Mnawezaje kurudiana na 'EX' zenu?

Mnawezaje kurudiana na 'EX' zenu?

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
969
Reaction score
1,939
Katika kitu kimenishindaga kwenye mahusiano ni kurudiana na ex wangu yeyote yule. Mimi roho yangu ni ndogo sana mtu akinikosea huwa inaniwia vigumu kumsamehe na kurudiana nae.

Niliwahi kujaribu lakini tulikutana tu mara moja nikagundua sina hisia nae tena wala mapenzi hakuna.
 
Katika kitu kimenishindaga kwenye mahusiano ni kurudiana na ex wangu yeyote yule. Mimi roho yangu ni ndogo sana mtu akinikosea huwa inaniwia vigumu kumsamehe na kurudiana nae. Niliwahi kujaribu lakini tulikutana tu mara moja nikagundua sina hisia nae tena wala mapenzi hakuna.
Inategemea mliachanaje mkuu!

kuna ile mnaachana kama hamjaachana vile.. hii rahisi sana hata kupiga mechi za kirafiki..

Kuna ile mnaachana standard hii ina nafasi ya kurudiani ( kuna mahala mnashindwa kukubaliana, mnaamua kila mtu apite kushoto )

Kuna ile mnaachana kwasababu ya watu

kuna kuachana kwa vita hii nadra sana kurudiana japo hutokea

kuna kuachana kwa kuuana, na kuwindana hii haiwezekani kurudiana maana ukifanya kistake unaliwa kichwa..

EX huwa anakuwa mtamu kinoma, hasa kwenye part ya maongezi wakati unamkomesha
 
Katika kitu kimenishindaga kwenye mahusiano ni kurudiana na ex wangu yeyote yule. Mimi roho yangu ni ndogo sana mtu akinikosea huwa inaniwia vigumu kumsamehe na kurudiana nae.

Niliwahi kujaribu lakini tulikutana tu mara moja nikagundua sina hisia nae tena wala mapenzi hakuna.
Kama una roho ya aina hiyo, ndoa itakushinda. Kumbuka huyo mtakayefunga ndoa ni mpaka golgota. Lakini kukwazana kupo pale pale na kitu muhimu katika ndoa ni kusameheana.
 
hauko pekeyako mkuu, unanguvu flan ya asili inayokuongoza kutokutegemea vilivyopita yaan unakuwa excited na vi2 vipya vipya2 ko hata kwenye aspect yngne nje na mahusiano upo hvo, ogopa sana m2 asiyesamehe ila anapotezea2.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom