'Mnyalu' wa UDSM: Muuza karatasi aliyetumia fursa

Kipilipili

JF-Expert Member
May 25, 2010
2,272
1,882
Habari!

Kwa wale waliowahi kusoma UDSM (Mlimani) miaka ya nyuma huenda wanamkumbuka huyu kijana "sharobaro" muuza karatasi ambaye inadaiwa ni "mnyalu" kutoka kule Iringa.

Alichokuwa anafanya ni kununua rimu kisha anabana karatasi 4 au 5 na kisha anauza kwa sh 100 (kwa wakati huo, sijui sasa kama bado anauza).

Wengi walimchukulia kama "muhuni" flani mganga njaa lakini mimi namtazama kama mjasiriamali alieiona fursa na kuitumia tena katika jumuia ya wasomi ambao wengi wao hawakuiona kama ni fursa au kama waliiona basi waliidharau na kuona kuwa wao ni wasomi hawawezi kufanya biashara "kichaa" kama ile.

Tumfanyie makadirio madogo;

Bei ya Rimu 1 aina ya MONDI = 6000
Rimu ina karatasi 500
Yeye anabana karatasi 4
Hivyo 500÷4=125 bundles
1 bundle=100Tsh
125 bundlesX100=12500 Tsh (mauzo)

Faida; 12500-6000=6500TSH(faida ya rimu moja tu)

Je akiuza rimu mbili kila siku kwa mwezi atakuwa na faida ya sh ngapi?
6500tsh X2 X5(working days) X4 Weeks=260,000Tsh

Tunajifunza nini kutoka kwa bwana "mnyalu"?? Mnyalu hana degree kama walivyo wengi wa wateja wake, wengine wana masters na hata Phd lakini mnyalu ameona fursa ndogo na kuitumia.

Je ni graduates wangapi wako mtaani wanashinda kuangalia TV kwa kisingizio cha kukosa ajira na hawaingizi hata alfu 10 kwa mwezi? jibu ni rahisi: HAWAWEZI KUFANYA KAZI HIYO kwa sababu si status yao, wao wana degree!!

Graduates wakiacha superiority complex waliyonayo basi nina hakika Macho yao YATAFUNGUKA na kuona Fursa nyingi zinazowazunguka ambazo nyingine hazihitaji mtaji mkubwa. Huu ni mfano tu mdogo kutoka kwa bwana "mnyalu", vipo vingi ambavyo graduates wanaweza kuvifanya individually au in groups

Ukiwa gradute unaweza kuiboresha wazo la biashara anayoifanya "mnyalu" na kulifanya kuwa ni wazo bora likakuingizia kipato zaidi.

Mfano:

1. Chukua begi lako la mgongoni ulilokuwa unatumia chuo
2. Chukua kiwi na brash unayoitumia kung'arisha viatu vyako
3. Nunua rimu mbili
4. Nunua staple machine ndogo
5. Nunua box la kalamu ya blue na nyeusi
6. Nunua karanga kg1, kaanga na funga kwenye vipakiti
7. Nunua BIG G/PK
8. Nenda ofisi za Tigo na ungainishe line yako na huduma ya kuuza Tigo Rusha (kuunganishwa ni bure)....uza Tigo Rusha

Weka vitu vyote kwenye begi na zunguka maeneo ya chuo na anza kutoa huduma.

Mtaji ukikua nunua mashine ya KUPIMA UZITO, weka kwenye bag na anza kutoa huduma....believe me wadada wanapenda sana kupima uzito ili kudhibiti miili yao isinenepe hovyo.

Kwa kifupi utakuwa unauza vocha, kung'arisha viatu vya wanafunzi, kuuza bites, kuuza kalamu na karatasi, kupima uzito n.k.

Je kwa mwezi utakuwa unaingiza kiasi gani??

