Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,842
- 31,073
Kwani hujui kuwa hiko chama kinasomeka kwa aka Chama cha Mauaji?Kwa kashifa nziito aliyokuwa nayo Madabida ya ARV feki,watu wamekufa kwa kupewa dawa feki,sikutegemea kama angekuwa na madaraka yoyote ndani ya Chama,lakini hiyo ndiyo CCM......hiyo ndiyo Tanzania.
Ndiyo maana hawaonagi taabu, wakishirikiana na policcm, kurusha mabomu ya machozi na wakati mwingine hadi kutumia risasi za moto, kwenye maandamano ya vyama vya upinzani, hususani Chadema na CUF, kama ambavyo walivyomuua Daudi Mwangosi, kule Mufindi İringa na kama vile walivyowalipua wa mabomu wafuasi wa Chadema hadi kusababisha vifo, kwenye mkutano wa amani wa Chadema huko Soweto Arusha.
Vile vile kama mauaji ya wafuasi wa CUF kule Pemba miaka 14 iliyopita, ambapo Tanzania kwa mara ya kwanza katika historia yake iliweza kuzalisha wakimbizi, waliokimbilia Mombasa Kenya.