Mnaozindika nyumba

Mnaozindika nyumba

KakaJambazi

JF-Expert Member
Joined
Jun 5, 2009
Posts
18,830
Reaction score
12,291
Nilikua nasikia kuwa wanaojenga nyumba mara nyingi huwa wanazizindika, sijui kuchimbia madude gani ili mchawi ashindwe kuroga.

Mimi yangu inakaribia kwisha kwisha kabisa na sijawahi kufanya huo upuuzi na sijafa, hii inakuaje!
 
Nilikua nasikia kuwa wanaojenga nyumba mara nyingi huwa wanazizindika, sijui kuchimbia madude gani ili mchawi ashindwe kuroga.
Mi yangu inakaribia kwisha kwisha kabisa na sijawahi kufanya huo upuuzi na sijafa, hii inakuaje!
"Watu wangu mnaangamia kwa kukosa maarifa"
Mkuu ushirikina haujawahi kumpa mtu furaha wala kumwongezea maisha.
 
Uwasilishaji wako wa hoja husika ni kama vile unaomba muongozo ni namna gani nawe pia waweza fanya huu uzuzu usio na tija(kwa kuzingatia kuwa nawe pia unakaribia kukamilisha nyumba yako)........Ndugu epa mbali kabisa na hili tendo,ni mara elfu ukamtafuta kiongozi wako wa imani akubarikie nyumba yako na si vingine!

Kuzindika nyumba ni sawa na kuwasha green light kwa mashambulizi ya kishirikina,maana hii inaashirikia imani haba.

CHOCHONDENDE USIJARIBU HUU UZUZU!!
 
Mwite mchungaji kabla ya kuhamia uiweke wakfu
Achana na mazindiko hayana faida yoyote..
 
Mkuu tafuta kiongozi wa dini yako apige dua/sala kisha hamia. Wachana na utapeli utawekewa mapepo kwenye nyumba yako na hutaishi kwa amani.

Kama huamini zindika uone mabalaa yatakavyopanga foleni kisha utaichukia nyumba yako na kuihama mwenyewe bila kulazimishwa na mtu!
 
Nilikua nasikia kuwa wanaojenga nyumba mara nyingi huwa wanazizindika, sijui kuchimbia madude gani ili mchawi ashindwe kuroga.
Mi yangu inakaribia kwisha kwisha kabisa na sijawahi kufanya huo upuuzi na sijafa, hii inakuaje!

uchawi haupo, we endelea na maisha yako...unless labda ulitaka tujue kwamba unamalizia nyumba yako!!
 
Nilikua nasikia kuwa wanaojenga nyumba mara nyingi huwa wanazizindika, sijui kuchimbia madude gani ili mchawi ashindwe kuroga.
Mi yangu inakaribia kwisha kwisha kabisa na sijawahi kufanya huo upuuzi na sijafa, hii inakuaje!

...kwa kauli hii tayari moyo wako umezindikwa...
 
Mbona hatamimi sijazindika nyumbayangu mpaka leo naishi vizuri ukimwamini mungu uchawi hauna nafasi

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Pole kwa kuwa na imani haba. Uchawi upo kwa wakristu hata biblia imesema. Sijui wasislamu wanasemaje. Njia nzuri ya kuzindika nyumba kama wewe ni mkristu ni kuiwekea wakfu kama alivyosema mjumbe mmoja hapo juu. Kwa wakatoliki imara. Ibariki nyumba yako kwa kununyizia maji ya Baraka. Yale maji ni kinga kubwa kwa kuwa yamechanganywa na chumvi. Hata aje mshenzi kutoka uarabuni akifika kwako ataishia kupiga story na kuondoka.
 
kweli kabisa....na hasa ukizingatia chumvi ni kinga tosha kwa mambo mabaya ya kishirikina.
Pole kwa kuwa na imani haba. Uchawi upo kwa wakristu hata biblia imesema. Sijui wasislamu wanasemaje. Njia nzuri ya kuzindika nyumba kama wewe ni mkristu ni kuiwekea wakfu kama alivyosema mjumbe mmoja hapo juu. Kwa wakatoliki imara. Ibariki nyumba yako kwa kununyizia maji ya Baraka. Yale maji ni kinga kubwa kwa kuwa yamechanganywa na chumvi. Hata aje mshenzi kutoka uarabuni akifika kwako ataishia kupiga story na kuondoka.
 
Nijuavyo mimi ni bora utafute kiongozi wako wadini aibariki nyumba yako basi
 
Nilikua nasikia kuwa wanaojenga nyumba mara nyingi huwa wanazizindika, sijui kuchimbia madude gani ili mchawi ashindwe kuroga.
Mi yangu inakaribia kwisha kwisha kabisa na sijawahi kufanya huo upuuzi na sijafa, hii inakuaje!

Kwanini usizindike account yako ya benki??labda miujiza itatokea.
 
Nilikua nasikia kuwa wanaojenga nyumba mara nyingi huwa wanazizindika, sijui kuchimbia madude gani ili mchawi ashindwe kuroga.
Mi yangu inakaribia kwisha kwisha kabisa na sijawahi kufanya huo upuuzi na sijafa, hii inakuaje!
Mkuu ila si bado hujahamia, hamia halafu ulete mrejesho.
 
Mbona hatamimi sijazindika nyumbayangu mpaka leo naishi vizuri ukimwamini mungu uchawi hauna nafasi

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Inategemea unaishi wapi! Nilisafiri siku moja na mfanyabiashara ya madini kutoka Arusha, nilipomdadisi kuhusu mauaji ya mara kwa mara huko Arusha, akanieleza kuwa ni kutokana na visasi katika biashara. Akazidi kunifahamisha kuwa visasi ni vingi Dar kuliko Arusha ila kwa Dar ukiwa na kisasi na mtu unamwendea kwa mganga lakini Arusha anakutwanga risasi.
 
nyumba utazindika ngapi? nyumba nyingine anapewa maelekezo mkandarasi anajenga kwa maelekezo nyumba inaisha na wapangaji wanaingia. huo ni upuuzi mtupu.
 
Back
Top Bottom