Jitahidi kujenga uhusiano mzuri na wateja wako, ikiwezekana tengeneza business card ioneshe kiwango chako cha elimu, believe me utapata connection humo humo kutoka kwa wateja wako mana wengine wana makampuni yao na watavutika tu na uthubutu wako na wangependa ufanye nao kazi.

Biashara hii mtaji wake ni MDOGO SANA. Ondoa aibu, Superiority complex na acha kukaa nyumbani bila kazi..
 
Mnyalu huwa anapata hela hafu unachukua karatasi unaweka hela pale. Ile ni good idea yake sema huwa mwanausalama pale chuoni.

All in all wazo zuri sana hili sio hata kwa style ya mnyalu mtu unaweza uka create biashara simple kwa kuangalia sehemu ulipo na fursa zipi hazipo then unaanzisha mdogo mdogo. Kuna watu na wajua walianza na biashara ndogo sasa hvi wako mbali. Kikubwa ni kutokata tamaa na kuwa na vision.
 
Duh..good idea..ila hii itawezekana 2040 kila mtu akishakuwa graduate..kwa sasa hivi graduates ni wachache na wana"abudiwa" na jamii kwa hivyo hawawezi kuwa na guts za kufanya haya mambo..wako radhi kula kwa shemeji..
 
Duh..good idea..ila hii itawezekana 2040 kila mtu akishakuwa graduate..kwa sasa hivi graduates ni wachache na wana"abudiwa" na jamii kwa hivyo hawawezi kuwa na guts za kufanya haya mambo..wako radhi kula kwa shemeji..

If you could be writting this twenty years ago ningekuelewa, not today.
 
Mnyalu huwa anapata hela hafu unachukua karatasi unaweka hela pale. Ile ni good idea yake sema huwa mwanausalama pale chuoni.

All in all wazo zuri sana hili sio hata kwa style ya mnyalu mtu unaweza uka create biashara simple kwa kuangalia sehemu ulipo na fursa zipi hazipo then unaanzisha mdogo mdogo. Kuna watu na wajua walianza na biashara ndogo sasa hvi wako mbali. Kikubwa ni kutokata tamaa na kuwa na vision.

Perfect..... ni kweli kabisa na mimi nimeleta mfano wa mnyalu ili jamii ifunguke macho si tu wafanye biashara hii ila wajifunze kufumbua macho kuangalia fursa katika mazingira yanayowazunguka.

swali la kizushi:Hivi bado mnyalu yupo hadi Leo UDSM ?
 
Duh..good idea..ila hii itawezekana 2040 kila mtu akishakuwa graduate..kwa sasa hivi graduates ni wachache na wana"abudiwa" na jamii kwa hivyo hawawezi kuwa na guts za kufanya haya mambo..wako radhi kula kwa shemeji..

Elimu haijawakomboa bado. Waache waendelee kula kwa shemeji, ni hapo dada atakapoachwa ndipo watatia akili!
 
Perfect..... ni kweli kabisa na mimi nimeleta mfano wa mnyalu ili jamii ifunguke macho si tu wafanye biashara hii ila wajifunze kufumbua macho kuangalia fursa katika mazingira yanayowazunguka.

swali la kizushi:Hivi bado mnyalu yupo hadi Leo UDSM ?
Maisha yanaweza kuwa ma rahisi mtu ukitoa uoga na kudhubutu kufanya jambo lolote bila kukata tamaa. Lazma ufike mbali uoga wa watu ndo umaskini wa wengi.
Mnyalu bado yupo chuoni haondokagi watu hudai ni mwana usalama mana hata mambo ya ndani kuhusu chuo yeye ndo huwa wa kwanza kuyajua.
 
Maisha yanaweza kuwa ma rahisi mtu ukitoa uoga na kudhubutu kufanya jambo lolote bila kukata tamaa. Lazma ufike mbali uoga wa watu ndo umaskini wa wengi.
Mnyalu bado yupo chuoni haondokagi watu hudai ni mwana usalama mana hata mambo ya ndani kuhusu chuo yeye ndo huwa wa kwanza kuyajua.

