CHADEMA
Political Party
- Apr 13, 2013
- 495
- 2,539
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kitakuwa na kikao cha Kanda ya Kusini ambacho hotuba ya ufunguzi itatolewa na NKMB JJ Mnyika, leo kuanzia saa 10.00 asubuhi Ukumbi wa, karibu na Maisha Club. kesho pia atafanya mkutano mkubwa hapo Mtwara Mjini kuanzia saa 8 mchana.
Ziara hiyo ni mwendelezo wa maboresho ya Kanda za Chama ikiwa ni maandalizi kuelekea uchaguzi Mkuu..
Ziara hiyo ni mwendelezo wa maboresho ya Kanda za Chama ikiwa ni maandalizi kuelekea uchaguzi Mkuu..
Ziara ya kanda ya Kusini itakuwa inahitimisha ziara za maboresho ya kanda nane za Tanganyika zilizo anza tangu mwezi Februari ikiwa ni azimio la Kamati kuu la kuziboresha kanda nane za kichama za Tanganyika kabla kuelekea Zanzibar na kuboresha kanda mbili za upande wa visiwani.
Vikao vya kanda ya Kusini vitakuwa vitatu.
1. Kikao cha Kamati tendaji ya kanda
2. Kikao cha baraza la uongozi la kanda.
3. Kikao cha wadau wa kanda ya Kusini
Vikao Kama hivyo vimeshafanyika kwenye kanda nyingine saba za Tanganyika ambazo ni.
1. Pwani (DSM na Pwani)
2. Serengeti (Shinyanga, Mara na Simiyu)
3. Kati (Dodoma, Singida na Morogoro)
4. Kaskazini (kilimanjaro , Tanga, Arusha na Manyara)
5. Juu Kusini (Mbeya , Iringa, Njombe, Rukwa na Ruvuma)
6. Victoria (mwanza , Kagera na Geita)
7. Magharibi (Kigoma , Tabora na Katavi ).
Mfumo wetu wa kanda umekuwa mfumo bora wa kuishii sera yetu ya majimbo na falsafa ya ugatuzi wa madaraka (decentralization).
Kila kanda ya kichama imewezeshwa kwa kuwa na makao makuu ya kisasa pamoja na Gari na pikipiki mpya zaidi 50 ili kuwezesha kazi za kisiasa kwenye kanda husika.