Mnyambuliko wa vitenzi

Mnyambuliko wa vitenzi

pkjag

Member
Joined
Jan 2, 2015
Posts
85
Reaction score
36
Hebu niwaulize nimeshuhudia utumizi wa mnyambuliko wa vitenzi ambao mwalimu wangu aliniambia sio sahihi. Hivi kukujaga ama kukujanga ni sahihi kwa sababu lugha nyingi za kibantu zina mfumo huo huo wa kunyambua vitenzi lakini kiswahili hakuna ama hauruhusiwi na waandishi wengi ambao nimesoma vitabu vyao na hakuna mnyambuliko wowote kama huo. Ila mfumo huu ni kawaida sana katika mazungumzo na je ulitokea wapi kwanza, kwasababu wakenya hutumia -nga na watz wanatumia -ga?
 
Kwa tanzania ni -ga. Ila sasa kwa kenya wakikuyu na wakamba wanashindwa -ga na kuitamka -nga. Makabila
haya hushindwa pia kutamka thelathini, utasikia dheladhini nk.
 
Hapo kitenzi ni 'kuja',mzizi ni '-j-' sasa kiambishi awali 'ku-' na tamati '-nga'(Kenya) na '-ga-'(Tanzania) naona vyote ni vya kilahaja.Tabia ya kuongeza vitamkwa kama nakujapo,nimekusalimiaga n.k inatumika kama misimu au lahaja za sehemu fulanifulani.Siamini kama kiswahili sanifu kinakubali uambishaji na unyambulishaji wa namna hyo.
 
Hebu niwaulize nimeshuhudia utumizi wa mnyambuliko wa vitenzi ambao mwalimu wangu aliniambia sio sahihi. Hivi kukujaga ama kukujanga ni sahihi kwa sababu lugha nyingi za kibantu zina mfumo huo huo wa kunyambua vitenzi lakini kiswahili hakuna ama hauruhusiwi na waandishi wengi ambao nimesoma vitabu vyao na hakuna mnyambuliko wowote kama huo. Ila mfumo huu ni kawaida sana katika mazungumzo na je ulitokea wapi kwanza, kwasababu wakenya hutumia -nga na watz wanatumia -ga?

Lugha ya mazungumzo ina tabia ya kukiuka kanuni za kisarufi na kileksika maana inatumiwa na watu tofauti tofauti.Ila inapowekwa katika maandishi lazima izifuate kanuni hizo.Unyambulishaji wa aina hyo huwezi kujua ulipotokea,maana unaweza kutokezwa na mtu mmoja kama kasumba ikageuka tabia ya eneo fulani.Mtazamo wangu tu!
 
Back
Top Bottom