Haahha...hilo la "usalama" ngoja tuliwache kiusalama uli tuwe salama.
Kingine ni kuwa jamaa ana good customer care, anajuwa kudeal na wateja wake. Na huwa anapendwa sana na wateja wake.
Japo kuna maneno ya chini chini kuwa kina dada wanampenda sana ila hayo si mahala pake hapa. Hoja ni kuwa ana good customer care skills ambayo ni nguzo muhimu sana katika biashara
 
Haahha...hilo la "usalama" ngoja tuliwache kiusalama uli tuwe salama.
Kingine ni kuwa jamaa ana good customer care, anajuwa kudeal na wateja wake. Na huwa anapendwa sana na wateja wake.
Japo kuna maneno ya chini chini kuwa kina dada wanampenda sana ila hayo si mahala pake hapa. Hoja ni kuwa ana good customer care skills ambayo ni nguzo muhimu sana katika biashara
Kweli kwenye customer care yuko vizuri sana na ni nguzo muhimu kwa biashara yoyote kitu ambacho naona Wabongo, wengi kinawasumbua ni customer care nzuri.
Mnyalu yeye zake huwa anapenda kutania sana wadada, na watu wamemzoea,kiasi kwamba huwa anaacha karatasi na box pembeni unachukua karatasi au Penn unaweka hela kwenye box na watu hufanya kwa uaminifu.Nadhani uongeaji mzuri na watu umemsaidia sana mfano kipindi cha UE huchukua chumba kidogo kule kwenye lecture za yombo anawahifadhia wadada mikoba yao cmu kwa kuwatoza mia tano, na ukiacha kitu after exams una vikuta safe.
Good customer care
Na uaminifu
Ni nguzo kwenye bussiness yoyote.
 
Kweli kwenye customer care yuko vizuri sana na ni nguzo muhimu kwa biashara yoyote kitu ambacho naona Wabongo, wengi kinawasumbua ni customer care nzuri.
Mnyalu yeye zake huwa anapenda kutania sana wadada, na watu wamemzoea,kiasi kwamba huwa anaacha karatasi na box pembeni unachukua karatasi au Penn unaweka hela kwenye box na watu hufanya kwa uaminifu.Nadhani uongeaji mzuri na watu umemsaidia sana mfano kipindi cha UE huchukua chumba kidogo kule kwenye lecture za yombo anawahifadhia wadada mikoba yao cmu kwa kuwatoza mia tano, na ukiacha kitu after exams una vikuta safe.
Good customer care
Na uaminifu
Ni nguzo kwenye bussiness yoyote.

I see....nimeipenda sana hiyo. Amepiga hatua kubwa sana siku hizi. Uaminifu unampa nafasi ya kuingiza pesa zaidi! Imagine kila mkoba Tsh 500! Na kipindi cha mtihani mikoba hairuhusiwi kwa hiyo kwa siku akihifadhi mikoba 50 tu asubuhi mpaka jion ana kama 25,000 hii ni siku moja tu. nasikia yombo kuna majengo mapya,enzi zetu hayakuwepo ,kwa hiyo atakuwa anavuna hasa pesa!Angekaa nyumbani asingezipata fursa zote hizo!!
 
Kweli kwenye customer care yuko vizuri sana na ni nguzo muhimu kwa biashara yoyote kitu ambacho naona Wabongo, wengi kinawasumbua ni customer care nzuri.
Mnyalu yeye zake huwa anapenda kutania sana wadada, na watu wamemzoea,kiasi kwamba huwa anaacha karatasi na box pembeni unachukua karatasi au Penn unaweka hela kwenye box na watu hufanya kwa uaminifu.Nadhani uongeaji mzuri na watu umemsaidia sana mfano kipindi cha UE huchukua chumba kidogo kule kwenye lecture za yombo anawahifadhia wadada mikoba yao cmu kwa kuwatoza mia tano, na ukiacha kitu after exams una vikuta safe.
Good customer care
Na uaminifu
Ni nguzo kwenye bussiness yoyote.

