ni lazima itumike hasa ukizingatia kuwa hatupigi kura hapa kuwachagua hao MODs kwani hatujui wengine ni watu wenye uwezo na tabia za namna gani.
__________________
Toa boriti ndani ya jicho lako kabla hujaelekeza kidole kwa mwenzio
 
Mimi si mwana-CCM wala CHADEMA. Inapofikia issue ya kitaifa sitaona aibu kutimiza wajibu kuitetea nchi yangu. Ikibidi kumpongeza Rais nitafanya hivyo kwa kujali utaifa wangu.

Kwa hiyo unataka kusema hapo unaitetea nchi siyo? We acha bana. Mafisadi walishaiteka nchi hata Said Mwema alishasema hiko kitu. Hivi unawezaje kusema JK anstahili sifa kwa kuwasamehe mafisadi??? Hivi inaingia akilini kumkamata mwizi kisha kumwambia nirudishie ulichokwiba kisha kumwacha awe huru. Haijalishi kama wezi wa EPA wamerudisha kiasi gani, suala hapa ni kuwawajibisha kama wezi wengine. Nahis IMF ama nao hawajapata habari kamili au JK kawadanganya.Narudia tean, Kosa haliwezi kutokuwa kosa kwa vile mwizi kakurudishia alichokwiba. Hapo ndipo tunapokuona nawewe hujaatazama vizuri hii sakata la EPA, therefore JK hastahili pongezi. He should have done more than what he has done hata kama analinda sana haki za binadamu[/QUOTE]

Kwa hiyo unataka kusema hapo unaitetea nchi siyo?
Sidhani kama ninahitaji kurudia kama umeelewa, nitarudia endapo tu kama utaniambia hujaelewa.

Mafisadi walishaiteka nchi hata Said Mwema alishasema hiko kitu.
Huenda hata Said akisoma hapa utamchana mbavu!

Hivi unawezaje kusema JK anstahili sifa kwa kuwasamehe mafisadi???
Sifa ambayo tumepewa watu weusi ni kuwa ukitaka kumficha jambo basi liweke kwenye maadiko kwani huwa sisi si wasomaji.
Unachokiuliza tayari nimekiandika hapo awali, tafadhali rudi nyuma na usome ili uchangie vizuri.
 
Kama tungekuwa na bunge makini lisilo na wababishaji na wezi wengi ndani yake. Wangemuondoa JK kwa kura ya kutokuwa na imani naye lakini kwa mtindo wa kwetu Tz anashangiliwa kwa kuvunja sheria na katiba yetu. Ajabu sana!
 
Kingunge azidi kukosolewa

na Deogratius Temba


WANASIASA na wanaharakati wa haki za binadamu, wamemkosoa mwanasiasa mkongwe na kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kingunge Ngombale - Mwiru, kuwa matamshi yake yanachafua upepo wa kisiasa nchini na hayana ukweli kwa wananchi kwa vile yanalenga kutetea ufisadi ndani ya chama hicho. Wamemtaka afahamu kuwa Watanzania wanajua kuwa ndani ya chama hicho kuna ufisadi unaoibuliwa sasa na wabunge wa vyama vya upinzani, na hapaswi kuwatisha wabunge wa CCM wanaochukia ufisadi.

Kauli hizo zimekuja baada ya Kingunge kupokea maandamano yaliyoandaliwa na CCM, Mkoa wa Dodoma juzi, kwa lengo la kupongeza hotuba ya Rais Jakaya Kikwete aliyoitoa bungeni mwishoni mwa wiki iliyopita. Akizungumza kwa mahojiano maalumu na Tanznaia Daima Jumapili, Mhadhili wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Mwesiga Baregu, alisema Kingunge anapaswa kutulia kwa kuwa ameshazeeka.

“Kingunge ameshindwa kuonyesha mapenzi kwa nchi hii na Watanzania, atajikuta hata kwa chama chake hana mapenzi, kwa sababu atachangia kuiua CCM. Kwa jinsi anavyotetea uongo hadharani wakati akijua kuwa hata watoto wadogo wanajua kuwa kuna ufisadi ndani ya chama hicho,” alisema Prof. Baregu. Alisema kiongozi wa zamani kama Kingunge, anapaswa kuwa makini na matamshi yake ili kulinda heshima yake badala ua kuropoka na kukitetea chama ambacho kimeshapoteza mwelekeo, heshima, maadili na kugubikwa na rushwa kila mahali.

Alimuasa Kingunge kuwa na mapenzi na maisha ya Watanzania na taifa kwanza kabla ya chama chake, kwa sababu Watanzania ni watu na wanahitaji kulindwa. Akizungumzia maandamano ya kuunga mkono hotuba ya Rais Kikwete, alisema wananchi wanasukumwa kuandamana na watu wenye vijisenti. Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Wilfred Lwakatare, kwa upande wake alisema Kingunge ana mawazo ya kizamani na hapaswi kuendelea kutoa michango ya mawazo kwa sasa kwa vile akili yake imechoka na haiendani na wakati huu wa mabadiliko ya kisiasa na mfumo wa vyama vingi.

“Asijidhalilishe kwa kutokwenda na wakati, anyamaze kimya, hakuna atakayemlazimisha kuongea, hakitakii mema chama chake, anasaidia kukiua kwa kauli zake,” alisema Lwakatare. Alisema kila Mtanzania anafahamu kuwa kero na maovu yote ya serikali ya CCM yameibuliwa na wapinzani bungeni, lakini CCM inachanganyikiwa na kupora hoja hizo huku ikijigamba kuwa imeziibua. Lwakatare alisema Kingunge anasahau kuwa hata Spika wa Bunge, Samuel Sitta na wabunge wengine ndani ya chama hicho, sasa wanakiri kuwa serikali imeshindwa kuwadhibiti mafisadi. Mkurugenzi wa Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA), Ananilea Nkya, alisema watu kuandamana ni tatizo ambalo limesababishwa na serikali kuruhusu mtu mmoja kuwa na fedha nyingi kupita kiasi, hivyo kuwa na uwezo wa kununua watu na kuwafanya waandamane.

“Serikali imebana pesa kwa raia wa kipato cha chini, wachache wanayo mabilioni, wanakuwa na jeuri ya kununua watu wengine, wanakuwa na uwezo wa kufanya chochote katika nchi. “Siamini kama Watanzania ni watu kidogo vile kama hao wanaoandamana, ninachojua ni kwamba ufisadi una nguvu ya kufanya chochote. Rais anawaogopa hawa kwa sababu ya kiasi cha fedha walizonazo. Hayati Mwalimu Nyerere hakukubali hata siku moja mtu mmoja kumiliki fedha kiasi hicho ambacho mafisadi wanamiliki sasa,” alisema Nkya.
Nkya alisema kuwa umefika wakati sasa kwa Watanzania wote kuuliza kwanini watu wanampinga rais waziwazi, na kila mtu ajitahidi kusikiliza hotuba za viongozi na azichambue na kujua nini kinaendelea ili kuepuka kudanganywa na mafisadi.

Kingunge akihutubia waandamanaji wachache mjini Dodoma juzi, alisema wapinzani wanataka umaarufu kwa kutumia kashfa na aliwakemea wabunge wa CCM ambao wamekuwa wakiunga mkono sera za wapinzani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…