Huyo jamaa aisee nampa Salute. Kuna vitu nimejifunza hapo
 
I see....nimeipenda sana hiyo. Amepiga hatua kubwa sana siku hizi. Uaminifu unampa nafasi ya kuingiza pesa zaidi! Imagine kila mkoba Tsh 500! Na kipindi cha mtihani mikoba hairuhusiwi kwa hiyo kwa siku akihifadhi mikoba 50 tu asubuhi mpaka jion ana kama 25,000 hii ni siku moja tu. nasikia yombo kuna majengo mapya,enzi zetu hayakuwepo ,kwa hiyo atakuwa anavuna hasa pesa!Angekaa nyumbani asingezipata fursa zote hizo!!
Anapata hela aisee nyingi tu kwa siku na siku hizi kuna lectures mpya za Yombo 4 na five zinaweza kuchukua wanafunzi zaidi ya elfu moja ndo kubwa kwa chuo. Hizo ndo maskani yake na anapata wateja mana hzo ndo lectures room kubwa zenye kutumiwa na wanafunzi wengi kwa wakati mmoja chuoni.
 
Maisha yanaweza kuwa ma rahisi mtu ukitoa uoga na kudhubutu kufanya jambo lolote bila kukata tamaa. Lazma ufike mbali uoga wa watu ndo umaskini wa wengi.
Mnyalu bado yupo chuoni haondokagi watu hudai ni mwana usalama mana hata mambo ya ndani kuhusu chuo yeye ndo huwa wa kwanza kuyajua.

Wakati mwingine ugumu wa maisha tumeutengeneza wenyewe kwa slogan iliyozoeleka kila pembe ya nchi "MAISHA MAGUMU KWELI AISEE", watu tunaishi ili kuliridhisha nafsi za watu wengine kwamba nikifanya hivi watanionaje wanaonifahamu huku ela huku ile ela inayotokana na ile kazi unaitaka (wengi wamejipa hadhi ambazo sio za kwao ndio maana unamkuta mtu yupo vizuri kwa mwonekano anapiga mizinga tu huku kazi zingine anaona sio hadhi yake wakati yupo APECHE ARORO, tena wengine unakuta anabeba na chuma kabisa jioni alafu anaenda kula ugali wa shikamoo na ukimwambia abebe gunia la mkaa alipwe buku anaweza kukutoa macho wakati hapo zile nguvu alizokuwa anazitumia kubeba chuma angezitumia kwenye gunia la mkaa angekuwa anaua ndege wawili kwa jiwe moja yaani mazoezi na kuingiza kipato jioni badala ya kubeba chuma anafanya mazoezi ya kujinyoosha tu)
 
Mnyalu huwa anapata hela hafu unachukua karatasi unaweka hela pale. Ile ni good idea yake sema huwa mwanausalama pale chuoni.

All in all wazo zuri sana hili sio hata kwa style ya mnyalu mtu unaweza uka create biashara simple kwa kuangalia sehemu ulipo na fursa zipi hazipo then unaanzisha mdogo mdogo. Kuna watu na wajua walianza na biashara ndogo sasa hvi wako mbali. Kikubwa ni kutokata tamaa na kuwa na vision.

Hivi Mnyalu ndio yule jamaa mwenye dreds,nakumbuka tulivyokua first ur alikua anapenda sana kuja theatre 1&2 anatuchekesha kinoma , he z so charming
 
mbona madem anawap bure;kuna dy niko yombo pale kaja dem anajichekesha akachukua karatas km 4 n pen huyo akasepa
huy jamaa hayuko seriuz ndo maana pia hatoboi
 
Back
Top Bottom